Friday 16 August 2013

KUSUJUDU JUU YA UDONGO



Baadhi ya wapinzani wa USHIA wamekuwa wakipotosha suala hili la Mashia kusujudu juu ya udongo kwa kudai kuwa mashia tunasujudia udongo. Ukweli ni kuwa tunamsujudia Mwenyezi Mungu kwa kusujudu juu ya udongo kama ambavyo nao husujudu juu ya mazuria. Ukisema kwa kusujudu juu ya udongo basi tumeabudu udongo utakuwa unamaanisha vilevile kuwa anayesujudu juu ya zuria atakuwa ameabudu zuria.
Kwetu Mashia sijidah ni kwa ajili ya Allah pekee, na kilichothibiti kwetu sisi na kwa Masunni ni kwamba, kilichobora ni kusujudu juu ya ardhi au kitu kilichoota ardhini kisicholiwa, na wala haisihi kusujudu juu ya kitu kinginecho.
Mtume Mohammad (S.A.W.W)  alikuwa akitandika udongo na makuti kisha kusujudu juu yake, na aliwafundisha Masahaba wake (R.A) wakawa wanasujudu juu ya ardhi na changarawe, na akawakataza kusujudu kwenye nguo au ncha za nguo zao. Mambo haya kwa Mashia yanajulikana bila hata kuulizana dalili. 

No comments:

Post a Comment