Thursday 29 October 2015

MAWAHHABI WAMDHALILISHA MTUME KUWA HAKUJIELEWA KUWA YEYE NI MTUME

MAWAHHABI WAMDHALILISHA MTUME KUWA HAKUJIELEWA KUWA YEYE NI MTUME
Waandishi wa kiwahhabi wameeleza suala la mwanzo wa wahyi kwa njia nyingi tofauti zenye kugongana. Tunakusudia kudondoa kilitokea nini kwa Mtume Muhammad (sa.w.w) baada ya kufikiwa na malaika Jibril kwa mara ya kwanza. Hapa tutajaribu kuzitaja chache tu:
a.  Khadija na Abubakr walimpeleka Muhammad (s.a.w.) kwa Waraqa bin Nawfal baada ya kuelezwa Waraqa kuwa Muhammad amepata matatizo, Waraqa akamuuliza Muhammad ana nini? Muhammad (s.a.w.) akamwambia: "Ninasikia ninaitwa nyuma yangu, ewe Muhammad, ewe Muhammad, nikisikia hivyo mimi hukimbia ovyo." Waraqa akamkataza asiwe anakimbia bali akaze roho ili ayasikie anayoambiwa..." Muhammad alishika maelekezo hayo, mara aliposikia akiitwa: Ewe Muhammad! Sema, Bismillahir Rahmanir Rahim, Alhamdulillahi rabbil a'lamina.... mpaka mwisho wa suratul Fatiha. Akaambiwa: Sema: "Laa ilaha illallahu" Muhammad (s.a.w.) baada ya hapo alikwenda kwa Waraqa bin Nawfal, akamjulisha hali hiyo. Waraqa akambashiria habari njema ya kuwa: "Hali kama hiyo alipewa pia Nabii Isa bin Maryam".
Tazama; Albidayatu Wannihaya J. 3 Uk. 9, Assiratun Nabawiyya J. 1 uk 83, Assiratul Halabiyya J. 1 uk 250, Siiratu Mughlataya uk, 15.
b.  Khadija alipompeleka Muhammad (s.a.w.) kwa Waraqa na akamweleza yaliyomtokea. Waraqa alisema: "Huyu ni Nabii wa Umma huu, mwambie atulize moyo."
Tazama: Albidayatu Wannihaya J.3 uk, 12, Siiratu Ibn Hisham J. 1 uk. 238, Assiratul Halabiyya J. 1 Uk. 239.
c.   Khadija alimwambia Muhammad (s.a.w.) atakapokufikia huyo anayekusomesha, uniambie, Mtume (s.a.w.) alipofikiwa na hali hiyo akamjulisha mkewe. Khadija akampakata katika mapaja yake, kisha akavua shungi yake, mara Mtume (s.a.w.) akaona yule aliyemjia anaondoka haraka. Mtume akamjulisha mkewe hilo, Khadija akasema, "Huyo ni Malaika, na wala siyo shetani, basi kaza roho na furahi".
Tazama: Assiratul Halabiyya J. 1 Uk. 252.
d.  Waraqa bin Nawfal alimwambia Khadija: "Muulize Muhammad (s.a.w.), nani anaemjia! Ikiwa ni Malaika Mikaeli basi amemletea amani. Na ikiwa ni Malaika Jibril basi amemletea vita na mateka. Khadija Alipomuuliza Mtume (s.a.w.) akajibu: "Ni Jibril". Khadija akapiga uso wake.
Taz: Tarikhul Yaa'quby J. 2 Uk. 23.
e.  Khadija alipewa kipande cha karatasi na mganga mmoja ili ampe Muhammad (s.a.w.) kama hali hii (iliyomfikia Muhammad) inasababishwa na ugonjwa wa kichaa, basi atapona... Khadija aliporudi kwa mumewe akamkuta anasoma Qur'an, Khadija akamchukua akaenda naye kwa yule mganga, walipofika kwa mganga, akafunua mgongo wa Mtume akaona muhuri wa Utume uko kati ya mabega mawili!!!
Tazama: Tarikhul Khamisi J. 1 Uk. 284, Assiratul Halabiyya J. 1 Uk. 243, Assiratun Nabawiyya J. 1. Uk. 83.
f.    Muhammad (s.a.w.) alipofikiwa na hali hiyo (ya kujiwa na Malaika) alikuwa akipanda katika kilele cha mlima mrefu na akitaka kujitupa chini (ili afe).
Tazama: Almuswannaf J. 5 Uk. 323.
g.  Muhammad (s.a.w.) alirudi kwa mkewe (kutoka katika pango) akiwa nafuraha kubwa akamwambia mkewe: "Nataka kukueleza habari njema, mimi nimeona katika ndoto kuwa Jibril amenijulisha kwamba ametumwa na Mola wangu aje kwangu... Khadija akamwambia: "Furahi, wallahi Mwenyeezi Mungu hatakufanyia lolote ila lililokuwa la kheri... kisha Khadija akaenda kwa mganga wa kinasara, kuuliza uwezekano wa kumuona Jibril. Mganga alishangaa sana kusikia jina la Jibril katika nchi hiyo, kisha akasema kuwa: "Huyo ni Mjumbe wa Mwenyeezi Mungu..."
Taz: Albidayatu Wannihaya J. 3 Uk. 13.

Nadhani umejionea mwenyewe uzushi wa mawahhabi, masalafi na answari sunnah dhidi ya Mtume wetu. Watu waongo na wazushi kama hawa, hawawezi kuaacha waislamu wa kawaida wakiishi kwa amani mustarehe bila kuleta chokochoko.

Lakini sisi waislamu sahihi, yaani Mashia tunaamini kuwa Mtume alikuwa Mtume bado akiwa tumboni mwa mama yake. Hivyo alipozaliwa tu alijulikana kuwa ni Mtume na miujiza mingi ilifanyika katika utoto wake na ujana wake. Kabla ya kufikisha miaka 40 ambapo utume wake ulizinduliwa rasmi na kuanza kazi ya kuueneza Uislamu duniani.

No comments:

Post a Comment