Saturday 7 July 2012

Kenya yasema itaendelea kununua mafuta ya Iran

Wizara ya Kawi nchini Kenya imesema itaendelea kununua mafuta ghafi kutoka Jamhuri ya Kiislamu ya Iran licha ya vikwazo vya upande mmoja vya Marekani na Umoja wa Ulaya dhidi ya sekta ya mafuta ya Tehran.
Katibu wa Kudumu wa wizara hiyo, Patrick Nyoike amesema kuwa serikali za Nairobi na Tehran zilitiliana saini mkataba kuhusu biashara ya mafuta mwezi uliopita na ameongeza kwamba Kenya itanunua tani milioni 4 za mafuta ghafi ya Iran kila mwaka. Nyoike hata hivyo hakutoa maelezo zaidi kuhusu mkataba huo kati ya nchi hizo mbili.
Hii ni katika hali ambayo Marekani na nchi za Umoja wa Ulaya zilianza kutekeleza vikwazo vya mafuta dhidi ya Iran hapo jana Julai 1 kama njia ya kuishinikiza Jamhuri ya Kiislamu ya Iran isimamishe miradi yake ya kuzalisha nishati ya nyuklia yenye malengo ya amani. Tehran imesema vikwazo hivyo havitakuwa na athari kwa uchumi wake bali nchi za Ulaya zinazokumbwa na mtitigo wa kiuchumi ndizo zitakazoumia kutokana na kupanda bei ya mafuta katika soko la kimataifa.

No comments:

Post a Comment