Monday 26 May 2014

SILAHA MPYA YA MAWAHHABI KTK KUKABILIANA NA DALILI PAMOJA NA HOJA ZA WAFUASI WA AHLUL BAIT (A.S) KIZAZI KITUKUFU CHA MTUME (S.A.W.W):

Siku hizi imeibuka kauli mpya ya kiwahhabi nayo ni hii:Washindwa kustahmili vishindo vya Dalili na Hoja zenye nguvu kuhusu mas-ala mbalimbali zitolewazo na Mashia Wafuasi wa Qur'an Tukufu na Itrah wa Mtume (s.a.w.w) yaani Maimam Watukufu ambao ndio Ahlul-Bait wake (a.s),basi utawaona wakihaha na kukimbilia neno lao dhaifu wakisema:HUU NI UONGOOO!
Hilo ndio neno lao ambalo sasa wanalitumia kukwepa dalili na hoja ambazo zinawajia mithili ya vimondo vyenye kuunguza fikra zao na itikadi zao za kiwahhabi ambazo zipo mbali kabisa na uislam kama vile fikra ya kuharamisha kusoma khitma kwa Maiti wetu,au kuharamisha kwao Maulid ya kuzaliwa Mtume wetu (s.a.w.w),au kuharamisha kwa Ziara kwa Mtume (s.a.w.w),au kuharamisha kwao Video na Picha ati haram kutizama video au kupiga picha,au kama vile kuharamisha kwao mwanamke wa Kiislam kusoma elimu ya Dunia kwamba ni haram kwake kuingia University kutafuta elimu ya Secular,au kama vile kuharamisha kwao Kufanya Tawassuli kwa Mtume (s.a.w.w) na kwa Mawalii wa Mweenyeezi Mungu (s.w),au kama vile kuharamisha kwao kuweka makochi ndani ya Nyumba ati ni Haram kwa kuwa Mtume (s.a.w.w) hakukalia makochi,au kama vile kuharamisha kwao Mwanamke kuwa Kiongozi,au kama vile kauli yao kwamba muislam asiyekata suruali au kanzu (kwa panga) na kuvaa kipisi cha kanzu au kipisi cha suruali basi huyo kwa mtazamo wao si muislam ni Kafiri, au yeyote yule anayepinga itikadi yoyote ile ya kiwahhabi ambapo humkafirisha sawa sawa awe Sunni au Shia......na na mengine mengi kuhusu fikra zao zilizo nje bali mbali kabisa na uislam.Tunapozitokomeza fikra kwa hoja na dalili maridadi basi huwa hawana hoja za kiakili wala kunakili zenye mashiko ili kukabiliana na hoja zenye nguvu wanazokumbana nazo hivyo siku hizi wamegundua njia ya kukabiliana na hoja wasizoziweza kuzibatilisha.Njia hiyo ni kusema kwao neno hili:HUU NI UNGOOOO! au utaskia wakisema: UMEDANGANYAAAAA!
Ushari wetu kwa Mawahhabi:
............................................
Ndugu Wahhabi ktk Maumbile:
Acha uwahhabi na fikra za Kiwahhabi za upotokaji ndio utaongoka,na ndio utakuwa
ukisoma post za Wafuasi wa Ahlul-Bait (a.s) na kuzielewa,kisha kufahamu na mwisho kujua ulichokisema.
Ama silaha yako hiyo dhaifu uliyoivumbua siku hizi ili kukabiliana na post zenye hoja kwa kusema HUU NI UONGO !!! Hiyo tunaichukulia sisi kama (kelele),kwa maana namna hiyo utahesabika kuwa (una_make noise),na kumake noise hiyo ni silaha ya Jahili,huyo ndiye hukabiliana na hoja kwa neno
hilo akisena Uongooooooo!!!
Ama Silaha ya mwenye elimu ni kutaja (hoja na dalili zake) ili kubatilisha dalili alizokumbana nazo,na sio kutumia muda wake kumake noise zilizo changanyika
na kelele.
Huu ni ushauri wa bure kwa Wafuasi wa Muhammad Bin Abdil Wahhabi wanaoitwa Mawahhabi ambao siku hizi wanajiita Sunni hali ya kuwa usunni Mwingine na Uwahhabi Mwingine tofauti kabisa kama vile JUA na MWEZI !.
Washukran.

No comments:

Post a Comment