Friday 16 August 2013

HURU NI MMOJA WA MAKAMANDA WALIOPEWA JUKUMU LA KUMPIGA VITA IMAMU HUSSEIN



Huru alipewa amri na Yazid bin Muawiyyah (Khalifah wa Mawahhabi) kuongoza kikosi kimojawapo kwa ajili ya kumpiga vita Imam Hussein Mjukuu wa Mtukufu Mtume Mohammad (S.A.W.W) mpaka pale Imam atakapokuwa tayari kuwa chini ya mtawala huyo aliyekuwa mlevi, mzinzi na mcheza kamari.
Kikosi cha Huru kilikuwa cha kwanza kukutana na Imam Hussein lakini alishindwa kuanza mashambulizi, na hivyo kumlazimisha Imam na Msafala wake kwenda katika eneo linaloitwa Karbala na hapo walikuwepo askari wa Yazid wengi zaidi na amri ikatoka kwa Ziyad bin Abih aliyekuwa gavana wa eneo hilo ya kwamba Imam Hussein akatwe kichwa mara moja.
Huru alianza kutetemeka kama kuti, na baadhi ya wenziwe walipomuuliza kuwa, “Je wewe unaogopa kufa?” Huru alijibu, Wallahi hapana, lakini ninaihiyarisha nafsi yangu baina ya pepo na moto.” Kisha hapo hapo alimpiga farasi wake, akaenda kwa Imam Hussein akamuuliza, “Ewe mwana wa Mjumbe wa Mwenyezi Mungu naweza kutubia?” Basi Huru alikubaliwa kuwa miongoni mwa wapiganaji wachache aliokuwa nao Imam Hussein na akawa mtu wa kwanza kuuwawa akiwa upande wa Imam Hussein (a.s).
Nami natamani kuwa kama Huru na niwe wa kwanza kuuliwa nikiwa upande wa haki.

No comments:

Post a Comment