Monday 19 October 2015

WAATHIRIKA WA KARBALA – AWN BIN JAAFAR IBN ABI TALIB (R.A)

WAATHIRIKA WA KARBALA – AWN BIN JAAFAR IBN ABI TALIB (R.A)
Aun ni mtoto wa Jaafar ibn Abi Talib (r.a) na Asma’a bint Amees (r.a)..
Alizaliwa ukimbizini Ethiopia (Uhabeshi) kwani baba yake yaani Jaafar alikuwa kiongozi wa wakimbizi wa kiislamu waliokimbilia Habash kutokana na dhuluma na mauaji waliokuwa akifanyiwa na makafiri wa Makkah wakati wa mwanzo wa Uislamu kutangazwa na Mtume Muhammad (s.a.w.w).
Uislamu ulipota nguvu baba wa Aun yaani Jaafar alirejea uarabuni na kwa kipindi hicho Mtume alikuwa amekwisha hamia Madinah. Miaka michache baadaye Jaafar aliongoza jeshi la waislamu katika mapambano yanayojulikana kama vita vya Mu’tah. Vita hivi vilikuwa vikali sana na waislamu wengi waliuawa ikiwa ni pamoja na kamanda wao, yaani Jaafar bin Abi Talib (r.a). Jaafar aliacha watoto wa kiume watatu yaani Awn, Muhammad na Abdullah.
Vijana hawa walifanana sana na mzee Abu Talib (r.a), hivyo Mtume Muhammad (s.a.w.w) na Imam Ally waliwapenda sana. Baadaye Imam Ally aliwaozesha mabinti wake. Ummu kulthumu aliolewa na Aun na Zainabu aliolewa na Muhammad. Hapa utagundua kuwa wale wanaosema kuwa Imam Ally waliwaozesha mabinti wake kwa Umar bin Khatab ni uongo na propaganda kwa minajiri ya kuwapotosha watu.
Awn aliendelea kuwa Mtiifu kwa Imam Ally kama imam wake wa kwanza, kisha akawa mtiifu kwa Imam Hassan kama imam wake wa pili na hatimaye akawa mtiifu kwa imam Hussein kama imam wake wa tatu. Awn alichinjwa pamoja na Mashia na Ahlulbayt wengine katika eneo la Karbala, Iraq, akipigana vita upande wa Mashia, yaani katika jeshi dogo la imam Hussein (a.s). Innalillahi wainna ilayhi rajiuun.
Source: Ashura Encyclopedia

By Jawad Muhaddithy 

No comments:

Post a Comment