Friday 16 August 2013

KUZURU MAKABURI NA FIKRA POTOFU ZA MAWAHHABI



Mawahhabi wanadai kuwa kuzuru makaburi, kuyagusa na kuwaomba watu wema na kutabaruku kwao ni kumshirikisha Mwenyezi Mungu Mtukufu.
Ukweli ni kuwa Kuyagusa makaburi na na kuwaomba wenye makaburi hayo ni shirki tu endapo kama muombaji atakuwa anaamini kuwa marehemu hao wanadhuru na kunufaisha. Lakini waislamu wanampwekesha Allah na wanafahamu kwamba ni Allah pekee ndiye mwenye kudhuru na kunufaisha na wao wanaomba mawalii wa Allah na maimamu ili wawe ni wasila tu na hii sio shirki.
Masunni na Mashia wanakubaliana juu ya hilo tangu zama za Mtume mpaka leo, isipokuwa Mawahhabi ambao ni wanachuoni wa Saudia wameikhalifu ijmai ya waislamu kwa Madhehebu yao mapya ambayo yalianzishwa katika karne ya 18 miladia. Kwa hakika hawa Mawahhabi wamewafitini waislamu kutokana na itikadi yao hii na wamewakufurisha na kuhalalisha kumwaga damu zao, wao huwapiga wazee miongoni mwa mahujaji wa nyumba tukufu ya Allah kwa kusema tu, “Assalaam alayka yaa Rasulullah” na hawamruhusu yeyote kugusa kaburi tukufu ya Mtume wetu. Hii ni dhulma kwa Mtume na waislamu kwa ujumla.
Sayyid Sharafuddin (sheikh wa Shia) alikwenda kuhiji nyumba tukufu zama za Mfalme Abdul Aziz Al-Suud, siku ya idd akaenda kusalimiana na mfalme na akampa mfalme huyo zawadi ya Qur’an iliyofungwa ndani ya ngozi, naye mfalme alifurahi na akaubusu Msahafu huo na kuuweka juu ya paji lake la uso kwa kuuheshimu na kuutukuza. Hapo ndipo Sayyid Sharafuddin alipomuuliza mfalme, ‘ewe mfalme, kwanini unaibusu ngozi na kuitukuza wakati hiyo ni ngozi ya mbuzi?’ Mfalme alijibu, ‘mimi nimeikusudia Qur’an tukufu ambayo imo ndani ya ngozi na sikukusudia kuitukuza ngozi.” Basi Sayyid akasema, “vema ewe mfalme, basi ni hivyo hivyo tufanyavyo sisi tunapoyabusu madirisha ya chumba cha Mtume au milango yake. Sisi pia tunafahamu kuwa hivyo ni vyuma tu, havidhuru wala havinufaishi, lakini huwa tunakusudia kilichopo nyuma ya vyuma hivyo na mbao hizo, kwa hiyo sisi hukusudia kumtukuza Mjumbe wa Mwenyezi Mungu (S.A.W.W) kama wewe ulivyoikusudia Qur’an kwa kuibusu ngozi ya mbuzi ambayo imefunika Qur’an. Basi waalikwa walitoa takbira “Allah akbar” kwa kufurahia maelezo ya sayyid na wakasema umesema kweli. Jambo hili lilimlazimisha mfalme huyo awaruhusu mahujaji kuligusa na kutabaruku kwenye kaburi la Mtume mpaka mwisho wa utawala wake. Mfalme aliyemfuatia akarudia hoja zao dhidi ya Mjumbe wa Mwenyezi Mungu na waja wema wengine.
Basi tatizo la Mawahhabi sio kwamba, hofu yao ni kuwa watu watamshirikisha Mwenyezi Mungu, laa hasha, lakini tatizo lao ni la kisiasa na ni kwa ajili ya kuwapinga waislamu na kuwaua ili kuimarisha ufalme wao na utawala wao dhidi ya waislamu, na Historia ni ushahidi mkubwa juu ya mambo waliyowafanyia umati Mohammad (s.a..w.w).

No comments:

Post a Comment