Sunday 20 April 2014

MAMBO MENGINE YA WAJIBU KATIKA SWALA NA AMBAYO NI RUKNI ZA NGUZO ZA SWALA

6- Qira’a: (Kusoma Suratul Fatiha, yaani: Al-Hamdu, kisha Sura yoyote).
Sura unayoisoma lazima uisome kuanzia mwanzo hadi mwisho, hairuhusiwi kusoma sura nusu, rakaa ya kwanza kisha kusoma nusu iliyobaki katika rakaa ya pili. Bali inatakiwa isomwe sura kamili mwanzo hadi mwisho.
Hapa lazima tuweke wazi: Ukichunguza swala za walio wengi ktk madh-hebu ya Ahlus-sunna, utakuta baada ya kusoma Al-hamdu, basi mtu anasoma sura yoyote ndefu kama Suratul-Baqarah kama Aya kumi kisha anarukuu, kisha anarudi rakaa ya pili anasoma Aya zingine kama ishirini au kumi na tano au zozote atakazoweza kutoka sura nyingine kama vile Suratun-Nisaa kisha anarukuu! Lakini kwa mujibu wa mafunzo sahihi tunayofundishwa au iliyofundishwa na Maimam wetu watukufu (a.s) kutoka Nyumba ya Mtume (s.a.w.w) ambao hakuna shaka yoyote (wala chembe ya shaka kwamba) wanaijua vizuri zaidi swala ya Mtume (s.a.w.w), swala sahihi lazima ktk QIRAA isomwe sura kamili ana sio nusu sura au robo yake au nusu robo. Na hivyo ni bora mwenye kuswali au kuswali kama Imam asome sura fupi ktk swala ambazo atakuwa na uwezo wa kuzisoma mwanzo hadi mwisho na sio kusoma sura ndefu wakati anajua anawaongoza watu ambao wanatofautiana hali zao za kiafya
7-Dhikr
8-Tashahhud
9-Salam
10-Tartib: (Kwa maana kwamba: Swala lazima iswaliwe kwa kufuata utaratibu huu: kuanzia Takbiratul-Ihram, Qira’a, kisha Rukuu, kisha sujud, kisha ukae ktk rakaa ya pili baada ya sajda usome TASHAHUD, ukimaliza ndio usimame kwa kwa ajili ya rakaa ya tatu,kisha ukae ktk rakaa ya mwisho usome TASHAHUD, na baada ya Tashahud umalizie kwa Salam, swala inatakiwa iwe ktk utaratibu huo au tuseme ifuate utaratibu huo, sio unaanza na Takbiratul-Ihram, kisha unaingia sajda, unaacha qira’a na rukuu, namna mwenye kuswali atakuwa hajafuata utaratibu, na atahesabika anaswali anavyotaka na sio inavyotakiwa).

11- Muwalaat: Yaani: Lazima mwenye kuswali ahakikishe anaswali swala yake kwa kufuatanisha vitendo pasina kuacha gape au nafasi baina aya kitendo na kitendo. Mfano: Baada ya Takbiratul-ihram, unaingia moja kwa moja kwenye Qira’a na baada ya Qira’a Al-hamdu na sura na baada ya hapo unaingia moja kwa moja kwenye Rukuu, namna hiyo. Hivyo haitakiwi kutoa Takbiratul-Ihram kisha kukaa kama dakika tano kama haupo kwenye swala kisha ndio usome Al-hamdu na sura kisha baada ya kurukuu unakaa kama dakika kumi ndio unaamua kurukuu, namna hiyo utakuwa hujafatanisha vitendo ktk swala, bali kwa kuachanisha vitendo namna hiyo maana ya swala inapotea kabisa na utatoka nje ya swala na kubatilisha swala yako. Na hata kusoma sura ndefu kama vile suratul-baqara ukiig’ang’ania mpaka uimalize hatua hiyo inaondoa kabisa ufuatanishaji wa vitendo ktk swala, na ndio ikawa ni bora kusoma sura fupi ktk swala kwa kuzikamilisha na sio nusu yake.

No comments:

Post a Comment