Friday 14 July 2017

SABABU ZA MTUME MUHAMMAD (S.A.W.W) KUMLEA IMAM ALLY (A.S)

SABABU ZA MTUME MUHAMMAD (S.A.W.W) KUMLEA IMAM ALLY (A.S)
Mtume Muhammad (a.s) na mama yetu bibi Khadija (a.s) walimchukua Imam Ali (a.s) baada ya kufa kwa watoto wao wenyewe wa kiume. Kwa hiyo imam Ali aliziba uwazi katika maisha yao na kuwa kama mtoto wao wa kumzaa hasa.

Sababu nyingine ya kumchukua imam Ali na kumlea ni kumuelimisha na kumuandaa kwa ajili ya takdir kubwa iliyokuwa ikimngojea katika nyakati zijazo. Hapa ninakusudia kumwandaa kuwa kiongozi wa baadaye wa Uislam.

Kiongozi wa Uislamu ni lazima aandaliwe kiislamu, katika mazingira ya Uislamu hasa. Ni tofauti na kukurupuka na kumpa uongozi mtu asiyeandaliwa vyema. Kumpa mtu uongozi wa jambo asilolijua vyema ni kulidumaza jambo lenyewe.

Dr. Taha Hussein wa Mirsi anasema kwamba Mtume wa Allah (s.w.t.) mwenyewe alikuwa kiongozi wa Ali, mwalimu na mwelekezaji, na hii ni sifa moja nyingine zaidi ambayo anayo Ali, na ambayo hakuna mwingine yeyote anayeshirikiana naye kwayo.

 “Uislamu unaweka tamasha la maendeleo ya dini ya ulimwengu katika mwanga wa historia.” (Uislamu, 1969)
Kadhalika, inaweza kusemwa kwamba kati ya marafiki na Masahaba wote wa Muhammad, Mtume wa Uislamu, Ali ndiye pekee aliyekua katika mwanga kamili wa historia.

Hakuna sehemu ya maisha yake, ama katika uchanga wake, utoto wake, uvulana wake ujana wake, uanaume wake au kupevuka, ambayo imefichikana kutoka kwenye mwangaza wa historia. Alikuwa ndio kivutio kikuu cha macho yote tangu kuzaliwa kwake mpaka kufa kwake. Kwa upande mwingine maswahaba waliobakia wa Mtume (s.a.w.) wanakuja kwenye mvuto wa nadhari ya mwanafunzi wa historia baada tu walivyokubali Uislamu, na kidogo, kama kipo, kinajulikana mpaka kufikia hapo.

Imam Ali alijaaliwa kuwa mkono wa kuume wa Uislamu, na ngao na kingio la Muhammad, Mtume wa Allah (s.w.t.) Takdira au maajaliwa yake yalikuwa kiungo kisichotenganishwa na takdira ya Uislamu, na maisha ya Mtume wake. Alikuwepo katika kila hali ya mambo katika historia ya harakati hii mpya, na alishika nafasi ya kuwa nyota ndani yake. Ilikuwa, kwa dharura, ni nafasi ambayo yeye pekee ndiye angeweza kuishika.
Aliakisi “taswira” ya mtume Muhammad (s.a.w.w). Kitabu cha Allah (s.w.t.) chenyewe kimemuita “nafsi” au mwandani (nafsi ya pili) ya Mtume Muhammad katika Aya ya 61 ya Sura ya tatu, na alionyesha jina lake maarufu toka upande mmoja hadi mwengine, wa historia.


Muundo wa ufanyaji kazi pamoja wa mtume Muhammad na imam Ali - amir na mfuasi – ulikuja kuweka “Ufalme wa Mbinguni” katika ramani ya dunia.

No comments:

Post a Comment