Monday 9 July 2012

UWAHHABI: ASILI NA KUENEA KWAKE sehemu 2


Katika mwaka 1306 (1888) wakati ambapo kitabu kiitwacho Mir’at al-Haramain kilipoandikwa, kiongozi wa Najd alikuwa ‘Abdullah ibn Faysal, kutokea kizazi cha Muhammad ibn Sa’ud, na Qadhi pia alikuwa ametokana na kizazi cha Muhammad ibn ‘Abd al-Wahhab.

Baba yake mzazi wa Muhammad ibn 'Abd al-Wahhab, ‘Abd al-Wahhab, ambaye alikuwa ni mcha Mungu, ‘alim halisi katika Madina, ndugu yake Sulaiman ibn ‘Abd al-Wahhab na waalimu wake walikuwa wamekwisha tambua kutoka maneno, matendo, ishara na mawazo yake, ambayo mara kwa mara alikuwa akidhihirisha katika sura ya maswali alipokuwa mwanafunzi huko Madina, kuwa atakuwa mpotofu ambaye ataidhuru mno Islam kwa undani katika kipindi kifupi kijacho. Wao wote kwa pamoja walimuasa na kumnasihi aache mawazo yke hayo ya upotoshi na vile vile walikuwa wakiwashauri Waislamu wote kwa ujumla wasimfuate na wajiepushe na Muhammad ibn 'Abd al-Wahhab. Lakini katika muda mfupi tu walikumbana na jambo walilokuwa nalo khofu, na yeye alianza kueneza uzushi wake huo kidhahiri kwa jina la Uwahhabi. Kwa ajili ya kuwapotosha majahili na wapumbavu, yey alijitokeza kwa mawazo ya kurekebisha na kuzua mambo ambayo hayakubaliani na vitabu vya maulamaa wa Islam. Yeye alithubutu kwa kishindo kuwatuhumu Waislamu wa Ahl as-Sunnah wal Jama’a kuwa ni makafiri. Yeye alikuwa akiamini kuwa ni shirk kumwomba Allah swt kwa kupitia Mtume Muhammad s.a.w.w. au Mitume mingine a.s. au ma-Awliya’’ na kuzuru makaburi.

Muhammad ibn 'Abd al-Wahhab alikuwa akimwona mtu yeyote yule anayesali na kuomba karibu na kaburi kuwa ni Mushrik. Yeye alisisitiza kuwa Waislamu wasemao kuwa mtu fulani au kitu fulani mbali na Allah swt kimefanya hivi au vile,kwa mfano, kwa kusema kuwa dawa fulani na fulani zimeponyesha au mimi nimeweza kupata kile nilichokuwa nikihitaji kwa kupitia Wasila wa Mtume Muhammad s.a.w.w. au au mawali fulani fulani basi hao wote ni Mushrik. Ingawaje waraka wa Muhammad ibn 'Abd al-Wahhab hazikuwa chochote isipokuwa ni uongo na fitina tu, lakini majahili hawakuweza kutofautisha baina ya ukweli na uongo, wale wasiokuwa na kazi, wazururaji, majahili, wenye kuvizia bahati na wenye nyoyo ngumu walizipokea mawazo yake na kujiweka bega kwa bega pamoja naye na kuamini wale Waislamu waliokuwa katika njia sahihi kuwa wote kwa pamoj ni makafiri.

Wakati Muhammad ibn 'Abd al-Wahhab alipowaomba ruhusa watawala wa Dar’iyya kutaka kueneza imani zake za uzushi kwa kupitia utawala wao, wao walimpokea kwa mikono miwili kwa matumaini ya kupanua eneo la utawala na kuzidi kwa nguvu zao.  Wao walijitolea kwa hali na mali kueneza imani hizo kila mahala.  Wao hata walithubutu kutangaza vita dhidi ya wale wote waliokuwa wakimkataa na kumpinga. Watu  Mahayawani na  wateka nyara wa jangwani walikuwa wakishindana katika kujiunga na jeshi la Muhammad ibn Sa’ud wakati pale iliposemwa kuwa ni halali kumwua na kupora mali za Waislamu. Katika mwaka 1143 ( 1730 ), Muhammad ibn Sa’ud pamoja na Muhammad ibn 'Abd al-Wahhab wakishirikiana kwa pamoja walifikia maafikiano kuwa wale wote ambao hawata kubalia Uwahhabi, basi watakuwa ni makafiri na Mushrik, na hivyo ilikuwa ni halali kwao kuwaua na kutaifisha mali yao yote, na walitangaza rasmi amri hiyo miaka saba iliyofuatia.  Hapo ndipo Muhammad ibn 'Abd al-Wahhab alipoanza kutunga uzushi wa ijtihad pale alipokuwa na umri wa miaka thelathini na miwili na aliitangaza kidhahiri pale alipokuwa na umri wa miaka arobaini.

No comments:

Post a Comment