Tuesday 16 February 2016

MATENDO MATUKUFU KWA MUISLAMU {2}

MATENDO MATUKUFU KWA MUISLAMU {2}

Kama kweli wewe ni mwislamu wa kweli jilazimishe kuwa na matendo yafuatayo.
{1} Unyenyekevu:-
Mtume Mtukufu {s.a.w.w.} amesema: "Kwa hakika unyenyekevu humzidishia kiumbe daraja na cheo kwa Mwenyezi Mungu. Kwa hiyo nyenyekeeni, Mwenyezi Mungu atawahurumieni.

{2}Huruma na upole:
Mtukufu Mtume {s.a.w.w.} amesema: "Mwenye Imani, imechanganyika elimu yake na upole, kwani elimu bila kuwa na upole haina faida yoyote".


{3} Kukaa vyema na watu:
Amesema Imam Jaffer As-Sadiq {a.s.}:- "Muislamu ni ndugu wa Muislamu, asimdhulumu, asimdanganye, asimtupe na kumuacha, asimsengenye, asimfanyie hiyana wala asimnyime".

No comments:

Post a Comment