Saturday 31 August 2013

UPOTOFU WA MAWAHHABI



Mawahhabi wanadai kuwa Muhammad ibn 'Abd al-Wahhab alikuwa akihubiri mawazo yake kwa ajili ya kujipatia utukufu katika imani yake katika upweke wa Allah swt na kuwakomboa Waislamu wasitumbukie katika Shirk.  Wao wanadai kuwa Waislamu wamekuwa wakitenda dhambi ya Shirk kwa karne sita mfululizo na hivyo yeye alikuja kuirejesha upya dini ya Uislamu. Yeye anazitoa Ayah za Qur’an Tukufu nambari 5 ya Surah al-Ahqaf, Ayah 106 surah  Yunus, Ayah 14 sura al-Ra’d ili kwamba Waislamu wote wakubaliane na mawazo yake. Hata hivyo, zipo Ayah nyingi kama hizo, na Maulamaa wanasema kuwa hizo Ayah zimekuwa zikiwazungumzia makafiri waliokuwa wakiabudu miungu na masanamu au waliokuwa washirikina.

Kwa mujibu wa Muhammad ibn 'Abd al-Wahhab, Mwislamu anakuwa Mushrik pale anapoomba kwa Mtume Muhammad s.a.w.w, au kwa Mtume a.s. mwingine, au walii au mcha Mungu karibu na kaburi au mbali kutoka hapo, yaani, iwapo anapomwomba msaada wa kutokana na shida aliyonayo, au anapoomba kutetewa mbele ya Allah swt kwa kutaja jina  lake au anapotaka kuzuru kaburi lake.  Allah swt anatuambia  kuhusu makafiri wanaoabudu miungu na masanamu katika Ayah ya tatu ya surah al-Zumar, lakini Mawahhabi wanaonyesha Ayah hii kama ndio waraka wa kuhalalisha utumiaji wao wa neno la Mushrik kwa ajili ya Waislamu waombao kwa kuwaweka Mitume a.s. au Mawalii kama ndio watu walio baina yao na Allah swt.  Wao wanasema kuwa hata Mushrik waliokuwa wakiabudu miungu pia walikuwa wakijua kuwa vyote vilikuwa vimeumbwa na Allah swt. Wao wanasema kuwa Allah swt amebainisha:  Na kama ukiwauliza, Ni nani aliyeumba mbingu na ardhi na akalitiisha jua na mwezi?” Bila shaka watasema, Allah (Surah Ankabut, ayah ya 61 na Sura Zukhruf, Aya ya 87). Wao wanadai kuwa hao Mushrik walikuwa hivyo makafiri Mushrik si kwa sababu walikuwa wakiamini hivyo bali wao walizungumza kama ilivyosemwa katika Ayah ya 3 ya Surah az-Zumar: Wale wanaofanya wengine kuwa marafiki badala ya Allah, wanasema, “Wao wanatusaidia kutufikisha karibu (ya Allah swt) kwa kututetea mbele Allah” Wao wanadai kuwa Waislamu wanaoomba katika makaburi ya Mitume, ma-Awliya’ kwa utetezi na misaada basi wanakuwa Mushrik kwa kusema hivyo.

Ni jambo la kipumbavu kabisa kwa Muhammad ibn 'Abd al-Wahhab kuwasema Waislamu wanakuwa makafiri na Mushrik kwa Ayah hiyo. Kwa sababu, makafiri wanawaambudu masanamu ili kwamba ni masanamu hayo tu ndiyo yatakayowasaidia kuwatetea wao; wao wanamwacha Allah swt  na badala yake wanakuwa na imani moja tu ya kuwaomba miungu na masanamu hayo kuwa watetezi wao.  Lakini ni uhakika uliyo bayana kuwa Waislamu kamwe hawawabudu Mitume a.s. au Ma-Awliya’ lakini wanayo imani kuwa kila kitu kinatoka kwa Allah swt. Sisi tunapenda kuwa hao ma-Awliya’ wawe ni Wasila wetu.  Makafiri wanaamini kuwa miungu na masanamu yao inawaombea chochote kile wakitakacho na kumfanya Allah swt kuwatimizia chochote kile wakitakacho.

 Wakati ambapo, Waislamu wanaomba msaada  wa Awliya’ ambao wanawajua kuwa hao ndio watumwa wapenzi  wa Allah swt, kwa sababu Allah swt ameahidi katika Qur’an tukufu kuwa Yeye atawaruhusu waja wake wapenzi kuwatetea na atakubali utetezi wao na Sala na kwa sababu Waislamu wanaamini ubashiri mzuri katika Qur’an. Kamwe huwezi kulinganisha baina ya kafiri anayeabudu miungu na masanamu na Waislamu wakiomba msaada wa Awliya’.  Waislamu na Makafiri wote ni binadamu  kwa  miili, na wanafanana kwa kuonekana, lakini Waislamu ni marafiki wa Allah swt na watakuwa Peponi milele wakati ambapo Makafiri ni maadui wakubwa wa Allah swt  na watakuwa Motoni milele.  Kujionesha kwao hakumaanishi kuwa watabakia vivyo hivyo daima.  Wale wanaowaabudu masanamu na miungu ambao ndio maadui wakubwa wa Allah swt, yatawafikisha hadi kuingia Jahannam. Lakini wale wanaowafanya marafiki wa Allah swt kuwa marafiki wao, basi Allah swt atawabariki na kuwarehemu.  Ipo Hadith isemayo: Rehema za Allah swt zinateremka pale waja wake wapenzi wanapotajwa, nayo pia inatuonyesha kuwa Allah swt ataonyesha rehema zake na misamaha yake pale Mitume a.s. na Awliya’  wanapoombwa.

Waislamu wote kwa pamoja wanatambua waziwazi kuwa Mitume a.s. na Awliya'  si watu wa kuabudiwa na wala si washiriki wa Allah swt.  Waislamu wanatambua vile vile kuwa wapo waja wa Allah swt ambao hawastahili kuombwa na papo hapo wapo waja wengineo ambao maombi yao hukubaliwa Kwake.  Katika surah Maidah, Ayah ya 35 tunaambiwa: “Tafuteni Wasila wa kunifikia Mimi” Allah swt anamaanisha kuwa Yeye atakubalia ibada za waja wake halisi na kuwapatia kile wakiombacho. Tunapata Hadith sharif iliyonakiliwa na al-Bukhari, Muslim na katika Kunuz ad-daqaiq, isemayo: “Kwa hakika, wapo wacha Mungu halisi wa Allah swt ambapo Yeye anawaumbia kile walacho kiapo; kamwe hawasingizii.” Waislamu wanawachukulia Awliya'  kama Wasila na kutegemea maombi na msaada wao kwa sababu wao wanaamini Ayah na hadith za hapo juu.

No comments:

Post a Comment