Thursday 5 July 2012

IMAM MAHDI (a.s)

Yeye ndie Imam na Al-hujjatul-mahdiy (a.s), Mohammad bin Hassan (a.s) na mama yake ni Sayyidah Narjis.
Alizaliwa (a.s) katika mji wa Samarraa usiku wa nusu ya mwezi wa Shaaban, mwaka (255) hijiria.
Na yeye (a.s) ndio hoja wa mwisho wa Mwenyezi Mungu juu ya ardhi na Khalifa wa mwisho wa Mtume (s.a.w) na Imam wa mwisho wa Waislaam, maimam ambao ni kumi na mbili na Mwenyezi Mungu-kwa utashi wake-ameurefusha umri wake mtukufu katika Dunia hii ili ardhi isibakie bila hujja wa Mwenyezi Mungu, kwani kama kusinge kuwa na hujja basi ardhi inge didimia pamoja na watu wake na yeye Imam haonekani kwa watu na Mwenyezi Mungu atamdhihirisha katika Aakhiriz-zamani (Zama za mwisho) baada ya Dunia kujawa na dhuluma na ujeuri (uovu), ili aijaze dunia hiyo kwa uadilifu na usawa.
Hakika Mtume (s.a.w) na maimam watwaharifu walitoa habari ya kuwa yeye atakuwa na ghaibah (Atatoweka na kuto onekana) kwa muda mrefu, na hatakuwa thabiti kwenye juu ya Uimam na wilaya yake na kumuamini isipokuwa yule ambae Mwenyezi Mungu ameujaribu moyo wake kwa Imani, na katika siku za ghaiba yake atakuwa katika hali ya kuwafikishia manufaa watu wa Ardhini kama jua lifikishavyo manufaa na faida zake kwa watu hao hata kama litakuwa limefunikwa na mawingu, na Mwenyezi Mungu atambakiza hai mpaka utakapo fika wakati wa kudhihiri kwake, na hapo kudhihiri kwa idhini yake Mwenyezi Mungu mtukufu na kuimiliki (kuitawala) Dunia yote na kueneza uadilifu na usawa Duniani na kueneza Uislaam na misingi yake yote na kuitekeleza Qur'ani na amri zake kwa watu wote na katika nyanja zake zote za maisha, na hapo Kheri kuenea na saada kutangaa kwenye miji yote na kuwaenea waja wote na kuthibitika kauli yake Mwenyezi Mungu isemayo:
ليظهره علي الدين كله ولو كره المشركون)
Ili auidhihirishe Uislaam juu ya dini zote hata kama washirikina watachukia.
Ewe Mwenyezi Mungu harakisha faraja yake na kufanye kwepesi kudhihiri kwake na utujaalie tuwe miongoni mwa wasaidizi na answari wake.

No comments:

Post a Comment