Wednesday 23 April 2014

HADITH YA MTUME KUHUSU MGAWANYIKO WA WAISLAM

Mtume wa Allah alisema, “Wana wa Israel walifarakana na kuwa makundi 71, Manaswara nao wamefarakana na kuwa makundi 72, na umati wangu utafarakana na kufikia makundi 73 na yote yataingia motoni, isipokuwa kundi moja tu.” Ebu niambieni kundi hilo enyi watu wenye akili.
Mimi nashangaa kuona waislamu wote na makundi yao wanaifahamu hadith hii lakini hawaifanyii kazi kwa kufanya utafiti na kubaini ni kundi gani lenye kuokoka na kuachana na makundi mengine yenye kupotoka.
Cha ajabu ni kuwa kila kundi linadai kuwa ndilo lenye kuokoka bila kuleta ushahidi uliosahihi.
Tafadhali tufanye utafiti ili tubaini kundi hili lenye kuokoka ili tujiunge nalo, vinginevyo tutaangamia. Mwenyezi Mungu anasema, “Na wale wanaojitahidi kwa ajili yetu, tutawaongoza kwenye njia zetu” Qur’an 29:69.
Na amesema tena, “Wale ambao husikiliza kauli (zisemwazo) wakafuata zile zilizo njema, hao ndio aliowaongoa Mwenyezi Mungu na hao ndio wenye akili”.
Bila shaka amesema kweli Mjumbe wa Mwenyezi Mungu pale aliposema kuwa fanya utafiti kuhusu dini yako mpaka isemwe kuwa wewe ni maj-nun.

No comments:

Post a Comment