Saturday 7 July 2012

UWAHHABI: ASILI NA KUENEA KWAKE sehemu 1


Katika zama za utawala wa Uthmaniyyah (Ottoman Empire), tawala zote ambazo zilikuwapo katika bara la Uarabu, kila jimbo lilikuwa na maofisa waliokuwa wameteuliwa kutoka serikali kuu. Baadaye, kila mkoa isipokuwa Hijaz ilikuwa mikononi mwa wale walioweza kuzinyakua na kuwa tawala za Kifalme.

Imani za Mawahhabi zilizoenezwa na Muhammad ibn ‘Abd al - Wahhab zilikuwa zimeshabadilika kuwa katika sura za kisiasa katika kipindi kifupi katika mwaka 1150 A.H.( 1737) na zilienea Bara zima la Arabia. Baadaye, kwa amri za Khalifa wa Istanbul, Muhammad ‘Ali Pasha, Gavana wa Misri, aliikomboa Arabia kwa msaada wa majeshi ya Misri.

‘Abd al-‘Aziz ibn Muhammad, aliyewaamini Mawahhabi, alitangaza vita kwa mara ya kwanza katika 1205 A.H. (1791) dhidi ya amir wa Makkah, Sharif Ghalib Effendi. Wao walikuwa wamekwisha eneza Uwahhabi kisirisiri hadi hapo. Wao waliwaua na kuwatesa Waislamu wengi mno, kuwachukua wanawake na watoto wao mateka na kuzipora mali zao zote.

Muhammad ibn 'Abd al-Wahhab alitokana na kabila la Bani Tamim. Alizaliwa katika kijiji cha Uyaina karibu na mji wa Huraimila huko katika jangwa la Najd, mwaka 1111 A.H.(1699) na kufa 1206 A.H.( 1792). Hapo awali alikuwa na nia ya kufanya biashara, hivyo alisafiri hadi Basra, Baghdad, Iran, India na Damascus, ambako kote huko alijipatia sifa la jina kama Sheikh wa Najdi kwa sababu za ujanja na tabia yake.Yeye aliona na kujifunza mambo mengi katika sehemu hizi na hivyo akawa na hamu ya kuwa kiongozi mkubwa. Hivyo ili kutaka kutimiza hamu yake hiyo ilimbidi abuni njia moja iliyokuwa tofauti na njia zinginezo ili aweza kutimiza malengo yake, na kwa kujitayarisha kwa hayo, alianza kuhudhuria mihadhara ya maulamaa wa Kihanbali waliokuwapo katika Mji Mtukufu wa Madinah na baadaye huko Damascus kwa kipindi fulani. Wakati aliporejea Najd, alianza kuandika makala juu ya maudhui ya dini kwa ajili ya wanakijiji wake.Katika kuandika makala hayo,yeye alikuwa akiongezea fikara zake alizokuwa amezipata kutoka makundi ya bid’a ya Mu’tazila na wengineo. Wanakijiji wengi waliokuwa masikini majahili, hususan wakazi wa Dar’iyya na chifu wao jahili, Muhammad ibn Sa’ud, walikuwa wakimfuata Muhammad ibn 'Abd al-Wahhab. Waarabu walikuwa wakiheshimu mno ukabila na kwa kuwa Muhammad ibn 'Abd al-Wahhab alikuwa si kutoka kabila maarufu, basi alimtumia Muhammad ibn Sa’ud kama chombo kwa kutangaza fitna yake mpya aliyokuwa ameiita Uwahhabi. Yeye alijitambulisha kama Qadhi (mkuu wa mambo ya dini ) na Muhammad ibn Sa’ud kama Hakim (mtawala). Kwa hila zake alikwishafanya mabadiliko katika katiba yao kuwa wao hawatarithiwa na mtu yeyote yule isipokuwa watoto wao tu.

No comments:

Post a Comment