Friday 16 August 2013

MIGAWANYIKO (MAKUNDI) YA MASAHABA



Masahaba wa Mtume Mohammad (S.A.W.W) wamegawanyika katika makundi makuu manne:
1.   Masahaba wema
Masahaba hawa walimtambua Mwenyezi Mungu na Mtume wake kwa maarifa ya kweli kabisa na wakamuunga mkono Mtume Mohammad (S.A.W.W) kwa dhati na kusuhubiana naye kwa ukweli katika kauli na utakaso wa moyo katika matendo, na wala hawakugeuka baada yake, bali waliimarika katika ahadi waliyomuahidi. Mwenyezi Mungu na Mtume wake wamewasifia Masahaba hawa kwa dhati kabisa. Mfano wa Masahaba wema ni Abudhar bin Ghiffar, Ammar bin Yasin, Salman Farsii, Mohammad bin Abubakar na Bilal bin Rabah.

2.   Masahaba waliosimu kwa woga au kupenda jambo fulani la waislamu.
Masahaba hawa kuna kipindi walimfuata Mtume na wakati mwingine walimpinga na kumuudhi Mtume kwa kuacha kufuata maagizo yake na kufanya makatazo yake. Maoni yao waliyapa nguvu juu ya hukumu tukufu za Qur’an na Qur’an iliwakemea mara nyingi watu hawa. Mfano wa Masahaba hawa ni Abusufian baba wa Muawiyyah na familia yake.

3.   Masahaba waliokuwa wanafiki
Masahaba hawa walimfuata Mtume Mohammad (S.A.W.W) kwa lengo la kumfanyia vitimbi, wakadhihirisha Uislamu, wakaficha ukafiri, wakajisogeza ili wauvuruge Uislamu na Waislamu. Bila shaka Mwenyezi Mungu ametelemsha sura nzima kuwalaani aina hii ya Masahaba, akawaonya kuwa wataingia katika tabaka la chini la moto wa Jahannam.
Mtume aliwataja baadhi yao na Sunni na Shia tunaafikiana kuwa kuna Masahaba walikuwa wanafiki na walijulikana. Mfano ni Abdallah bin Salun
4.   Masahaba maalumu (Ahlulbayt wa Mtume)
Majina ya Ahlulbayt ni Mtume Mohammad mwenyewe, Ally ibn Abitalib, Fatumah bint Mohammad, Hassan bin Ally na Hussein bin Ally (a.s)
Watu hawa wametakaswa na Allah na kuondolewa uchafu (Qur’an 33:33). Allah amewajibisha kuwasalia sambamba na Mtume (Qur’an 8:41). Allah amewajibisha kwa kila Muislamu kuwapenda watu hawa na ndio malipo ya utume wa Mtume Mohammad (S.A.W.W). (Qur’an 42:23). Wao ndio wenye mamlaka ambao Mwenyezi Mungu ameamrisha kuwatii (Qur’an 4:59). Wamebobea katika elimu (4:59). Wao ni wenye kumbukumbu ambao Mtume ametuagiza kushikamana nao, tena akawafananisha na safina ya Nuhu ambayo mwenye kuipanda ataokoka na mwenye kuikengeuka ataangamia.
Soma; As-sawaiqul Muhriqah ya Ibn Hajar uk. 184 na 234
           Musnad Ahmad Juz. 5 uk. 182
           Kanzul Umaal juz. 1 uk. 44

No comments:

Post a Comment