Sunday 20 April 2014

Swali kwa Ahlul-Sunnah wal-Jamaa

Bi Fatumah Zahra (a.s) alifariki miezi mitatu tu baada ya kifo cha baba yake yaani Mtume Mohammad (S.A.W.W) na kuzikwa mahali pasipoeleweka na mpaka leo kaburi lake halijulikani liko wapi. Lakini Sayyidna Abubakar aliyefariki miaka miwili baada ya kifo cha mtume na sayyidna Umari aliyefariki miaka 20 baadaye walizikwa pembeni ya kaburi la Mtume.  Kwa nini mabwana hao wawili wazikwe pembeni ya mtume na wala si bint wake wa pekee (bi Fatumah)? Je ni bint huyo mtukufu ndiye aliomba azikwe mbali na baba yake? Kwa nini? Au waislamu ndio waliozuia bint huyo kuzikwa pembeni ya baba yake?

(soma Sahih al Bukhari Arabic - English juzuu la 5 hadith ya 546 kwa majibu ya maswali hayo). 

No comments:

Post a Comment