Sunday 6 August 2017

Bi KHADIKA KAMA MALKIA WA MAQRAISHI

Bi KHADIKA KAMA MALKIA WA MAQURAISHI
Assalaam Alaykum.
Khadija alikuwa mtu wa nyumbani, pia ndugu zake na binamu zake hawakupenda kusafiri na misafara. Kwa hiyo, alimuajiri wakala wakati wowote msafara ulipotoka kwenda nje (ya Hijazi), na kumfanya wakala huyo kuwa na madaraka ya kupeleka bidhaa zake kwenye masoko ya nje kuziuza huko. Kwa uwezo mzuri wa kuteua mawakala, na kununua na kuuza wakati na mahali muafaka aliweza kupata faida kubwa sana, na baadaye, akawa mfanyabiashara tajiri sana wa Makka.
Ibn Sa'ad anasema kwenye Tabqaat yake kwamba misafara ya wafanya biashara wa Makka ilipoanza safari, mzigo wa Khadija peke yake ulikuwa sawa na mizigo ya wafanyabishara wengine wote wa Qurayish katika msafara huo. Alikuwa dhahiri kwa kila mtu ni kama msemo "golden touch" ("mguso wa dhahabu") yaani kila atakacho kigusa hata kama ni vumbi litageuka kuwa dhahabu. Watu wa Makka, katika hali hiyo, walimpa jina la Malkia wa Qurayish. Aidha walimwita Malikia wa Makka.

MUBAHALA (MAAPIZANO KATI YA MTUME NA WAKRISTO)

MUBAHALA (MAAPIZANO KATI YA MTUME NA WAKRISTO)
Assalaam Alaykum.
Kabla hatujaingia ndani kuzungumzia suala la Mubahala, kwanza ni vizuri tufahamishe maana ya Mubahala. Muhabala ni: Kuapizana. Ujumbe wa Kikristo kutoka Najran ulifika kwa Mtume kujadili suala la Nabii Isa (a.s.). Mtume aliwajulisha kuwa: Hakika mfano wa Isa mbele ya Mwenyezi Mungu ni kama mfano wa Adam, aliumbwa kwa udongo kisha akamwambia: Kuwa naye akawa. (3:59).
Kwa kuwa Nabii Isa alizaliwa bila baba, Wakristo wamedhani kuwa baba yake ni Mwenyezi Mungu. Aya hii inaondoa dhana hiyo ambayo inapingana na utukufu wa Mwenyezi Mungu, na inawapigia mfano wa ajabu zaidi katika kuumbwa Adam bila ya baba wala mama. Aliumbwa kwa udongo kisha akaambiwa: kuwa naye akawa, na kwa neno hilo hilo Nabii Isa (a.s) ndivyo alivyoumbwa.
Ujumbe huo ulipokuwa haukukubaliana na hoja hii, Mwenyezi Mungu akateremsha Aya:- "Na atakayehojiana nawe (Muhammad) katika hili baada ya ujuzi uliokufikia, waambie: Njooni tuwaite watoto wetu na watoto wenu, na wanawake wetu na wanawake wenu, na nafsi zetu na nafsi zenu, kisha tuombe kwa kunyenyekea tuijaalie laana ya Mwenyezi Mungu iwashukie wenye kusema uongo." (3:61).
Hili lilikuwa tarehe ishirini na nne mfungo tatu mwaka wa kumi. Mtume akawaita ili waanze kuapizana. Wakajibu:- "Ngojea tujadiliane". Walipokwenda faragha, wakamuuliza Askofu Abdul Masih; ana Maoni gani katika suala hili? Akajibu:- Enyi Wakristo: Wallahi nyinyi mnajua kuwa Muhammad ni Nabii aliyeletwa na amekuja na ushahidi ulio wazi juu ya jambo la huyu (Yesu a.s.). Wallahi hakuna watu walioapizana na Nabii wakasalimika, ikiwa mtaapizana naye mtaangamia".
Askofu Peter yeye aliwaambia: "Enyi Wakristo: Mimi naziona nyuso hizi (kundi la Mtume) kama zitamuomba Mwenyezi Mungu auondoe mlima kutoka mahala pake, Wallahi atauondoa. Msiapizane naye mtaangamia, na hatabaki Mkristo ye yote hapa duniani mpaka siku ya Kiama".
Alipoulizwa Ahtam, akawaambia: Niacheni nikamuulize Muhammad, alipomkabili Mtume akamuuliza, "Ewe Abulqasim'! Unatoka na kina nani kwa ajili ya maapizano haya?" Mtume (s.a.w.) akamjibu: "Ninaapizana nanyi nikiwa na watu bora hapa duniani na watukufu mno mbele ya Mwenyezi Mungu, nao ni hawa (akawaonyesha) Ali, Fatima, Hasan na Husein."
Taarifa ya kikosi hicho cha Mtume (s.a.w) ilipowafikia wakaogopa kuapizana na Mtume, na badala yake wakaomba sulhu kwa Mtume (s.a.w.) kwa kutoa dirham arobaini elfu.
TAZAMA: 
Tarikh Ibn Athir J.2 Uk. 200 
Tafsirul Qurtubi J.4 Uk. 104 
Tafsirul Ibn Kathir J.1 Uk. 376-379 
Tafsirul Khazin J.1 Uk. 359-360 
Tafsirul Maragh J.3 Uk. 175 
Tafsirul Kabir J.8 Uk. 81 
Zadul Masir J.1 UK. 399
Katika Ayatul Mubahala, iliposema:- "Tuwaite watoto wetu" Mtume (s.a.w.) alimwita: Hasan na Husein. Iliposema: "Na wanawake wetu" Mtume (s.a.w.) alimwita: "Fatima bint Muhammad". Iliposema: "Na nafsi zetu" mtume akamwita: "Ali". Kwa hivyo Ali bin Abi Talib ni nafsi ya Mtume Muhamad (s.a.w.).
Tukio hili Ia Mubahala tukilitazama kwa upande wa pili, linatukumbusha lile tukio la "KlSAA" Iliposhuka Ayatut Tat'hir:- Hakika Mwenyezi Mungu anataka kukuondoleeni uchafu watu wa nyumba (ya Mtume) na (anataka) kukutakaseni sana sana" (33:33). Iliposhuka Aya hii Mtume alimchukua Ali na Fatima na Hasan na Husein, akawafunika nguo kisha akasema: "Ee Mola! Hawa ni watu wa nyumba yangu, basi waondolee uchafu na uwatakase sana sana." Mama Ummu Salama (mke wa Mtume) alipotaka kuingia humo, Mtume (s.a.w.) akamzuia:
Kama ambavyo kwenye tukio la Mubahala ulipofika wakati wa kuomba maombi maalumu kwa ajili ya maapizano kati yake na Wakristo wa Najran, Mtume alimchukua Ali na Fatima na Hasan na Husein tu. Ingawa wakati huo Mtume (s.a.w.) alikuwa nao wakeze, na Masahaba ambao ni marafiki zake pia, lakini hapa hawakuingia. Wake za Mtume na Masahaba hawakuingia katika "KISAA" na hawakusimama katika uwanja wa Mubahala, kwa sababu Mwenyezi Mungu aliwahusisha darja hii Ahlul Bait tu peke yao.
TAZAMA: 
Tafsirul Khazin J.3 Uk. 259 
Tafsirul Ibn Kathir J.3 Uk. 494 
Tafsirul Qurtubi J.14 Uk. 183 
Zadul Masir J.6 Uk. 381

MNAJIMU

MNAJIMU
Kiongozi wa Waumini, Ali mwana wa Abu Talib (a.s) na jeshi lake juu ya migongo ya farasi walikuwa wakaribia kuelekea Nahrwan.
Ghafla mmoja katika wafuasi wake maarufu alimjia na bwana mwingine akisema: “Ewe kiongozi wa waumini, huyu bwana ni mtabiri na ana jambo la kukueleza.” Mtabiri huyo akasema: “Ewe kiongozi wa waumini, si vizuri nyinyi kusafiri wakati huu, tafadhali subirini masaa mawili au matatu ya siku yapite kisha muendelee na safari yenu”.
“Kwa nini?”
“Kwa sababu nyota zinatuambia kuwa mtu yeyote ambaye atasafiri nyakati hizi atashindwa na adui yake. Yeye na wafuasi wake watapata shida kubwa. Lakini mkisafiri wakati ambao nimependekeza mtashinda na mtafaulu katika kufikia lengo lenu.”
Imam akasema, “Farasi wangu anatarajiwa kupata mtoto unaweza kuniambia atakayezaliwa atakuwa farasi wa kiume au wa kike?”
“Nikifanya hesabu naweza kueleza”
“Unasema uwongo, kwa wewe haiwezekani, kwa sababu imeandikwa katika Qur’an, ‘Hakuna yeyote isipokuwa Allah anayejua kuhusu mambo yaliyofichikana, na pia ni Mwenyezi Mungu peke Yake ambaye anaejua ni nini kilichobebwa (kiume ama kike) katika tumbo la mama.’ Hata Mtume wa Mungu (Muhammad (s.a.w.w) hakuwahi kudai jambo kama hili unalodai. Unadai kuwa una elimu yote kuhusu dunia hii? Na je, unajua wakati mtu ana bahati nzuri ama mbaya katika majaaliwa yake? Kama mtu yeyote anakuamini na kuamini mambo yako, basi hamhitajii Mwenyezi Mungu kabisa.”
Baada ya hayo yote imam Ali (a.s) aliwaambia wale watu wengine waliobaki: “Tambueni! Msifuate mambo kama haya, yanamfanya mtu kuamini yasiyoonekana na ni kama mtabiri ama mchawi. Na mchawi ni kafiri na kafiri ni wa motoni.”
Baada ya hayo aliziangalia mbingu na akasema maneno machache ambayo yalikuwa yanahusu imani yake kwa Allah (s.w.t).
Kisha alimwangalia yule mtabiri na akasema “Kwa makusudi nitakwenda kinyume na ushauri wako na tutaondoka sasa hivi bila kuchelewa.” Mara baada ya maneno hayo aliwaamuru wafuasi wake waanze safari.
Waliondoka kuelekea kwa maadui. Kama ilivyolinganishwa na vita vya jihad vingine, katika Jihad hii, Imam (a.s) alifaulu ajabu na kupata ushindi mkubwa.

Friday 14 July 2017

FIKRA YA KISUNNI: KHALIFA ACHAGULIWA NA WAISLAM. HIYO NDIO NJIA YA KUMPATA KHALIFA

FIKRA YA KISUNNI: KHALIFA ACHAGULIWA NA WAISLAM. HIYO NDIO NJIA YA KUMPATA KHALIFA:
SWALI KWAO:
IKIWA KHALIFA ANAPATIKANA KWA KUCHAGULIWA NA WAISLAM NA KWAMBA MTUME (S.A.W.W) AMEWAACHIA WAISLAM WACHAGUE WENYEWE WAMTAKAYE. BASI TUNAOMBA MTWAMBIE KHALIFA WENU WA PILI NI NANI ALIMCHAGUA NA KWA KIBALI GANI AU NI WAISLAM WEPI WALIOMCHAGUA. TUPENI HISTORIA YENU KUHUSU HILO?!
NDIO; TUNAKUBALI KHALIFA WENU WA KWANZA WAISLAM WALIMCHAGUA KATIKA UKUMBI WA SAQIFA KUPITIA MSHIKE MSHIKE KANGA KUCHANIKA NA KAMA MSEMAVYO KUWA HIYO NDIO NJIA SAHIHI KWENU NYINYI MNAVYOONA YA KUPATIKANA KWA KHALIFA WENU BAADA YA MTUME (S.A.W.W)!!!!. LAKINI HATUKUBALI HIVI HIVI BALI TUNAKUBALI ILI TUKUULIZENI SWALI LA KIMANTIKI: JE, HUYO KHALIFA WENU WA PILI NA WA TATU HIZO NJIA ZILIZOTUMIKA KUWATEUA KAMA MAKHALIFA ZIMEELEZWA WAPI KATIKA HISTORIA YA MAISHA YA MTUME S.A.W.W?!.
MNATIA HURUMA NDUGU ZETU, YAANI MAMBO YAPO WAZI TU LAKINI HAKUNA WA KUJIULIZA NA HAMTAKI KUJIULIZA MASWALI YA KUDADISI WALA KUJENGA FIKRA ZA KIAKILI MNAPANDIKIZWA ELIMU FEKI BILA KUJITAMBUA KUHUSIANA NA MATUKIO YA KIHISTORIA.
HEBU JIULIZENI: NI UISLAM GANI HUO AMBAO HAUNA MFUMO MMOJA WA KUPATIKA KHALIFA (YAANI YAANI KIONGOZI) WA KUWAONGOZA WAISLAM?!. MARA MNASEMA KHALIFA ANACHAGULIWA NA WAISLAM. ILI MRADI TU MTETEE UKHALIFA WA KHALIFA WENU WA KWANZA.
LAKINI KHALIFA WA PILI HAJACHAGULIWA NA WAISLAM NA MKIULIZWA NANI ALISEMA ABUBAKAR AMTEUE OMARI NDIO JAMBO ZURI KUMPATA KHALIFA. KISWAHILI KINAINGIA MFUKONI !!! MAANA TUNAWAULIZA ABUBAKAR ALIYEMTEUA SWAHIBA WAKE OMAR AWE KHALIFA (BAADA YA KUJIONA YEYE ABUBAKAR AKARIBIA KUANGAMIA) HILO LINAMFANYA AWE BORA KULIKO MTUME (S.A.W.W), MAANA YEYE KWA MTAZAMO WENU ALIUACHA UMMA HUU BILA KUUTANGAZIA NANI KHALIFA NA WASII WAKE BAADA YAKE...!!
HIVYO MNATOA MESEJI KWA KUJUA AU KWA KUTOJUA KUWA ABUBAKAR, KHALIFA WENU WA KWANZA KWA HESABU YENU NYINYI NI BORA ZAIDI YA MTUME WETU MUHAMMAD (S.A.W.W) ?! KWA KUWA KAFANYA JAMBO BORA ZAIDI, LA KUMTEUA SWAHIBA WAKE OMAR BIN KHATTABI KAMA MTU ATAKAYETAZAMA NA KUONGOZA UMMA HUU WA KIISLAM BAADA YAKE NA HILO MTUME (S.A.W.W) HAKULIONA?!!!
SUBHANNALLAH MNAMDHALILISHA MTUME WETU (S.A.W.W) NAKUMPA SIFA YA KUTOJALI WALA KUWA NA MAPENZI NA UMMA HUU NA HII IKIWA NI MATOKEO YA UJUHA WENU NA KUENDEKEZA TAASUBI ZENU MPAKA MMEKUWA VIPOFU MNAMUONA ABUBAKAR BORA KULIKO MTUME WA UISLAM (S.A.W.W)!!.
TUKIMCHUNGUZA KHALIFA WA TATU, TUNAKUTA ALIPATIKANA KWA KUTEULIWA NA WATU SITA KWA NIABA YA UMMA WA KIISLAMU. HIVI KWELI KILA KIONGOZI ANA UTARATIBU WAKE WA KUPATIKANA? JE UISLAMU HAUNA UTARATIBU WA KUPATIKANA VIONGOZI.
SISI MASHIA TUNASEMA FIKRA YENU NI POTOFU KWANI MTUME ALIACHA AMEWAPANGA SAFI NZIMA YA MAKHALIFA AMBAO NI KUMI NA MBILI, WA KWANZA WAO AKIWA NI IMAM ALLY (A.S)

USHIRIKINA NA AINA ZAKE:

USHIRIKINA NA AINA ZAKE:
Assalaam Alaykum.
Ushirikina ni wa aina mbili: Ushirikina wa wazi na ushirikina uliofichika. Ushirikina wa wazi una maana ya kumshirikisha mtu au kitu na Nafsi Kamili ya Allah au kumshirikisha na sifa Zake. Kumfanyia Allah washirika maana yake kushirikisha kitu na Upweke Wake na kuukiri ushirikishaji huu kwa ulimi, kama Sanamiyya (waabudu sanamu) au Mazorostania, ambao wanaamini katika kanuni mbili:
Nuru na giza. Wakristo pia wanafanya hivyo. Wanaamini katika utatu na kuugawanya uungu katika sehemu tatu - Baba, Mwana, na Roho Mtakatifu. Wanaamini katika tabia tofauti za kila mmoja, na mpaka watatu hawa waungane, bila hivyo uungu wenyewe hautakuwa kamili.
Qur’ani Tukufu inakataa imani hii, na Allah (s.w.t.) anaelezea upweke wake katika maneno haya:
“Kwa hakika wamekufuru wale waliosema: Hakika Allah ni Mmoja katika watatu; hali hakuna mungu ila Allah Mmoja….” (5:73).
Kushirikisha vitu na sifa za Uungu, maana yake ni kuamini kwamba sifa Zake, kama elimu Yake au nguvu ziko tofauti na, au ni nyongeza katika Nafsi Yake Kamilifu.
Ashariyya wa Abu’l-Hasani Ali bin Ismail Ashari Basari, wanaelezewa na Maulamaa wenu wakubwa, kama Ali bin Ahmad katika kitabu chake Al-Kashf na Minhaju’l-Adilla fi Aqa’idi’l-Mila, Uk. 57 kuwa wanaamini kwamba Sifa za Allah ni nyongeza katika Nafsi Yake kamilifu, na kwamba ni za milele. Hivyo yeyote mwenye kuamini kwa njia yeyote ile kwamba tabia au sifa yeyote ya Allah ni nyongeza katika Nafsi yake kamilifu, huyo ni mshirikina.
Kila sifa Yake ni yenye asili kwake.
Ushirikina katika matendo ya mtu, ina maana kumshirikisha mtu mwingine katika Dhati Yake Yenye kujitosheleza Daima dumu.
Mayahudi wanaamini kwamba Allah aliumba viumbe na kisha akajiweka mbali na viumbe Wake. Katika kuwalaumu watu hawa, aya ifuatayuo iliteremshwa:
“Na Mayahudi wanasema: Mkono wa Allah umefungwa! Mikono yao itafungwa (kwa pingu) na watalaaniwa kwa yale wanayoyasema. Bali, mikono yake yote iwazi; Hutoa apendavyo…” (5:64).
Ghullat wanaunda kundi lingine la washirikina. Pia wao wanaitwa Mufawwiza. Wanaamini kwamba, Allah ameweka au kuaminisha Mamlaka ya mambo yote kwa Maimam watukufu. Kwa mujibu wao, Maimam ni waumbaji na pia hutupatia sisi riziki. Kwa uwazi, wale wanaomuona mtu kuwa mshirika katika Mamlaka ya Uungu ni mshirikina.
Ushirikina Katika Swala:
Ushirikina katika Sala, ina maana ya mtu kugeuza mazingatio yake wakati wa swala kwa makusudi kuelekea kwa kiumbe aliyeumbwa badala ya kuelekea kwa Allah. Kama mtu akikusudia kuomba kwa kiumbe aliyeumbwa, huyo ni mshirikina. Qur’ani Tukufu inakataza haya katika maneno haya.
“…Anayetarajia kukutana na Mola Wake, naafanye vitendo vizuri, na asimshirikishe yeyote katika ibada ya Mola wake.” (18:110).
Aya hii inaonyesha kwamba sharti la msingi wa imani ni kwamba mtu lazima afanye lolote lile ambalo ni zuri na asije kumshirikisha yeyote pamoja na Allah katika kutoa utii na ibada Kwake. Kwa maneno mengine, yule ambaye anasali au kutekeleza Hija, au kufanya kitendo chochote kizuri kwa ajili tu ya kujionyesha kwa watu uzuri wake, ni mshirikina.
Amewashirikisha wengine pamoja na Allah katika jambo la kutekeleza vitendo vyake. Kuonyesha kujikinai kwa matendo mazuri ni ushirikina mdogo, ambao hutangua vitendo vyetu vizuri.
Imepata kuelezwa kwamba Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alisema: “Jiepusheni na ushirikina mdogo.” Watu wakamuuliza, “Ewe, Mtume wa Allah, ni nini ushirikina mdogo? Akajibu: “Al- riya wa’s-sama” (yaani, kuonyesha watu au kuwafanya wasikie juu ya ibada yako kwa Allah).
Vile vile Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alisema: “Kitu kibaya mno ninachokuhofieni kwenu ni ushirikina uliofichika; hivyo kuweni na hadhi ya juu yake kwa kuwa miongoni mwa wafuasi wangu ushirikina ni wa siri mno kuliko kutambaa kwa mdudu chungu juu ya jiwe gumu katika usiku wa giza.”
Tena alisema: “Mtu ambaye anatekeleza ibada ya Sala kwa njia ya majivuno, ni mshirikina. Mtu ambaye anafunga au kutoa sadaka au kutekeleza Hija au kumuachia mtumwa huru ili kuonyesha kwa watu uadilifu wake au kujipatia jina zuri, ni mshirikina.”
MAWAHHABI NA MASALAFI NI WASHIRIKINA KWA SABABU
1. Saudi Arabia, Israel na Marekani ni wafadhili wakubwa wa Mawahhabi na masalafi
2. Wanategemea misaada ya katika juhudi zao za kuwafitinisha waislamu, hivyo humwomba asiye kuwa Mwenyezi Mungu.
3. Katika ibada zao hufikilia namna ya kuwadhuru wanadamu badala ya kumwelekea Muumba

UBORA WA MTU MBELE YA ALLAH (S.W) UNATEGEMEA UCHAMUNGU NA SIO UKARIBU WA MTU KWA MTUME (S.A.W.W)

UBORA WA MTU MBELE YA ALLAH (S.W) UNATEGEMEA UCHAMUNGU NA SIO UKARIBU WA MTU KWA MTUME (S.A.W.W)
Kuna watu wanasema kuwa masahaba wote wa Mtume (s.a.w.w) walikuwa ni wachamungu. Sielewi labda ni kutokujua Historia yao au kutokufahamu maana ya sahaba.
Sahaba ni Mtu yeyote aliyezaliwa au kusilimu wakati Mtume (s.a.w.w) akiwa hai awe alimuona kwa macho au hakumuona kwa sababu ya upofu au umbali wa kutoka eneo analoishi huyo na eneo alilokuwa akiishi Mtume (s.a.w.w) na hivyo kusababisha wasionane kwa macho, lakini bado ni sahaba. Hii itakuwa na maana kuwa malaki ya watu waliokuwa wakiishi Uarabuni kipindi hicho walikuwa Masahaba. Wale waliozaliwa au kusilimu baada ya Mtume kufariki wanaitwa Tabiin, na kizazi kilichopatikana baada ya tabiin huitwa tabitabiin. Sasa hakuna uwezekano wa kuwasema wote kuwa wachamungu bila kuwatofautisha kulingana na matendo yao.
Jee wake wa Mtume Muhammad (s.a.w.w); hawakuwa Waislamu? Hawakuwa ma mama wa waumini? Mbona Mwenyezi Mungu amewawekea sharti ya ucha-Mungu (Sura 33:32) ndipo wapate daraja yao, kwa kuwaambia: 'Enyi wake wa Mtume! Nyinyi si kama yeyote kati ya wanawake, kama mtamcha Mwenyezi Mungu...' Hili ni kutuonyesha kwamba kama hawatakuwa na mwendo mwema (hawatamcha Mola wao), basi ile kuwa ni wake wa Mtume tu hakutawafaa kitu. Bali ikizidi, kama watafanya machafu yoyote, inatakikana adhabu yao iwe maradafu kama inavyoelezwa kwenye Sura 33:30. Na hivyo ndivyo inavyotakikana tuwe kwa masahaba.
Ili tupate mafunzo toka kwa Masahaba tunatakiwa tuchunguze mienendo yao, tutakao ona kuwa wana mienendo mizuri tuwafuate na tutakao ona kuwa wana mienendo mibaya tuambizani kukwepa kuwafuata.
Maana kama wao-waliokaa na Bwana Mtume (s.a.w.w.) na kupokea kwake maadili yote hawatatuwekea ruwaza njema, nani mwingine atatufanyia hilo? Na jee, kama hatutawatuhumu kwa yale maovu waliyoyatenda, watu wengine si watayachukulia kuwa ni mema kwa sababu tu yamefanywa na sahaba wa Mtume (s.a.w.w.), hasa kwa hivi ambavyo, Kisunni, mwendo wa baadhi ya sahaba [1] wa Bwana Mtume (s.a.w.w.) huhesabiwa kuwa ni sunna?!
Kutokana na aya mbili tatu tulizozitaja hapo juu, nataraji nimeweza kuthibitisha kwamba ule mtazamo wa kuwa sahaba wote ni waadilifu, baada ya kuambiwa kwamba sahaba ni yule aliyemwona Mtume (s.a.w.w) japo kwa mbali-na akafa ni Mwislamu, ni mtazamo unaopingana na Qur'ani Tukufu na mafunzo ya Bwana Mtume (s.a.w.w.).
Nitaendelea kutoa mada hii kuonesha kuwa imani ya kuwa Masahaba hawakosei na kwamba wote ni wachamungu unavyopingana na ukweli wa maisha yao wenyewe Masahaba. Kwa mfano masahaba walipingana vita na kuuana, hivi ni kweli kwamba aliyeua na aliyeuawa wote walikuwa wachamungu? Haitoshi baadhi ya ndugu wa Mtume ndio waliokuwa makafiri wakubwa na wakimpiga vita Mtume (s.a.ww.).
Marejeo:
[1] - Taz. uk. 74 wa Juzuu ya Nne ya al-Muwafaqat ya Shatibi.

MGOMO WA MWALIMU

MGOMO WA MWALIMU
Sayyid Jawad Amuli, alikuwa Aalimu (Faqih) mashuhuri sana, ambaye ndiye aliandika kitabu Miftahul Karamah (Kitabu maarufu sana).
Siku moja alikuwa akishughulika na kula chakula wakati aliposikia mlango ukibishwa. Mara alipojua kuwa alikuwa mfanyakazi wa mwalimu wake - Sayyid Mahdi Bahrul Uluum - haraka alifungua mlango. Mfanyakazi alimwambia, “Bwana, Mwalimu anakuita upesi. Chakula tayari kimeandaliwa mbele yake lakini hawezi kukigusa hadi ufike huko.”
Hakukuwa na muda wa kupoteza; hata kabla ya kumaliza chakula chake, Sayyid Jawad aliharakisha kwenda nyumbani kwa Sayyid Baharul-Uluum.
Punde tu mwalimu alipomwona Sayyid Jawad kwa hasira na huzuni kubwa alimwambia: “Ewe Sayyid Jawad! Wewe humwogopi Allah? Na huoni haya mbele ya Allah?”
Sayyid Jawad alipatwa na mshangao mkubwa. Alifikiria hata hivyo, ni nini kimetokea na ni tukio gani limejitokeza? Hadi kufikia wakati huu jambo kama hilo halijawahi kutokea kwamba mwalimu wake angemkaripia kiasi hicho. Alishughulisha akili yake kuweza kugundua sababu yake. Bila msaada wowote aliuliza: “Bwana wangu, kama inawezekana tafadhali nijulishe makosa yangu.”
Alijibiwa, Jirani yako fulani hakuweza kupata mchele na ngano kwa siku saba zilizopita na katika hizi siku amekuwa akila tende za kukopa kutoka kwa muuza duka ambaye yuko mwisho wa njia. Leo alipokwenda kuchukua mkopo, kabla hajauliza chochote, muuza duka alimhuzunisha kwa kumwambia: “Sasa hivi una deni kubwa sana.”
“Kwa kusikia hayo aliona haya na bila kunyanyua kichwa aliondoka na kurudi nyumbani bila ya kitu. Leo yeye na familia yake wana njaa.”
Sayyid Jawad Amuli akasema: “Wallahi naapa kuwa sikujua kuhusu jambo hili. Kama ningejua hivyo mimi bila shaka ningewasaidia.”
Mwalimu alisema: “Huzuni na hasira yangu vyote ni kwa sababu ya kutojua kwako. Zaidi ya hayo kwa nini hujui hali ya jirani yako? Na ni kwa nini wamemaliza siku saba usiku na mchana katika hali hiyo bila ya wewe kujua jambo hilo. Na kama ulijua jambo hili na ukawa hukuchukua hatua yoyote, haungechukuliwa kama Mwislamu, bali kama Myahudi.”
Sayyid Jawad akasema, “ Nieleze nifanye nini?”
Mwalimu akamjibu: “Mfanyakazi wangu atabeba sinia iliyojaa chakula. Wewe nenda naye kwenye nyumba ya yule bwana. Mfanyakazi atarudi afikapo mlangoni. Baada ya hapo utabisha mlango na uwaombe ule pamoja nao chakula chao cha usiku. Chukua hizi pesa na uziweke chini ya zulia au mkeka. Na umuombe akusamehe kwamba kwa kuwa jirani yao, hukuweza kuwajali. Iwache hii sinia hapo hapo na urudi hapa. Naketi hapa na siwezi kula chakula hiki hadi urudi na unieleze kuhusu huyo bwana mcha Mungu. “
Mfanyakazi akachukua hiyo sinia iliyojaa chakula kizuri na kufatana na Sayyid Jawad.
Walipofika karibu na mlango, mfanyakazi alirudi.
Baada ya kubisha hodi, aliingia ndani. Mwenye nyumba akamsikiza Sayyid Jawad akiomba msamaha na kwa maombi yake alikichukua chakula kutoka mikononi mwake.
Baada ya tonge la kwanza tu, aligundua kuwa hakikuwa chakula cha nyumba ya Sayyid Jawad. Mara moja aliacha kula na kusema: “Hiki chakula hakitengenezwi na mwarabu yeyote. Hivyo basi hakijatoka kwenye nyumba yako. Hadi wakati ambapo utanieleza chakula hiki kimetoka wapi ndio tutakila.
“Makisio ya yule bwana yalikuwa sawa. Chakula hicho kilikuwa kimetengenezwa nyumbani kwa Bahrul Uluum na alikuwa Muirani kutoka Burujard.
Sayyid Jawad alisisitiza kwa kusema, “Kwanini unajisumbua kutaka kujua kilipotayarishwa chakula hiki, wewe endelea chukua kula. “Lakini Bwana huyo hakukubaliana naye na akasema: “Mimi sitagusa chakula hiki hadi uniambie ukweli.”
Sayyid Jawad aliona hakuna kitakachowezekana hadi aseme ukweli. Hivyo basi akaeleza hadithi yote kutoka mwanzo hadi mwisho. Baada ya kumsikiliza Sayyid Jawad, bwana huyo alikila hicho chakula lakini alishangaa. Akasema: “Sisi hatukumueleza mtu yeyote siri hii. Bali hata hatukukubali jirani yetu wa karibu ajue kuhusu jambo hili, sijui ni vipi Sayyid alivyokuja kulijua hili.”

SABABU ZA MTUME MUHAMMAD (S.A.W.W) KUMLEA IMAM ALLY (A.S)

SABABU ZA MTUME MUHAMMAD (S.A.W.W) KUMLEA IMAM ALLY (A.S)
Mtume Muhammad (a.s) na mama yetu bibi Khadija (a.s) walimchukua Imam Ali (a.s) baada ya kufa kwa watoto wao wenyewe wa kiume. Kwa hiyo imam Ali aliziba uwazi katika maisha yao na kuwa kama mtoto wao wa kumzaa hasa.

Sababu nyingine ya kumchukua imam Ali na kumlea ni kumuelimisha na kumuandaa kwa ajili ya takdir kubwa iliyokuwa ikimngojea katika nyakati zijazo. Hapa ninakusudia kumwandaa kuwa kiongozi wa baadaye wa Uislam.

Kiongozi wa Uislamu ni lazima aandaliwe kiislamu, katika mazingira ya Uislamu hasa. Ni tofauti na kukurupuka na kumpa uongozi mtu asiyeandaliwa vyema. Kumpa mtu uongozi wa jambo asilolijua vyema ni kulidumaza jambo lenyewe.

Dr. Taha Hussein wa Mirsi anasema kwamba Mtume wa Allah (s.w.t.) mwenyewe alikuwa kiongozi wa Ali, mwalimu na mwelekezaji, na hii ni sifa moja nyingine zaidi ambayo anayo Ali, na ambayo hakuna mwingine yeyote anayeshirikiana naye kwayo.

 “Uislamu unaweka tamasha la maendeleo ya dini ya ulimwengu katika mwanga wa historia.” (Uislamu, 1969)
Kadhalika, inaweza kusemwa kwamba kati ya marafiki na Masahaba wote wa Muhammad, Mtume wa Uislamu, Ali ndiye pekee aliyekua katika mwanga kamili wa historia.

Hakuna sehemu ya maisha yake, ama katika uchanga wake, utoto wake, uvulana wake ujana wake, uanaume wake au kupevuka, ambayo imefichikana kutoka kwenye mwangaza wa historia. Alikuwa ndio kivutio kikuu cha macho yote tangu kuzaliwa kwake mpaka kufa kwake. Kwa upande mwingine maswahaba waliobakia wa Mtume (s.a.w.) wanakuja kwenye mvuto wa nadhari ya mwanafunzi wa historia baada tu walivyokubali Uislamu, na kidogo, kama kipo, kinajulikana mpaka kufikia hapo.

Imam Ali alijaaliwa kuwa mkono wa kuume wa Uislamu, na ngao na kingio la Muhammad, Mtume wa Allah (s.w.t.) Takdira au maajaliwa yake yalikuwa kiungo kisichotenganishwa na takdira ya Uislamu, na maisha ya Mtume wake. Alikuwepo katika kila hali ya mambo katika historia ya harakati hii mpya, na alishika nafasi ya kuwa nyota ndani yake. Ilikuwa, kwa dharura, ni nafasi ambayo yeye pekee ndiye angeweza kuishika.
Aliakisi “taswira” ya mtume Muhammad (s.a.w.w). Kitabu cha Allah (s.w.t.) chenyewe kimemuita “nafsi” au mwandani (nafsi ya pili) ya Mtume Muhammad katika Aya ya 61 ya Sura ya tatu, na alionyesha jina lake maarufu toka upande mmoja hadi mwengine, wa historia.


Muundo wa ufanyaji kazi pamoja wa mtume Muhammad na imam Ali - amir na mfuasi – ulikuja kuweka “Ufalme wa Mbinguni” katika ramani ya dunia.