Friday 23 August 2013

MASAHABA KATIKA JESHI LA USAMAH



Mtume Mohammad (S.A.W.W) aliandaa jeshi ili kulikabiri jeshi la Rumi siku mbili kabla ya kifo chake na akampa uamiri Usamah bin Zaidi ibn Harith, aliyekuwa na umri wa miaka 18. Katika jeshi hilo Mtume aliwaamrisha wakuu wa Muhajirina na Answar kama vile Abubakar bin Quhafah, Umar, Abu-Ubaidah kujiunga na jeshi hilo. Miongoni mwao wapo waliopinga uamiri wa Usamah na wakasema, itakuwaje tuongozwe na kijana ambaye bado hajakomaa?
Hivyo Mtume alitoka akiwa mgonjwa na amefungwa kitambaa kichwani akiyumba kati ya watu wawili akapanda juu ya mimbari na kusema, “Enyi watu ni maneno gani yanayonifikia kutoka kwa baadhi yenu kuhusu uamiri wa Usamah, basi ikiwa mtakebehi kwa kumpa kwangu uamirijeshi Usamah, kwa hakika mlikwisha kebehi kumpa kwangu uamiri baba yake kabla ya mwanawe. Basi namuapa Mwenyezi Mungu kwa hakika Zaid alistahili kuwa amiri na mwanaye pia anastahili kuwa amiri baada yake.
Tazama:
1.     Taqabat cha ibn Saad Juz. 2 uk. 190
2.     Tarikh Ibn al-Athir juz. 2 uk. 317
3.     Tarikh At-Tabari Juz. 3 uk. 226
4.     As-Siratul Halabiyyah ju. 3 uk. 207
Kisha Mtume akawa anawahimiza wafanye haraka kwenda kuungana na jeshi la Usamah ili kuindinda nchi. Lakini mpaka Mtume anafariki Masahaba wengi wakiwemo Abubakar na Umar walikuwa hawajajiunga na jeshi la Usamah, vinginevyo wasingekuwapo Madinah wakati Mtume alipofariki.
Ukweli wa tukio hili ni kuwa kwa mara nyingine tena Baadhi ya Masahaba walipinga amri ya Mwenyezi Mungu na Mtume wake. Rejea Qur’an 33:36 na 59:7 upate maelekezo ya Mwenyezi Mungu juu ya kumtii Mtume wake.
Ikiwa tutataka kufanya mazingatio katika kisa hiki tutagundua kuwa Khalifah Umar bin Khatab ndiye chimbuko la upinzani huu kwani baaada ya kifo cha Mtume alikwenda kwa Khalifah Abubakar na akamtaka amuuzulu Usamah na kumbadilisha na kuweka amiri mwingine. Abubakar akamwambia, “mama yako amekula hasara ewe mwana wa Khatab, waniamuru nimuuzulu na hali ya kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu alimtawalisha?”
Tazama:
1.     Taqabat al-Qubra cha Ibn Saad juz. 2 uk. 190
2.     Tarikh At-Tabari juz. 3 uk. 226

No comments:

Post a Comment