Friday 20 September 2013

HADITH YA MTUME INAYOWALAUMU MASAHABA KWA KUWAFUATA WAYAHUDI NA WAKRISTO



Amesema Mtume Mohammad (S.A.W) kuwaambia Masahaba wake, “Bila shaka Mtafuata nyendo za waliokutangulieni shubiri kwa shubiri na dhiraa kwa dhiraa (Hatua kwa hatua au kidogo kidogo) hata kama wataingia katika shimo la kenge, mtawafuata”. Masahaba wakauliza, “Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, ni wayahudi na wakristo?” Mtume akajibu, “Ni nani basi (kama sio hao)?”
Rejea:
1.     Sahihi bukhari juzuu 4 ukurasa wa 187
2.     Sahihi Muslim juzuu ya 8 ukurasa wa 57
3.     Musnad Ahmad bin Hambal juzuu ya 3 ukurasa wa 84 na 94

Ndani ya Qur’an na katika Historia sahihi inaeleweka wazi kuwa Wayahudi walimuasi Mtume wao Nabii Mussa (a.s), wakaiasi amri yake, wakamuudhi na wakaiabudia ndama alipokuwa hayupo, kisha walifanya njama dhidi ya Hurun nduguye Mussa (a.s) na walikaribia kumuua. Kwa ajili hiyo walipewa adhabu ya unyonge na umaskini na wakastahiki adhabu ya Mwenyezi Mungu, yakiwa ni malipo yao kwa matendo waliyokuwa wakiyafanya. Walirtadi baada ya kuamini kwao na wakafanya njama dhidi ya Mitume ya Mwenyezi Mungu na kumpinga Mtume kila alipowaambia jambo wasiololitaka.
Ebu tulinganishe maelezo haya ya Mayahudi na hali halisi katika Uislamu.
1.     Nabii Mussa (a.s) alimuomba Allah ajalie nduguye Haruna awe Msaidizi wake na Allah alikubali, Harun naye akawa Mtume kama alivyokuwa Mussa (a.s). Mtume Mohammad (S.A.W) naye alimuomba Allah amfanye nduguye Imam Ally (a.s) kuwa khalifah baada yake na ikawa hivyo, hata kama Baadhi ya Masahaba walimzuia Imam Ally (a.s) kuongoza dola ya kiislamu lakini bado Mashia wanafuata mungozo wa Imam Ally mpaka leo hii kama imam na khalifah wa kwanza wa Mtume.
2.     Mtume alimteua Imam Ally (a.s) kuwa khalifah baada yake lakini baadhi ya Masahaba walifanya njama na kumzuia kuwaongoza waislamu
3.     Omar bin Khatab (R.A) alikuwa akimpinga Mtume Mohammad (S.A.W) katika kila tukio aliloona halipendi yeye Omar na wafuasi wake wanamsifu kwa hilo hadi leo hii. Kwa mfano Omar alimpinga Mtume katika sulhu ya Hudaibiyya, Msiba wa Alhamis, na pia aligoma kujiunga na jeshi la Usama bin Zaid.

No comments:

Post a Comment