Thursday 29 October 2015

MAWAHHABI WAMDHALILISHA MTUME KUWA HAKUJIELEWA KUWA YEYE NI MTUME

MAWAHHABI WAMDHALILISHA MTUME KUWA HAKUJIELEWA KUWA YEYE NI MTUME
Waandishi wa kiwahhabi wameeleza suala la mwanzo wa wahyi kwa njia nyingi tofauti zenye kugongana. Tunakusudia kudondoa kilitokea nini kwa Mtume Muhammad (sa.w.w) baada ya kufikiwa na malaika Jibril kwa mara ya kwanza. Hapa tutajaribu kuzitaja chache tu:
a.  Khadija na Abubakr walimpeleka Muhammad (s.a.w.) kwa Waraqa bin Nawfal baada ya kuelezwa Waraqa kuwa Muhammad amepata matatizo, Waraqa akamuuliza Muhammad ana nini? Muhammad (s.a.w.) akamwambia: "Ninasikia ninaitwa nyuma yangu, ewe Muhammad, ewe Muhammad, nikisikia hivyo mimi hukimbia ovyo." Waraqa akamkataza asiwe anakimbia bali akaze roho ili ayasikie anayoambiwa..." Muhammad alishika maelekezo hayo, mara aliposikia akiitwa: Ewe Muhammad! Sema, Bismillahir Rahmanir Rahim, Alhamdulillahi rabbil a'lamina.... mpaka mwisho wa suratul Fatiha. Akaambiwa: Sema: "Laa ilaha illallahu" Muhammad (s.a.w.) baada ya hapo alikwenda kwa Waraqa bin Nawfal, akamjulisha hali hiyo. Waraqa akambashiria habari njema ya kuwa: "Hali kama hiyo alipewa pia Nabii Isa bin Maryam".
Tazama; Albidayatu Wannihaya J. 3 Uk. 9, Assiratun Nabawiyya J. 1 uk 83, Assiratul Halabiyya J. 1 uk 250, Siiratu Mughlataya uk, 15.
b.  Khadija alipompeleka Muhammad (s.a.w.) kwa Waraqa na akamweleza yaliyomtokea. Waraqa alisema: "Huyu ni Nabii wa Umma huu, mwambie atulize moyo."
Tazama: Albidayatu Wannihaya J.3 uk, 12, Siiratu Ibn Hisham J. 1 uk. 238, Assiratul Halabiyya J. 1 Uk. 239.
c.   Khadija alimwambia Muhammad (s.a.w.) atakapokufikia huyo anayekusomesha, uniambie, Mtume (s.a.w.) alipofikiwa na hali hiyo akamjulisha mkewe. Khadija akampakata katika mapaja yake, kisha akavua shungi yake, mara Mtume (s.a.w.) akaona yule aliyemjia anaondoka haraka. Mtume akamjulisha mkewe hilo, Khadija akasema, "Huyo ni Malaika, na wala siyo shetani, basi kaza roho na furahi".
Tazama: Assiratul Halabiyya J. 1 Uk. 252.
d.  Waraqa bin Nawfal alimwambia Khadija: "Muulize Muhammad (s.a.w.), nani anaemjia! Ikiwa ni Malaika Mikaeli basi amemletea amani. Na ikiwa ni Malaika Jibril basi amemletea vita na mateka. Khadija Alipomuuliza Mtume (s.a.w.) akajibu: "Ni Jibril". Khadija akapiga uso wake.
Taz: Tarikhul Yaa'quby J. 2 Uk. 23.
e.  Khadija alipewa kipande cha karatasi na mganga mmoja ili ampe Muhammad (s.a.w.) kama hali hii (iliyomfikia Muhammad) inasababishwa na ugonjwa wa kichaa, basi atapona... Khadija aliporudi kwa mumewe akamkuta anasoma Qur'an, Khadija akamchukua akaenda naye kwa yule mganga, walipofika kwa mganga, akafunua mgongo wa Mtume akaona muhuri wa Utume uko kati ya mabega mawili!!!
Tazama: Tarikhul Khamisi J. 1 Uk. 284, Assiratul Halabiyya J. 1 Uk. 243, Assiratun Nabawiyya J. 1. Uk. 83.
f.    Muhammad (s.a.w.) alipofikiwa na hali hiyo (ya kujiwa na Malaika) alikuwa akipanda katika kilele cha mlima mrefu na akitaka kujitupa chini (ili afe).
Tazama: Almuswannaf J. 5 Uk. 323.
g.  Muhammad (s.a.w.) alirudi kwa mkewe (kutoka katika pango) akiwa nafuraha kubwa akamwambia mkewe: "Nataka kukueleza habari njema, mimi nimeona katika ndoto kuwa Jibril amenijulisha kwamba ametumwa na Mola wangu aje kwangu... Khadija akamwambia: "Furahi, wallahi Mwenyeezi Mungu hatakufanyia lolote ila lililokuwa la kheri... kisha Khadija akaenda kwa mganga wa kinasara, kuuliza uwezekano wa kumuona Jibril. Mganga alishangaa sana kusikia jina la Jibril katika nchi hiyo, kisha akasema kuwa: "Huyo ni Mjumbe wa Mwenyeezi Mungu..."
Taz: Albidayatu Wannihaya J. 3 Uk. 13.

Nadhani umejionea mwenyewe uzushi wa mawahhabi, masalafi na answari sunnah dhidi ya Mtume wetu. Watu waongo na wazushi kama hawa, hawawezi kuaacha waislamu wa kawaida wakiishi kwa amani mustarehe bila kuleta chokochoko.

Lakini sisi waislamu sahihi, yaani Mashia tunaamini kuwa Mtume alikuwa Mtume bado akiwa tumboni mwa mama yake. Hivyo alipozaliwa tu alijulikana kuwa ni Mtume na miujiza mingi ilifanyika katika utoto wake na ujana wake. Kabla ya kufikisha miaka 40 ambapo utume wake ulizinduliwa rasmi na kuanza kazi ya kuueneza Uislamu duniani.

Monday 19 October 2015

WAATHIRIKA WA KARBALA – AWN BIN JAAFAR IBN ABI TALIB (R.A)

WAATHIRIKA WA KARBALA – AWN BIN JAAFAR IBN ABI TALIB (R.A)
Aun ni mtoto wa Jaafar ibn Abi Talib (r.a) na Asma’a bint Amees (r.a)..
Alizaliwa ukimbizini Ethiopia (Uhabeshi) kwani baba yake yaani Jaafar alikuwa kiongozi wa wakimbizi wa kiislamu waliokimbilia Habash kutokana na dhuluma na mauaji waliokuwa akifanyiwa na makafiri wa Makkah wakati wa mwanzo wa Uislamu kutangazwa na Mtume Muhammad (s.a.w.w).
Uislamu ulipota nguvu baba wa Aun yaani Jaafar alirejea uarabuni na kwa kipindi hicho Mtume alikuwa amekwisha hamia Madinah. Miaka michache baadaye Jaafar aliongoza jeshi la waislamu katika mapambano yanayojulikana kama vita vya Mu’tah. Vita hivi vilikuwa vikali sana na waislamu wengi waliuawa ikiwa ni pamoja na kamanda wao, yaani Jaafar bin Abi Talib (r.a). Jaafar aliacha watoto wa kiume watatu yaani Awn, Muhammad na Abdullah.
Vijana hawa walifanana sana na mzee Abu Talib (r.a), hivyo Mtume Muhammad (s.a.w.w) na Imam Ally waliwapenda sana. Baadaye Imam Ally aliwaozesha mabinti wake. Ummu kulthumu aliolewa na Aun na Zainabu aliolewa na Muhammad. Hapa utagundua kuwa wale wanaosema kuwa Imam Ally waliwaozesha mabinti wake kwa Umar bin Khatab ni uongo na propaganda kwa minajiri ya kuwapotosha watu.
Awn aliendelea kuwa Mtiifu kwa Imam Ally kama imam wake wa kwanza, kisha akawa mtiifu kwa Imam Hassan kama imam wake wa pili na hatimaye akawa mtiifu kwa imam Hussein kama imam wake wa tatu. Awn alichinjwa pamoja na Mashia na Ahlulbayt wengine katika eneo la Karbala, Iraq, akipigana vita upande wa Mashia, yaani katika jeshi dogo la imam Hussein (a.s). Innalillahi wainna ilayhi rajiuun.
Source: Ashura Encyclopedia

By Jawad Muhaddithy 

Monday 12 October 2015

QURANI MUUJIZA WA MILELE QUR ANI WA MTUME (S.A.W)

QURANI MUUJIZA WA MILELE QUR ANI WA MTUME (S.A.W) 
Qur'ani ni muujiza wa Mtume (s.a.w) ulio hai na wa milele, kwani Qur'ani ndio kitabu pekee kutoka mbinguni ambacho utashi wa Mwenyezi Mungu ulitaka kibakie ni chenye kuhifadhiwa kutokana na mabadiliko, nyongeza, pia upungufu na kugeuzwa- pamoja na kukithiri kwa watu wenye nia na malengo ya kukibadilisha na wafanyao mipango ya kukizua na kukigeuza- ili kitabu hiki kiwe cha milele na katiba ya milele ya maisha hadi siku ya kiama, maadamu kuna mwanadamu anaye ishi juu ya ardhi hii na hilo ni kutokana na hukumu za hali ya juu zilizomo kwenye majalada yake mawili na mafunzo ya kiwango cha juu ambayo kuyatekeleza kwake yana mhakikishia mwanadamu saada na kumpatia maendeleo, kupea na kufikia kwenye daraja za juu mwanadamu huyo.
Hakika Qur'ani pamoja na kuwa ni kitabu cha kielimu, utamaduni hukumu, haki, maadili, adabu, siasa na uchumi, ni muujiza wa mbinguni na wa milele wenye athari kubwa ya kiroho na kimaaanawia ya hali ya juu, hakika kitabu hiki kiliwashinda wanafasaha wakubwa wa kiarabu waliokuwa na nyaraka au waandishi wa nyaraka saba zilizo kuwa zimetundikwa na kuwekwa kwenye kaaba tukufu, na hawakuweza kuleta mfano wa sura moja tu ya Qur'ani, bali kutokana na kushikwa na aibu walikuwa wakizitoa nyaraka walizo tundika juu ya kaaba kati ya zile nyaraka zao, na walifanya hivyo kutokana na kushindwa kwao na kudhalilika kwao, pia kutokana na aibu iliyo washika mbele ya Qur'ani ambayo ni muujiza katika fasaha na balagha yake na katika mfumo wake na utaratibu wake, na lau kama wangeliweza kuleta sura moja tu mfano wa Qur'ani kusinge kuwa na haja ya kutumia mapigano dhidi ya Uislamu na vile vita vibaya na vyenye kuangamiza ambavyo viliishia kuleta maafa kwao na waheshimiwa wao na watu wao na kuvunja utukufu na heshima zao na hadhi zao, pia utawala wao, na kuwavisha vazi la njaa, khofu, udhalili na taabu.
Hii ndio Qur'ani ambayo ni muujiza, na hiki ndio kitabu cha mbinguni cha milele, kitabu ambacho ndani yake kuna mambo yamfikishayo mwanadamu kwenye saada na maisha ya neema na raha, kitabu ambacho hueneza kheri na baraka kwa watu wote, na hutawanya amani na salama katika ardhi hii na katika nchii zote, kumepokelewa riwaya mbali mbali kuhusiana na ubora wa kujifunza kitabu hiki na kukisoma pia kukihifadhi na kutekeleza maamrisho yake, na kufanya matendo kwa mujibu wa maamrisho ya kitabu hicho na zingine nyingi ambazo zinazo muhimiza mwanadamu kukitilia umuhimu.