Thursday 5 July 2012

SWAUMU (FUNGA)


Swaum ni kujizuia na kula na kunywa na vitu vinginevyo katika muda maalum kwa nia ya kujikaribisha kwa Mwenyezi Mungu. Na ni moja wapo kati ya matawi ya dini yaliyo ya lazima.

SWAUMU NA MASHARTI YA KUWAJIBIKA KWAKE
Ni wajibu kwa kila muislaam kufunga mwezi wa ramadhani yanapo kamilika mashartyi yafuatayo:
1- Kubalehe, si wajibu kwa mtu ambae hajafikia balee kuanzia mwanzoni mwa al fajiri ya mweziwa ramadhanikufynga, japo kuwa kauli ya ahwat inasema ya kuwa ni bora kuitimiza ikiwa amenuwia kufunga sunna na akabalee kati kati ya mchana.
2-3- Kuwa na akili timamu na asiwe amezimia, ikiwa atapatwa na wazimu au kuzimia kiasi kwamba nia izingatiwayo kwenye swaumu ikampita na akazindukana katikati ya mchana haita kuwa ni wajibu kwake kufunga siku hiyo, ndio ikiwa alitangulia kutia nia kabla ya kuzimia au kupatwa na wazimu kauli ya ahwat ni kuwa itamlazimu kuikamilisha swaumu hiyo.
4- Asiwe na hedhi wala nifasi, kwa hivyo basi si wajibu kwa mwenye hedhi wala mwenye nifasi kufunga na haita swihi kwa watu hawa wawili funga hata kama hedhi au nifasi hiyo itakuwa ilichukua sehemu fulani ya siku (mchana).
5- Kutokuwa na madhara katika funga, kama akiwa na ugonjwa na ikiwa atafunga ataweza kudhurika ima kwa kuzidisha ugonjwa huo au kuchelewa kupona au kuzi kwa maumivu, na hayo yote huangaliwa kiwango cha kawaida, na hakuna tofauti kati ya kuwa na yakini juu ya kupatikana madhara hayo au kuwa na dhanna juu ya kupatikana madhara na kuwa na ihtimali ipelekeayo kukubali kuwepo kwa khofu itokanayo na vyanzo vya kiakili, katika mambo yote hayo si wajibu kufunga, na ikiwa atafahamu ya kuwa hata pata madhara kwenye nafsi yake lakini akaogopa madhara kwenye heshima yake au mali yake pamoja na kutatizika katika kustahamili hali hizo haita kuwa ni wajibu kwake kufunga, pia ikiwa atakuwa amesongwa na jambo la wajibu lililo sawa na hilo au lenye umuhimu zaidi kama lau kama ataogopea heshima ya mwenziwe au mali yake pamoja na kuwa ni wajibu wake kuihifadhi.
6- Kutokuwa msafiri, lau kama atakuwa katika safari ambayo ni juu yake kupunguza sala, haita kuwa wajibu kwake kufunga bali pia haiswihi funga yake, ndio safari ambayo ni wajibu kukamilisha sala saumu haita anguka yaani ni wajibu kufunga.
Mas’ala: Sehemu ambazo msafiri ana hiari ya kupunguza au kukamilisha sala itamlazimu sehemu hizo kula na swaumu haita swihi sehemu hizo.
Mas’ala: Huzingatiwa katika kujuzu kula kwa msafiri kuwa awe amevuka mpaka wa mji wake, mpaka ambao huzingatiwa katika kupunguza sala na ufafanuzi wake umepita katika mas’ala ya sala ya msafiri.
Mas’ala: ni wajibu –kwa kauli ya ahwat- kukamilisha funga kwa mtu ambae amesafiri baada ya kupinduka kwa jua na swaumu hiyo itatosheleza hakutakuwa na haja ya kuilipa, ama alie safiri kabla ya kupinduka jua haiswihi kwake kufunga siku hiyo- japo kuwa atakuwa hakunuwia safari kuanzia usiku kwa kauli ya ahwat- kwa hiyo inajuzu kwake kula (kuto funga) baada ya kuuvuka mpaka wa mji wake na ni juu yake kuilipa swaimu hiyo.
Mas’ala: Ikiwa masafiri atarudi kwenye mji wake au kupita sehemu ambayo anakusudia kubakia hapo kwa muda wa siku kumi kuna sura zifuatazo:
1- Arudi sehemu hiyo baada ya kupinduka kwa jua, katika hali kama hii si wajibu kwake kufunga.
2- Awe amerudi kabla ya kupinduka kwa jua na katika safari yake alikula, wakati huo si wajibu kwake kufunga pia.
3-Awe amerudi kabla ya kupinduka kwa jua na awe hakula katika safari yake, katika sura kama hii ni wajibu kwake kunuwia funga na afunge kwa muda ulio bakia.
Mas’ala: ikiwa msafiri atafunga kwa kuto fahamu hukumu na akafahamu hukumu hiyo baada ya kumalizika mchana, funga yake itasihi na si wajibu kwake kuilipa na ikiwa atafahamu hukumu hiyo katikati ya mchana saumu itabatilika na mtu alie sahau saumu yake haita swihi.
Mas’ala: Inajuzu kusafiri katika mwezi wa ramadhan hata kama si dharura, na nilazima kuto funga katika safari hiyo, ama katika mambo mengine maalum ya wajibu kauli yenye nguvu inasema haijuzu kusafiri ikiwa jambo hilo ni wajibu kwa kuchukua malipo na mfano wake na vile vile siku ya tatu kati ya siku za itikafu, ama kauli iliyo dhahiri ni kuwa inajuzu kusafiri ikiwa wajibu huo ni kwa sababu ya nadhiri, ama yamini (kiapo) kukiunganisha na hukumu hiyo kuna ishkaali.
Mas’ala: Funga ya wajibu haiswihi kwa msafiri ambae katika safari yake ni wajibu kupunguza sala- pamoja na kufahamu hukumu hiyo- isipokuwa katika sehemu tatu:
1- kufunga siku tatu nazo ni siku ambazo ni baadhi ya siku kumi ambazo zinakuwa badala ya hadyu (mnyama katika hajji ya tamattui kwa yule ambae atashindwa kuitekeleza.
2-Kufunga siku kumi na nane ambazo ni badala ya mnyama ikiwa ni kafara kwa mwenye kutoka arafa kabla ya kuzama jua.
3- Kufunga swaumu ya sunna ambayo imetiliwa nadhiri kuifungakatika safari sehemu nyingine sawa iwe safari au nyumbani, kama ambavyo haiswihi kufunga saumu ya wajibu safarini tofauti na sehemu zilizo tajwa, vile vile haisihi kufunga saumu ya sunna isipokuwa siku tatu kwa ajili ya hajja katika mji mtukufu wa madina na kauli ya ahwat ni kuwa iwe siku ya juma tano, al khamisi, na ijumaa
Mas’ala: Huzingatiwa katika kusihi kwa funga ya sunna ya kuwa mtu asiwe na dhima ya kulipa funga ya mwezi wa Ramadhani, na hakuna madhara ikiwa atakuwa na funga ya wajibu kwa kuchukua malipo au ya kulipa kadhaa au ya kafara na mfano wa hizo, ikiwa anafunga hizo itajuzu kwake kufunga saumu ya sunna katika sehemu zote hizo kwa kauli ya adh’har, kama ambavyo inaswihi kwake funga ya sunna ambayo inaswihi kuifungia safarini hata kama atakuwas na kadhaa ya mwezi wa Ramadhani kutokana na kauli ya ahwat na inajuzu kwake kuchukua ujira kwa ajili ya kufunga swaumu ya wajibu kwa ajili ya mtu mwingine au kumfungia kwa kujitolea kabla ya kulipa swaumu zake za mwezi wa Ramadhani.
Mas’ala: Mzee wa kiume na kike pindi ikiwawia vigumu kufunga inajuzu kwao kula na badala yake watatoa kibaba kimoja cha chakula kila siku ikiwa ni kafara ya siku hiyo, na si wajibu kwako kuilipa siku hiyo, na ikiwa watashindwa kufunga basi funga itaanguka kwao na vile vile wakati huo kafara itaanguka, na hukumu hii hutumika kwa mwenye kiu ( yaani mwenye ugonjwa wa kiu) pia ikiwa funga itamtatiza atatoa kila siku kibaba kimoja cha chakula na ikiwa hakuweza kutoa kibaba hicho pia uwezekano wa kafara kuporomoka upo.
Mas’ala: mama mja mzito ambae siku zake zimekaribia ikiwa ataogopa kupatwa na madhara yeye mwenyewe au mwanae itajuzu kula- bali huenda ikiwa wajibu kama ikiwa funga itamlazimu kupata madhara yaliyo haramishwa kwa mmoja kati ya watu hao wawili- na atatoa kafara kila siku ya kibaba kimoja cha chakula na ni wajibu kwake kuilipa funga hiyo.
Mnyonyeshaji mwenye maziwa kidogo ikiwa ataogopa yeye mwenyewe kupatwa na madhara au mwanae anae nyonya itajuzu kwake kula- bali pengine huenda ikawa wajibu kama tulivyo sema katika mas’ala yaliyo tangulia- na ni juu yake kuzilipa siku hizo na kutoa kafara kwa kila siku kibaba kimoja cha chakula, na hakuna tofauti kati ya mnyonyeshaji sawa awe mama au mtu alie chukua ujira kwa kazi hiyo au mwenye kujitolea kufanya kazi hiyo, na kauli ya ahwat inasema ya kuwa ni lazima hukumu hii itumike pale tu ikiwa njia pekee ya kunyonyesha ni hii na hakuna njia nyingine ya kumnyonyesha mototo isipo kuwa hii hata kama ni kutumia njia nyingine ikiwa hakuna kizuwizi, ama ikiwa kuna uwezekano huo haitajuzu kwake kula.
Mas’ala: Kibaba cha chakula ni sawa na kilo tatu takriban,na ni bora zaidi kiwe ni kibaba cha ngano au unga wangano na kauli ya adh;har ni kuwa inafaa aina yoyote ya chakula hata kama ni mkate.

No comments:

Post a Comment