Friday 16 August 2013

MSIBA WA IMAM HUSSEIN (a.s).



Imam Hussein alipouliwa na vikosi vya jeshi vilivyosheheni wanafiki waliotumwa na Yazid bin Muawiyyah, alikatwa kichwa, kikachomekwa juu ya mkuki na kutembezwa mbele ya msafala wa jeshi la Yazid na mateka wao yaani wajukuu na vitukuu wa kike wa Mtume Mohammad (S.A..W.W) miongoni mwao akiwamo Zainabu bint Ally and Sukaina bint Hussein. Mateka hawa wa kike walikuwa wamevuliwa hijabu, kusimangwa na kuzomewa kila walikopita mpaka walipofika makao makuu ya utawala wa Bani Umayyah yaliyokuwa katika msikiti ya Umayyah ulioko Damascus Syria.
Walipofika huko mateka walipewa wasaa wa kujitetea ili wasiuliwe kama walivyouwawa ndugu zao wa kiume. Bi Zainabu alisimama na kuulaumu utawala wa Yazid kutokana na dhulma yake juu ya Uislamu na Waislamu. Akamwambia, “hata mfanye juhudi za kiasi gani kuufifiza utajo wa Ahlulbayt hamtoweza kwani sisi tumeinuliwa na Mwenyezi Mungu na Mtume wake.”
Alisema kweli Bi Zainab kwani leo utajo wa Ahlulbayt unazidi kuongezeka na watu wanaotumia majina yao ni wengi kiasi kwamba karibia kila nyumba utakuta jina la Ahlulbayt limetumika. Kinyume chake unaweza kuzunguka mji mzima na ukakosa mtu anayeitwa Yazid, Muawiyyah, Hindu au Abusufian. Hawa watu wane walikuwa ni msingi wa madhila yaliyowakuta Ahlulbayt Rasulullah na waislamu kwa ujumla.
Kiwiliwili cha Imam Hussein (a.s) kilizikwa na Mashia wake hapo hapo Karbala na kichwa chake kikazikwa na maadui zake katika msikiti wa Banu Umayyah huko Damascus Syria.

No comments:

Post a Comment