Sunday 20 April 2014

Je Abubakar ni kweli kuwa alikuwa ndiye ndugu wa karibu zaidi kwa Mtume kuliko wengine

Miongoni mwa Maswahaba, Sayyidna Abubakar hudaiwa kuwa ndiye bora kuliko wengine kwa sababu ya ukaribu wake kwa Mtukufu Mtume (S.A.W.W). Kama habari hii ni ya kweli kwa nini Mtume Mtukufu hakumchagua yeye kuwa ndugu yake wakati Mtume alipowapanga Maswahaba katika makundi ya wawili wawili na kuwafanya kuwa ndugu, muda mfupi baada ya Hijra, wakati ambapo Mtume Mohammad (S.A.W.W) alimtangaza Imam Ally (a.s) kuwa ndugu yake, akimwambia, “wewe ni ndugu yangu katika ulimwengu huu na ulimwengu ujao”.
Kwa vigezo gani ninyi Masunni mnasema kuwa Abubakar alikuwa ndugu wa karibu zaidi kwa Mtume kuliko wengine?  

Angalia Historia ya Makhalifa, cha Jalaludin Suyuti, Tafsir ya Abdassamad Clarke ya English, ukurasa wa 177 (Taha Publishers)

No comments:

Post a Comment