Wednesday 19 September 2012

Iwapo makundi yanayopinga serikali za Ulaya yatapewa silaha na fedha kutajitokeza hali kama ile inayoshuhudiwa Syria


Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Ali Khamenei leo amemkaribisha Waziri Mkuu wa Syria na ujumbe anaoandamana nao ofisi kwake na kusema kuwa, sababu kuu ya matukio ya kuumiza yanayoshuhudiwa kwa sasa nchini Syria ni Marekani na utawala ghasibu wa Israel. Amesema Harakati ya Nchi Zisizofungamana na Siasa za Upande Wowote ina haki ya kuingilia kisiasa masuala ya Syria na si Marekani, NATO na baadhi ya nchi za Ulaya.
Amesema kuendelea hali ya sasa nchini Syria na mauaji yanayofanywa dhidi ya wananchi havikubaliki. Ameongeza kuwa wanaopaswa kulaumiwa katika masuala ya Syria ni wale wanaotayarisha uwanja wa kutumwa silaha kwa wingi ndani ya Syria na kuyasaidia kwa fedha makundi ya waasi.
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kuwa, kuyapa silaha makundi ya upinzani katika nchi yoyote na kuyasaidia kwa fedha na kipropaganda kutasababisha hali kama ile inayoshuhudiwa kwa sasa nchini Syria. Amesisitiza kuwa iwapo hii leo wapinzani wa siasa za serikali za Ulaya wanaofanya maandamano watapewa silaha na fedha, hapana shaka kwamba kutajitokeza hali kama inayoshuhudiwa nchini Syria.
Ayatullah Khamenei amesisitiza kuwa serikali ya Syria imedhulumiwa katika kadhia ya sasa na kuongeza kuwa, serikali ya Damascus inapaswa kuyafichulia mataifa ya Kiarabu hali ya mambo na njama zinazofanyika nyuma ya pazia dhidi ya nchi hiyo kwa kuwanyima kisingizio cha aina yoyote wapinzani wake na kudumisha mageuzi ya kisiasa.
Kwa upande wake Waziri Mkuu wa Syria Wael Nader al-Halqi amesifu misimamo ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kuhusu masuala mbalimbali na kutoa ripoti kuhusu hali ya nchi yake.
Al-Halqi amesisitiza juu ya kuhuishwa nafasi ya Harakati ya Nchi Zisizofungamana na Siasa za Upande Wowote (NAM) katika masuala ya Syria na akasema, serikali ya Damascus imeazimia kukabiliana na makundi ya kigaidi na kusafisha kabisa maeneo mbalimbali yanakojificha makundi hayo sambamba na kudumisha marekebisho ya kisiasa na mazungumzo ya kitaifa.  

No comments:

Post a Comment