Sunday 27 September 2015

SHIA NA QUR’AN TUKUFU

SHIA NA QUR’AN TUKUFU
Shia wanaitakidi kuwa Qur’an ni wahyi wa Mwenyezi Mungu uliteremshwa kutoka kwa Mwenyezi Mungu katika ulimi wa Nabii mtukufu kwa kubainisha kila kitu, nayo ni muujiza wa milele ambao wanadamu wameshindwa kupambana nao katika balagha, fasaha na katika ukweli na maarifa ya hali ya juu, haiguswi na mabadiliko, mageuzi wala upotovu, na hii ambayo iko mikononi mwetu tunayoisoma ndio ile ile Qur’an iliyoteremshwa kwa Nabii (s.a.w.w.) na atakaye dai yasiyokuwa hayo basi ni muongo au ni mwenye kukosea au amechanganyikiwa na wote hawako katika uongofu, hakika hayo ni maneno ya Mwenyezi Mungu ambayo hayapatwi na upotovu kwa hali yeyote.
Sheikhul Muhadithiina Muhammad bin Ali Al-Qummiy ambaye amepewa lakabu ya Asuduuq amesema: Itikadi yetu katika Qur’an ambayo ameiteremsha Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa Nabii wake Muhammad (s.a.w.w.) ni ambayo iko baina ya jalada mbili na ambayo iko kwa watu na sio zaidi ya hayo... na anayetunasibishia kuwa tunasema zaidi ya haya basi ni muongo.
Assayid Al-Khuiy ambaye ni mmoja wa marajii wakubwa wa kishia katika zama hizi anasema, “iliyomashuhuri baina ya Waislamu ni kutokuwepo opotoshaji katika Qur’an na iliyopo mikononi mwetu ni Qur’an yote iliyoteremshwa kwa Nabii (s.a.w.w.).
Ama Sheikh Muhammad Al-Ghazaaliy anasema katika kitabu chake Difau anil-aqiydati wa shariah dhidu matwa’inil-mustashiriqiyna “Nimesikia kutoka kwa hawa miongoni mwa watu ambaye anasema katika majilisi za hadhara: Hakika Shia wana Qur’an nyingine ambayo ni zaidi na inapunguza Qur’an yetu iliyo maarufu nikamwambia: Iko wapi hii Qur’an? na kwa nini majini na wanadamu hawakuona nakala yake kwa muda wote huu mrefu? Huu uongo ni wa nini?... kwa nini kusingizia wahyi na watu. Ama hadithi ambazo sio sahihi ambazo baadhi wanaweza kuzitegemea ambazo zinaeleza kupotoshwa kwa Qur’an na ambazo zipo katika vitabu vya hadithi katika Shia, hakika ni dhaifu na hazikubaliwi na mfano wake ni nyingi katika vitabu sahihi vya Ahlus-Sunna na tutaonyesha mifano ya hayo katika Sahih Bukhariy, tunatanguliza hadithi walizozipokea kuhusu kusahau Mtume (s.a.w.w.) katika baadhi ya Aya:-
Kutoka kwa baba yake kutoka kwa Aisha amesema: Mtume wa Mwenyezi Mungu alimsikia mwanaume anasoma sura usiku akasema! Mwenyezi Mungu amrehemu amenikubusha Aya kadha wa kadha nilikuwa nimezisahau katika sura kadha wa kadha. Vile vile katika Sahih Bukhariy ni kwamba, walipokuwa wanakusanya Qur’an hawa kupata sehemu ya Surat Tauba isipokuwa kwa Khuzaimah Al-Answariy na hii inapingana na ukweli unaosema kuwa Qur’an imepokewa kwa Tawatiri na wala sio kwa Riwaya za Ahadi (mtu mmoja):
Al-ahzaab nilikuwa namsikia Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) anaisoma usiku kucha isipokuwa kwa mtu mmoja Khuzaimah Al-Answariy Khuzaima Al-Answariy ambaye Mtume wa Mwenyezi Mungu amejaalia ushahidi wake kuwa ni sawa na ushahidi wa waumini wawili. 
Nilifuatalia kukusanya Qur’an kutoka kwenye vipande vya nguo, mifupa, magome kwa watu waliohifadhi hadi nikakuta Aya mbili za sura ya Tawba kwa Khuzaimah Al-Answariy na sikuipata kwa yeyote asiyekuwa yeye.

Haya ni maelezo ya wazi kuwa Mashia tunaamini kuwa Qur’an tuliyonayo ni kamilifu kama ilivyoshuka kwa Mtume Muhammad (s.a.w.w). Na hadith zinazodai kuwa Qur’an ni pungufu au zaidi ni dhaifu na za uongo na zinapatikana zaidi katika vitabu vya Ahlulsunah waljamaa kuliko katika vitabu vya Shia. Hivyo tusisingiziane imani mbovu ili tu kuzua mtafaruku au kuzuia watu wasijue ukweli. 

UISLAMU UNAPINGA KILA AINA YA UBAGUZI

UISLAMU UNAPINGA KILA AINA YA UBAGUZI
Mtume wetu (s.a.w.w.) amesema: “Waarabu wasijigambe kwamba wao ni bora kwa wasio Waarabu na kinyume chake; na weupe wasijigambe kwa ubora kwa weusi na kinyume chake. Ubora uko tu katika elimu na uchaji.
Katika Qur’ani Tukufu Allah (swt) anasema:
 Enyi watu! Hakika tumekuumbeni ninyi mume na mke; na tumekufanyeni mataifa na makabila ili kwamba mpate kujuana; hakika aliye mbora sana miongoni mwenu mbele ya Allah ni yule amchae Allah zaidi…” (49:13).
Vile vile katika Sura hiyo hiyo ndani ya Qur’ani Anasema:
 Kwa hakika Waumini wote ni ndugu, basi patanisheni baina ya ndugu zenu na mcheni Allah ili mrehemiwe.” (49:10).
Kwa hiyo, watu wote, Waasia, Waafrika, Wazungu, Waamerika weupe, weusi, wekundu au manjano, makabila yote ambayo ni Waislamu ni ndugu, na hakuna hata mmoja anayeweza kudai ubora juu ya mwingine.
Kiongozi mkubwa wa Waislamu, Mwisho wa Mitume, alitenda juu ya msingi huu. Alionyesha mapenzi yake makhususi kwa Salman Farsi wa Iran, Suhaib wa Asia ndogo, na Bilal wa Abysinia (Uhabeshi – Ethiopia ya sasa).
Na kwa upande mwingine alimpuuza Abu Lahab (ambaye jina lake lina maana ya Baba wa Miali ya Moto), ami yake mwenyewe ambaye amelaaniwa katika Sura ya Qur’ani Tukufu ambayo inasema:
 Imeangamia mikono miwili ya Abu Lahab! Naye amekwisha angamia…” (111:1).
Ulimwengu umeshuhudia matatizo ya taratibu mbaya mno katika nchi za Maghribi ambayo yalikuwa ni matokeo ya ubaguzi wa rangi. Katika nchi hizo weusi hawaruhusiwi kwenye mahoteli, migahawa, makanisa, na sehemu nyingine za mikusanyiko iliyokusudiwa kwa weupe tu. Uislamu ulipiga marufuku taratibu hizo za kikatili miaka 1400 iliyopita na kutangaza kwamba Waislamu, bila kujali kabila, rangi, au utaifa wote ni ndugu. Hivyo Waarabu wakienda kombo, nitawalaumu, na nitakuwa rafiki wa Mashi’a wawe wa Iran au nchi yoyote duniani.

Kiukweli Uislamu hauruhusu kuwatendea maovu hata watu wasiokuwa waislamu na hivyo kuhimiza kuwafanyia uadilifu watu wasiokuwa Uislamu. 

KIINI CHA MACHAFUKO KATIKA UISLAMU

KIINI CHA MACHAFUKO KATIKA UISLAMU
Mpaka katikati ya karne ya kumi na saba (17) Uislamu ulikuwa na nguvu kubwa za kisiasa duniani. Nguvu hii ilitokana na mwenendo wa Serikali ya Wauthman (Dola ya Wauthmani) ambayo ilikuwa imetawala eneo kubwa la Afrika Kaskazini, Bara Arab, nchi za Ulaya Mashariki kama vile Bulgaria, Hungaria, Yugoslavia, Romania, na hata sehemu za Urusi n.k.
Lakini watawala wa mataifa ya Kikristo, hususan wa Ulaya Magharibi, walipoona Uislamu unazidi kuenea na kupanda mbegu safi ya utamaduni wake, wakaona vibaya kwa kuwa mwenendo wa Kiislamu una nguvu kubwa na ni vigumu kuwafanya watu kubadilika baada ya kuingiwa na silika ya Kiislamu. Kwa haraka kabisa wakaunda vikundi vya wataalamu mbali mbali vikiongozwa na Serikali zao kuzunguka katika mataifa ya Kiislamu kwa nia ya kutafiti njia itakayowasaidia kuondoa mshikamano wa Waislamu. 
Maadui walifanya uchunguzi kwa uyakinifu na wakabainikiwa kuwa nguvu za Waislamu hutokana na umoja wao ambao kwa hakika ndio msingi wa mafanikio ya kila tabaka. Pili, ni kuwa waliona wazi kuwa Waislamu ni wenye kujenga tabia ya kuaminiana wao kwa wao, kwa hali hiyo isingekuwa rahisi kuwaingia na kuwasaliti. 
Hatua ya kwanza ikawa kupenyeza baadhi ya watu wao ndani ya Waislamu na kujifanya Waislamu kusudi wapate imani ya Waislamu. 
Hatua iliyofuatia ilikuwa ni wao kuingia katika vyeo vya Kiislamu na kujifunza elimu humo. Inaripotiwa kuwa Napoleon alifika Misri na kujifunza katika kitivo cha Sheria cha Chuo Kikuu cha Al-Azhar. 
Vikundi vingine vilijihusisha na kutafiti njia za kuingia ukoloni katika maeneo ya Kiislamu na kuziangusha Serikali zake. Waitaliano waliingia Libya na kuanzisha utawala wao huko. Waingereza waliuangusha utawala wa Tippu Sultan mwaka 1799 na kuondolea mbali matumaini ya kisiasa ya Waislamu katika Bara Hindi. Kuanzia hapo Ubeberu wa Kiingereza ulitashahari katika eneo hilo. Katika miaka ya 1894 Waingereza walifanikiwa kuwapata vibaraka ambao walijitolea kuutumikia utawala wao dhidi ya Uislamu. Ghulam Ahmad wa Kadian akaunyenyekea Ukafiri wa Kiingereza kufikia hadi ya kusema baada ya kumwamini Mwenyezi Mungu imani ya pili ni kumwamini Malkia.
Uturuki nako Serikali iliangushwa. Hii ilikuwa baada ya vibaraka kuingia katika ngazi za juu katika Serikali. Adhana ilipigwa marufuku baada ya mapinduzi. Katika utaratibu huu maadui wa Uislamu waliweza kufanikiwa kuuvunja umoja wa Waislamu kwa kuwatumia wanachuoni na watu maarufu katika wenye tamaa. Na huo basi ulikuwa mwanzo wa machafuko. Mpaka hivi sasa, na katika kila nchi zenye Waislamu na ambazo zinatawaliwa na watu wenye nia mbaya na Uislamu, wanawatumia Waislamu wenye mawazo ya kitumwa.
Miongoni mwa watu waliotumiwa kuvunja nguvu za waislamu kwa kuanzisha vita vya wenyewe kwa wenyewe katika kila kona ya bara Arabu alikuwa Muhammad Abdulwahhabi akishirikiana na mfalme wa Najdi, kazi ambayo wafuasi wake wanaendelea nayo mpaka sasa. Kila eneo lenye Mawahhabi amani imetoweka, anzia Urusi, Pakistan, Afghanistan, India, China, Iran, Iraq, Yemen, Kuwait, Saudi Arabia, Syria, Misri, Libya, Tunisia, Somalia, Lebanon, Jordan, Morocco n.k. kote kuna matukio yametokea ya kuwalipua na kuwashambulia watu wasiokuwa na hatia kwa madai tu ya kutetea madhahebu yao au kupambana na makafiri, cha ajabu utakuta wanaoitwa makafiri ni waislamu wenzao wa kishia na kisunni.

KIINI CHA MACHAFUKO KATIKA UISLAMU

KIINI CHA MACHAFUKO KATIKA UISLAMU
Mpaka katikati ya karne ya kumi na saba (17) Uislamu ulikuwa na nguvu kubwa za kisiasa duniani. Nguvu hii ilitokana na mwenendo wa Serikali ya Wauthman (Dola ya Wauthmani) ambayo ilikuwa imetawala eneo kubwa la Afrika Kaskazini, Bara Arab, nchi za Ulaya Mashariki kama vile Bulgaria, Hungaria, Yugoslavia, Romania, na hata sehemu za Urusi n.k.
Lakini watawala wa mataifa ya Kikristo, hususan wa Ulaya Magharibi, walipoona Uislamu unazidi kuenea na kupanda mbegu safi ya utamaduni wake, wakaona vibaya kwa kuwa mwenendo wa Kiislamu una nguvu  kubwa na ni vigumu kuwafanya watu kubadilika baada ya kuingiwa na silika ya Kiislamu. Kwa haraka  kabisa wakaunda vikundi vya wataalamu mbali mbali vikiongozwa na Serikali zao kuzunguka katika mataifa ya Kiislamu kwa nia ya kutafiti njia itakayowasaidia kuondoa mshikamano wa Waislamu.
Maadui walifanya  uchunguzi kwa uyakinifu na wakabainikiwa kuwa nguvu za Waislamu hutokana na umoja wao ambao kwa hakika ndio msingi wa mafanikio ya kila tabaka. Pili, ni kuwa waliona wazi kuwa Waislamu ni wenye kujenga tabia ya kuaminiana wao kwa wao, kwa hali hiyo isingekuwa rahisi kuwaingia na kuwasaliti.
Hatua ya kwanza ikawa kupenyeza baadhi ya watu wao ndani ya Waislamu na kujifanya Waislamu kusudi wapate imani ya Waislamu.
Hatua iliyofuatia ilikuwa ni wao kuingia katika vyeo vya Kiislamu na kujifunza elimu humo. Inaripotiwa kuwa Napoleon alifika Misri na  kujifunza katika kitivo cha Sheria cha Chuo Kikuu cha Al-Azhar.
Vikundi vingine vilijihusisha na kutafiti  njia za kuingia ukoloni katika maeneo ya Kiislamu na kuziangusha Serikali zake. Waitaliano waliingia  Libya na kuanzisha utawala wao huko. Waingereza waliuangusha utawala wa Tippu Sultan mwaka 1799 na kuondolea mbali matumaini ya kisiasa ya  Waislamu katika Bara Hindi. Kuanzia hapo Ubeberu wa Kiingereza ulitashahari katika eneo hilo. Katika miaka ya 1894 Waingereza walifanikiwa kuwapata  vibaraka ambao walijitolea kuutumikia utawala wao dhidi ya Uislamu. Ghulam Ahmad wa Kadian  akaunyenyekea Ukafiri wa Kiingereza kufikia hadi ya kusema baada ya kumwamini Mwenyezi Mungu  imani ya pili ni kumwamini Malkia.
Uturuki nako Serikali iliangushwa. Hii ilikuwa baada ya vibaraka kuingia katika ngazi za juu katika Serikali. Adhana ilipigwa marufuku baada ya mapinduzi. Katika utaratibu huu maadui wa Uislamu waliweza  kufanikiwa kuuvunja umoja wa Waislamu kwa  kuwatumia wanachuoni na watu maarufu katika  wenye tamaa. Na huo basi ulikuwa mwanzo wa machafuko. Mpaka hivi sasa, na katika kila nchi zenye Waislamu na ambazo zinatawaliwa na watu wenye nia mbaya na Uislamu, wanawatumia Waislamu wenye mawazo ya kitumwa.

Miongoni mwa watu waliotumiwa kuvunja nguvu za waislamu kwa kuanzisha vita vya wenyewe kwa wenyewe katika kila kona ya bara Arabu alikuwa Muhammad Abdulwahhabi akishirikiana na mfalme wa Najdi, kazi ambayo wafuasi wake wanaendelea nayo mpaka sasa. Kila eneo lenye Mawahhabi amani imetoweka, anzia Urusi, Pakistan, Afghanistan, India, China, Iran, Iraq, Yemen, Kuwait, Saudi Arabia, Syria, Misri, Libya, Tunisia, Somalia, Lebanon, Jordan, Morocco n.k. kote kuna matukio yametokea ya kuwalipua na kuwashambulia watu wasiokuwa na hatia kwa madai tu ya kutetea madhahebu yao au kupambana na makafiri, cha ajabu utakuta wanaoitwa makafiri ni waislamu wenzao wa kishia na kisunni.

Saturday 26 September 2015

NAMNA NABII IBRAHIM (A.S) ALIVYOFUNDISHA KUHUSU MWENYEZI MUNGU

NAMNA NABII IBRAHIM (A.S) ALIVYOFUNDISHA KUHUSU MWENYEZI MUNGU
Namna Nabii Ibrahiim (AS) alivyoonesha kuwa, nyota, mwezi na jua si miungu. Na hizi ni hoja zetu tulimpa nabii Ibrahiimu juu ya watu wake. Usiku ulipomwingilia akaona nyota. Akasema "hii ni Mola wangu" Ilipotua akasema " Siwapendi miungu wanaopotea" Na siku ya pili alipouona mwezi akasema: "Huu ndiye Mola wangu" Ulipotua akasema "Asiponiongoa Mola wangu, bila shaka nitakuwa miongoni mwa wapotofu. Na siku ya tatu alipoliona jua, akasema Hili jua ndilo Mola wangu. Huyu ni Mola wangu mkubwa, lilipotua akasema Enyi watu wangu! Mimi simo katika hayo mnayoyashirikisha na Mwenyezi Mungu. Mimi nimeuelekeza uso wangu kwa yule aliyeumba mbingu na ardhi, hali ya kuwa nimewacha Dini ya upotevu. (6:74-83).
Namna nabii Ibrahiim (AS) alivyoonesha washirikina kuwa masanamu si miongu. "Wakasema: Je wewe umeifanya hivi miungu yetu, ee Ibrahiim? Akasema: Siyo bali amefanya huyu mkubwa wao, basi waulizeni kama wanaweza kunena! Basi wakajirudi nafsi zao na wakasema Hakika ninyi mlikuwa katika madhalimu" (26:58-64).
Namna Ibrahiimu alivyombwaga mfalme kwa hoja: "Hukumsikia yule aliyehojiana na Ibrahiim juu ya Mola wake kwa sababu Mwenyei Mungu alimpa ufalme? Ibrahiimu akasema "Mola ni yule anayehuisha na kufisha" Yeye akasema "Mimi pia nahuisha na kufisha" Ibrahiimu akasema: "Mwenyezi Mungu hulichomoesha jua mashariki, basi wewe lichomoze magharibi". Akafedheheka yule aliyekufuru na Mwenyezi Mungu hawaongozi watu madhalimu"(2:258).

Umuhimu wa kufikiri kwa kujenga hoja: Qur'an kwa nafsi yake inajieleza mara kwa mara kuwa hoja za ujumbe wake ziko wazi kwa watu wanaotumia akili, wenye kuzingatia, wenye kutafakari. "Na hakuna atakayeamini ila kwa idhini ya Mwenyezi Mungu, naye hujaalia uchafu uwaendee wale wasiotumia akili zao"(10:100).
Katika aya hizi tunajifunza kuwa Mwenyezi Mungu ni wa milele, hafi hata kwa dakika moja, haonekani kwa macho, yeye ni muweza wa kila kitu. Na kwamba vingine vinauwezo kiasi walivyowezeshwa na Mwenyezi Mungu tu. Hivyo tumwabudu Mwenyezi Mungu muumba na sio miungu ya kubuni na watu wenzetu kama wafanyavyo wakristo wanao dai kuwa Yesu ni mwana wa Mungu na ni Mungu mwenyewe.

SIDDIQ (WAKWELI) NI WATATU TU, KATIKA UISLAMU

SIDDIQ (WAKWELI) NI WATATU TU, KATIKA UISLAMU
Imam Muhammad ibn Ismail al-Bukhari katika kitabu chake Tarikh al-Kabeer, ametaja maneno ya Mtume wetu (s.a.w.w.) yalioelezwa na Ibn Abbas kuwa watu watatu ni “Siddiq”: hakika bila shaka Hizqil  mwamini kati ya watu wa Firauni, Habib al-Najjar mwamini kati ya ukoo wa Yaseen na Ali Ibn Abi Talib ndio wa kweli.
Nawab Siddiq Hasan Khan wa Bhopal katika kitabu chake cha tafsir  kiitwacho Tafsir Fathul Bayan ameeleza hadithi kutokana na Ibn Abi Laila, na hadithi hiyo hiyo imetolewa na Tafsir Durr-e-Manthur  ya Jalaluddin Suyuti lakini iko tafauti ya baadhi ya maneno tu,  wanasema kwamba “Ni watukufu watatu tu ambao hawakukufuru au  kumuasi Mwenyezi Mungu kabisa hata kiasi cha kupepesa macho na  walikimbilia kuamini dini ya haki. Miongoni mwao na wa mwanzo na bora wao ni Ali Ibn Abi Talib; wa pili mwamini katika kaumu ya Firauni, na watatu wao anatokana na ukoo wa Yaseen. Na watatu hawa tu ni Siddiq (Washuhudiawo na kweli).”
Wa kweli au Siddiq hapa inakusudiwa, ni watu wa mwanzo kusilimu katika kaumu yao na tena hawakuwahi kufanya dhambi, bali walipousikia Ukweli wa Uislamu waliupokea mara moja bila kusita na wakaufuata moja kwa moja bila kuchanganya na mila zao zingine.

Nakuombeni tufuate nyendo zao, nasi tuingie katika Uislamu moja kwa moja bila kuchanganya na mila zingine za ajabu ajabu.

Friday 25 September 2015

IMANI YA KUWEPO KWA MANABII WA MWENYEZI MUNGU

IMANI YA KUWEPO KWA MANABII WA MWENYEZI MUNGU
Inapothibitika kwamba Muumba wetu ni Mwenyeezi Mungu Mtukufu, na ni Muumba Mwenye Hekima, haiwezekani kwa viumbe wake kumuona, kumgusa, kumwenza au kuzungumza Naye, hivyo, ni lazima kwamba Manabii na Mitume Wake wawe ni miongoni mwa viumbe wake, ili kwamba waweze kuwawaidhi waja Wake yale mambo yenye manufaa kwao, na ambayo ni muhimu kwa kuwepo kwao, na ikiwa hatutawafuata, itatuongoza kwenye mauti.
Hivyo, ni lazima Mwenyeezi Mungu kwa ajuaye kuwapelekea viumbe vyake Mitume wake, ambao wanawaamrisha mema na kuwakataza maovu, nao watabaki na kuendelea kuwepo katika dunia hii kutoka Kwake. Wao ni Mitume na Manabii wake miongoni mwa viumbe wake. Wanawafundisha watu hekima, na wanajishirikisha pamoja nao katika mambo yao.
Mwenyeezi Mungu amewapa elimu, hekima, hoja na dalili, kwa mfano, wanawahuisha maiti, wanawaponyesha vilema n.k. Hivyo, dunia haiwezi kuwa tupu bila ya "Hoja"(Imamu) ya Mwenyeezi Mungu, ambaye ana elimu ni shahidi wa maneno na vitendo vya haki vya Mtume, na uadilifu wa Mwenyeezi Mungu.
Tunaamini kwamba dunia haiwezi kuwa tupu bila ya "Hoja" (Maimamu) Zake zinazotoka katika kizazi cha Mitume tu;
Vile vile Mwenyezi Mungu humchagua Mtume Wake miongoni mwa kizazi cha Mitume. Ni hivyo, kwa sababu Mwenyeezi Mungu ameweka njia imulikayo kwa wanaadamu. Ameumba kizazi tohara na kisafi, na miongoni mwao amewachagua Mitume na Manabii Wake ambao ni wateule wa Mwenyeezi Mungu na mfano bora kwa wanaadamu.

Walitoharishwa tangu kwenye manii ya wazazi wao na wakawekwa salama katika mifuko ya uzazi ya mama zao. Uchafu wa ujinga haukuwagusa, wala hawakuchanganyika nao baadaye, kwa sababu Mwenyezi Mungu amewapa daraja tukufu na adhimu kabisa.
Hivyo, yeye ambaye ni hazina ya elimu ya Mwenyeezi Mungu, mdhamini Wake wa yasioonekana, mwenye kujua siri Zake, Hoja Yake kwa viumbe Vyake, kinywa chake na ulimi Wake, lazima awe nazo sifa Zake. Kwa hivyo, Hoja (yaani Imamu) anatoka miongoni mwa vizazi vya Mitume, ili kwamba kwa kuwa nayo elimu ya Mtume aweze kuwa badala ya Mtume, na amrithi kama wasii wake, ili kwamba ikiwa watu watakataa kumkubali, aweze kuwanyamazisha.
Elimu ya Mtume wa mwenyeezi Mungu (s.w.t.) ambayo watu walikuwa nayo, ilidumu (baada ya Mtume Mtukufu) kwa muda mfupi, kwa sababu kwa haraka tofauti kati yao zikatokeza, na wakaanza kutumia maoni na fikara zao wenyewe. Kama wangelimkubali Hoja (Imamu au Khalifa) wakamtii na kumfuata, haki ingesimamiwa na Hoja, tofauti na mabishano yangeondoka, dini ingekuwa imara na salama, na imani ingeshinda shaka.
Baada ya kufariki kwa Mtume wa Mwenyeezi Mungu (s.w.t.), watu hawakuungana kumfuata Hoja huyo, wala kumtii. Kwa hakika, hakuna Mtume au Nabii wa Mwenyeezi Mungu, ambaye umati wake hawakutofautiana baada yake. Sababu ya tofauti zao miongoni mwao ni kwa ajili ya kupinga na kujitenga na Hoja, ambaye amechaguliwa baada ya Mtume wa Mwenyeezi Mungu.

HISTORIA YA MUHAMMAD ABDULWAHABI (2)

HISTORIA YA MUHAMMAD ABDULWAHABI (2)
Muhammad bin Abdul Wahhab alikuwa haraka sana. Alibaleghe kabla hajatimiza miaka kumi na mbili. Wakati huo huo baba yake alimposea mke.  Inasemekana kuwa alihifadhi Qur’an kabla hajafikia  umri wa miaka kumi (10). Alijifunza elimu ya Fiqhi kwa Babake Sheikh Abdul Wahhab bin Sulayman, mwanachuoni mcha Mungu wa madhehebu ya  Hambal. Kadhalika alijifunza elimu za Tafsiri ya  Qur’an na hadithi n.k.
Baadaye alisafiri kwa njia ya biashara na kujifunza  elimu katika miji ya Madina, Basra na Baghdad (Iraq) na akafika Iran kwa madhumuni ya kujifunza  Tasawwuf.
Baba yake pamoja na Masheikh zake walikuwa wakimtabiri kuwa atatokea kuwa mtu  mpotoshaji kutokana na mwenendo wake wa kubishana  nao katika masuala mbali mbali ya kidini, na kwa kuwa alikuwa hana nidhamu wala adabu ya kidini. 
Masheikh zake pamoja na baba yake walikuwa wakiwatahadharisha watu kuwa wasikae pamoja naye wala kusikia maneno yake kwa kuwa yalikuwa ni ya  kupotosha. Kaka yake, Sheikh Sulayman bin Abdul  Wahhab, aliandika kitabu “AL-SAWAA’IQ AL- ILAHIYAH FI AR-RADD ALA AL-WAHHABIYYAH” kupinga mafundisho ya uchafuzi na uzushi ya  mdogo wake.
Kila alipozusha hoja ya upotovu mbele ya Masheikh zake walimfedhehesha. Katika kitabu chao kinachoeleza maisha yake, Mawahhabi wenyewe wanakiri kuwa alikuwa amegombana na kubishana na baba yake na pia kaka yake. Soma katika kitabu “SHEIKH MUHAMMAD ABDUL WAHHAB” uk. 26 na tena katika kitabu “FITNAT-UL-WAHHABIYYAH” uk. 4.
Katika kitabu “MAAL-WAHHABIYYIN” uk. 18, Al-Allamah Jaafar Subhaniy ameandika yafuatayo: “Hakika Muhammad bin Abdul Wahhab hakuwa wa mwanzo katika kuanzisha mwenendo huu. Isipokuwa yeye alichukua fikara zilizotawanywa na Ibn Taimiyya  na mwanafunzi wake Ibn Qayyim na Ibn Abdul Hadi; akajengeka katika mfumo wa maelekezo yao  kutokana na kupitia vitabu vyao mara kwa mara, hivyo akaibuka kuwa kielezeo cha uhakika wa mafunzo yao.

Ibn Taimiyya ni mmoja kati ya wanachuoni wa madhehebu ya Hambal katika karne ya nane. Yeye  alihukumiwa kwenda jela mjini Damascus (Syria) mwaka 728 A.H. kwa ajili ya kuonyesha itikadi na maoni yanayotofautiana na rai ya Waislamu wote”.
WAISLAMU TUMTII NANI PAMOJA NA ALLAH?
Mwenyezi Mungu anasema: "Mtiini Mwenyezi Mungu na mtiini Mtume na Ulul'amri katika nyinyi" (4:59). Katika Aya hii kuna mambo matatu muhimu: a. Kumtii Mwenyezi Mungu (b) Kumtii Mtume (c) Kuwatii Ulul'amri.
Kumtii Mwenyezi Mungu, maana yake ni kushika amri zake na kuacha makatazo yake. Kama ambavyo; kumtii Mtume (s.a.w.) maana yake ni kufuata uongozi wake.
Katika Aya hii mwenyezi Mungu anaamrisha wa atiiwe Ulul'amri na yeyote ambaye Mwenyezi Mungu anaamrisha atiiwe lazima awe maasum (Mwenye kuhifadhiwa na makosa). Basi, lazima Ulul'amri waliotajwa katika Aya hii wawe Maasum. Naam; kidogo tujikumbushe lile tukio Ia "KISAA" Mwenyezi Mungu aliposema: "Hakika Mwenyezi Mungu anataka kukuondoleeni uchafu watu wa nyumba (ya Mtume) na (anataka) kukutakaseni sana sana." (33:33)
Hapa tutaangalia Nukta mbili katika Aya hii: (a) AR'RIJSU = Uchafu, matendo mabaya, Haramu, Laana, Kufru, Adhabu. Tazama: Al-Muujamal wasit (kamusi) Kwa mantik hii utaona kuwa: Ahlul Bait, Mwenyezi Mungu amewaondolea uchafu na matendo mabaya. Amewaepusha haramu, hawana laana, wanarehema, amewaondolea kufru na adhabu.
(b). At'tuhru: Kutokuwa na uchafu wa aina yoyote. Taz: Al-muujamal wasit (Kamusi) Kwa hiyo; Ahlul Bait (a.s.) hawana uchafu wa aina yo yote. Natija inaonyesha kuwa: Ahlul Bait ni Watakatifu na ni Maasum.
Hawa wanaotiiwa hapa ni Ahlulbayt wa Mtume (saww) ambao Mtume aliwatangaza kuwa ni viongozi baada yake, nao ni Imam Ally (a.s) ambaye ni khalifa wa kwanza, Imam Hassan yaani khalifa wa pili, Imam Hussein yaani Khalifa wa tatu,... na khalifa wa 12 ni Imam Muhammad Mahdi (a.s). hawa ndio urul-amri waliowataja Mwenyezi Mungu katika aya hapo juu kwa tafsiri sahihi itokanayo na Mtume mwenyewe.
Sio kila kiongozi mwislamu anaingia katika kauli hii kwa sababu ziko aya nyingine ambazo Allah ametukataza kuwatii viongozi madhalimu, waovu na watenda dhambi.

MATENDO MATUKUFU KWA MUISLAMU {I}

MATENDO MATUKUFU KWA MUISLAMU {I}

{1}Kuwa na tabia nzuri:-
Mtukufu Mtume {s.a.w.w.} amesema:- "Hakika aliye kamilika imani miongoni mwa walioamini ni yule mwenye tabia nzuri".
{2}Kuwa na elimu:
Mwenyezi Mungu amesema:- "Kwa hakika wanaomwogopa Mwenyezi Mungu miongoni mwa waja wake ni wale wataalamu {wanavyuoni}".   {Quran Sura ya 35 aya ya 28}.
Mtukufu Mtume {s.a.w.w} amesema:- "Mwenye kutafuta elimu {mwanafunzi} hupendwa na Mwenyezi Mungu, hupendwa na Malaika, hupendwa na Mitume, na wala hatapenda elimu {ya dini} isipokuwa yule mtu ambae ni mwema."
{3}Ushujaa:
MtukufuMtume {s.a.w.w.} amesema:-"Haimfai mwenye imani awe bahili wala mwoga'". Mwenyezi Mungu anawasifu wenye imani katika Qur'an hivi:

''Muhammad ni Mtume wa Mwenyezi Mungu na walio pamoja naye ni wenye nyoyo thabiti {mashujaa} mbele ya makafiri". {Qur'an Sura ya 48, aya ya 29}.

Wednesday 23 September 2015

KUUMBWA KWA MWANADAMU

KUUMBWA KWA MWANADAMU
 Hatua ya awali ya uumbaji, pale ambapo Adam aliumbwa tunamwachia Allah.
Lakini kwa sasa hatua ya kwanza katika kuumbwa kwa Mwanadamu hurejea kwenye hali wakati Kijusu (Mimba) kinapowekwa kimpango katika tumbo la uzazi, ingawa imefungwa ndani ya aina tatu za sitiri zilizo wazi na aina tatu za viza. Ya kwanza ikiwa ni ile ya ukuta wa nje, ya pili ni ya tumbo la uzazi na ya tatu ni ya Kondo la nyuma. Huu ni wakati ambapo kijusu hakiwezi kujilisha wala kuondoa madhara yoyote yatokanayo nayo.

Mtiririko wa Hedhi umeadilishwa ili kutoa lishe kwa ajili yake, kama vile maji yanavyochukua lishe kupeleka kwenye mimea. Hivyo mpango huu huendelea mpaka kufikia wakati ambao viungo vyake vimekamilishwa, ngozi juu ya mwili wake huwa imara kiasi chakustahimili hali ya hewa - hivyo kwamba haiwezi kupata madhara yoyote kutoka kwenye hewa na macho yake yanapata uwezo wa kustahimili mwanga.
Wakati vyote hivi vinapokuwa vimekwisha fanyika, mama yake hupata uchungu wa uzazi, ambao kwa ukali humtikisa kumfikisha kwenye kuhangaika, kufikia upeo wa kuzaliwa mtoto.
Na kwa kuzaliwa mtoto, mtiririko wa heidhi uliokuwa ukipeleka lishe kwenye tumbo la uzazi unabadilishwa kwenda kwenye matiti ya mama.
Ladha yake inabadilishwa hivyo hivyo na rangi yake, na kuwa lishe aina ya pekee tofauti ambayo hufaa hasa kwa hali ya mtoto, kama na wakati ahitajiayo (hayo) hayo, kulinganishwa na mtiririko wa damu.

Wakati ule ule wa kuzaliwa kwake anaanza kutikisa na kulamba midomo yake kwa ulimi wake kuonyesha hamu yake ya (kunyonya) maziwa hukuta jozi ya matiti ya mama yake matamu mno yaliyohifadhiwa yakining'inia tayari kwa kumpatia lishe kwa ajili yake. Hupata lishe yake kutoka maziwa katika njia hii mpaka wakati huo, kwa vile mwili wake bado ni mororo, viungo vyake na matumbo yake ni laini na dhaifu.

Bila shaka Mwenyezi Mungu aliyeandaa utaratibu huu wa uumbaji anastahili kushukuriwa na kuabudiwa. 

BAHLUL NA WAZIRI WA KHALIFA HARUN RASHID

BAHLUL NA WAZIRI WA KHALIFA HARUN RASHID
Siku moja Waziri mmoja wa Harun alimwambia Bahlul, "Ewe Bahlul, Khalifa amefanya wewe uwe mtawala na Hakimu wa ufalme wa mbwa, kuku na nguruwe wote."

Bahlul alimjibu: "Basi kuanzia hivi sasa, wewe hauna budi kuzitii amri zangu kwani wewe pia upo miongoni mwa raia wangu."

Wote waliokuwa pamoja na Waziri walicheka mno na kulimfanya aondoke kimya kwa kuaibishwa.

FUNZO KUTOKANA NA HABARI HII.
1.  Watawala waache kuwanyanyasa na kuwakejeli wananchi walio chini yao, vinginevyo wananchi watakuwa na haki ya kujitetea na kuwafedhehesha watawala hao.

2.  Kila mtu anahaki zake, na anatakiwa alinde haki zake kwa kila hali. Hakuna sababu ya msingi ya kumfanya mwananchi awe mwoga katika nchi yake mwenyewe. 

Saturday 19 September 2015

MAPINDUZI YA KIISLAMU NA HUJUMA ZA KIWAHHABI.

MAPINDUZI YA KIISLAMU NA HUJUMA ZA KIWAHHABI.
Asalaam alaykum.
Kwa hakika Mapinduzi ya Kiislam nchini Iran, yalileta mshituko mkubwa katika ghuba, na kuzisononesha tawala zote zilizoko sehemu hiyo na hasa hasa zinazohusiana na mataifa makubwa na kuyategemea kwa kila hali,na kwa upande mwingine madola hayo ya kikoloni yanazitegemea nchi hizo na miongoni mwa tawala hizi ni ule utawala wa Kiwahhabi unaotawala nchi kubwa miongoni mwa nchi za Kiislam, nchi ambayo inasifika kwa utajiri mkubwa wa asili na inanufaika kwa hali maalum ya kijiografia.

Basi ukoloni mbaya na vibaraka wake na watendaji wake wakiongozwa na walinganiaji wa Kiwahhabi wamekusudia kupinga mapinduzi ya Kiislam na kimbunga chake kwa njia mbalimbali, miongoni mwa upinzani huo ni kuzusha wasiwasi ndani yake na kuwasha mioto ya vita dhidi yake na kulazimisha vikwazo vya kiuchumi dhidi ya Mapinduzi hayo.

Na njama zote hizi za upinzani dhidi ya mapinduzi ziliposhindwa, wakakusudia kuleta picha mbaya ya utamaduni wa mapinduzi na kuondosha Maf-humu yake na kuuzushia uongo na kuupakazia uzushi ili kuwazuia watu kufuata muongozo wake na kumfuata kiongozi wa mapinduzi hayo.

Kwa hakika njama hii ya kiuadui dhidi ya utamaduni wa mapinduzi ya Kiislam, inabainika ktk mambo yafuatayo:
1) Kueneza matangazo na magazeti aina nyingi katika nchi mbalimbali za ulimwengu ili kuzungumzia dhidi ya mapinduzi na kufanya ushawishi dhidi yake na kuonyesha sura mbaya ya utamaduni wake halisi.
2)Kuchapisha vijitabu na vitabu vingi mno kuhusu utamaduni huo kwa kupitia mikono ya watu na waandishi ambao wameuza nafsi zao na hawajali isipokua mlo wao na pengine vyeo vyao vya kidunia wakiongozwa na yule muongo mkubwa Ih-Sa'an ilahi Dharir (marehemu) ambae ni miongoni mwa watu waliokua wanapata mali nyingi kutoka Saudia.
Mtu huyu alisimama kidete kwa nguvu zake zote na kwa kila kitu ambacho Saudia inakitoa ili kuleta picha mbaya ya taaluma ya mapinduzi miongoni mwa Waislam.
Na huyu bwana alikua maskini kwa kila kitu hata katika madai yake kuwa anayafahamu madh-hebu ya Shia Imamiyyah, basi anachanganya na kuvuruga na wala hapambanui baina ya Asili na na Far-i. Wala baina ya Aqida na Riwaya, na anatoa ushahidi kwa kutumia riwaya kuwa eti ndiyo madh-hebu ya Shia yalivyo.
Yapo mengi zaidi ya hayo katika uongo wake na uzushi wake na natija mbovu alizotoa.
3)Kuyaeneza Madh-hebu ya Kiwahhabi miongoni mwa vijana katika eneo hilo kwa njia mbalimbali huku wakibainisha wazi kuwa Mawahhabi ndio Waislam na kwamba wao ndio wanaompwekesha Mwenyezi Mungu na ndio wanaoitumia Qur'ani na Sunna kwa usahihi, na wasiokua wao ni makafiri!!!
Waandishi wabaya wa aina hii wamepata washabiki wengi hata hapa Afrika ya Mashariki, na washabiki hawa humkufurisha kila mtu mwenye fikra tofauti na zile za uwahhabi.
Tunamwomba Allah atuepushe na ushabiki huu wenye maradha kwa Uislamu.

Allah Mtukufu Ndiye Mjuzi Zaidi

MTUME AAGIZA KUFUATA QUR’AN NA AHLULBAYT

MTUME AAGIZA KUFUATA QUR’AN NA AHLULBAYT
Imepokewa kutoka kwa Sahaba Zaid bin Arqam: Amesema Mtume (s.a.w.):- "Mimi ninakuachieni vizito viwili ambavyo mkishikamana navyo hamtapotea baada yangu, Qur’an na AhIul Bait wangu, viwili hivi havitaachana mpaka vitakaponifikia katika Haudh."
TAZAMA:
Tafsir Ibn Kathir J.4 Uk. 122
Tafsirul Khazin J.1 Uk. 4
Tarikh Bughdad J.8 Uk. 442
Sahihi Muslim J.4 Uk. 1873
Sahihi Tirmidh J.2 Uk. 308
Jamiul Usul J.1 Uk. 187
AIbidayatu Wannihaya J.7 Uk. 362
Majmauz Zawaid J.9 Uk. 163


Hadithi hii inathibitisha kuwa baada ya kuondoka Mtume watakaoshika mahala pake ni Ahlul Bait (a.s.) ambao tumekwisha waona katika tukio Ia "KISAA" na katika tukio la "MUBAHALA"

Mwenyezi Mungu ameamrisha kufuata uongozi wao aliposema: "Shikamaneni na kamba ya Mwenyezi Mungu nyote wala msitengane". 3:103 Tamko la kamba hapa ni AHLUL BAIT" na hapa tutaonyesha maneno ya Imam Shaafy "Na nilipowaona watu Madhehebu yao yamewapeleka katika bahari yao ya upotovu na ujinga, nikapanda kwa jina Ia Mwenyezi Mungu katika meli yenye kuokoa, nao ni watu wa nyumba ya Mtume mwisho wa Mitume. Na nikaishika kamba ya Mwenyezi Mungu nayo ni kuwatawalisha (Ahlul Bait) kama tulivyoamuriwa kushikamana na kamba, watakapo farakana katika dini makundi sabini na kidogo kama ilivyokuja katika Hadithi. Na asipatikane wa kuokoka miongoni mwao isipokuwa kundi moja, niambieni ni kundi gani hilo enyi wenye akili na maarifa je! Katika makundi yatakayoangamia mojawaponi ni lile kundi la watu wa Muhammad? Au wao ni katika kundi litakalo salimika, niambieni. Ikiwa utasema kundi la Muhammad ni katika kundi litakalookoka, basi huo ni msimamo wa kweli, na ukisema kundi hilo ni katika makundi yatayoangamia bila shaka umepotosha uadilifu, basi niachie Ali awe kiongozi wangu na kizazi chake, na wewe bakia katika mapambo ya ulimwengu."

Imam Shaafy hapa anatukumbusha tamko muhimu Ia Mtukufu Mtume (s.a.w.) aliposema: "Mfano wa Ahlul Bait wangu ni kama mfano wa Meli ya Nuhu, atakayepanda humo ataokoka, na atakayebaki nje atazama".

TAZAMA:
Manaqib Ali Uk. 132
Mustadrakus Sahihain J.2 Uk. 343
Majmauz Zawaid J.9 Uk. 168
Kanzul Ummal J.6 Uk. 216

Hilyatul Awliyaa J.4 Uk. 306 

WAUMINI WATATU WA KWANZA KATIKA UISLAMU

WAUMINI WATATU WA KWANZA KATIKA UISLAMU
Katika kitabu cha Tafsir Durr-e-Manthur na katika Fathul Qadeer cha Abu Ali Muhammad Ibn Ali al-Shawkani imeandikwa hivi kwa  ushahidi wa aya ya Qurani, “Wassabiquunas Saabiquun” (Sura 56, Aya 10-12). Ibn Abi Hatim ametoa hadithi alionena Abdullah Ibn Abbas kwamba watakatifu WATATU ndio walioikubali (walioamini)  mwanzo dini ya Kiislamu, JOSHUA mtoto wa Nun alikuwa wa  kwanza kumwamini Mtume MUSA na mwenye imani alioamini mwanzo katika Al-Yaseen kuukubali utume wa Mtume Isa (Tazama  Sura 36, Aya 20-26) na wa tatu wao ni Ali mtoto wa Abu Talib  aliotangulia kukubali Utume wa Mtume wetu mtukufu.
Ibn Mardwaih katika maelezo yake kuhusu Aya hiyo hiyo ametoa  hadithi kutokana na Ibn Abbas akisema hivi kwamba aya hii  yaonyesha sifa juu ya Hizqil mwenye kuamini kati ya watu wa Firauni (Tazama Sura 40, Aya 28-33), Bwana Habib al-Najjar mwenye imani katika kabila ya Yaseen na Ali Ibn Abi Talib, kila mmoja katika wao ni wa mwanzo kuamini kati ya watu wao, na Ali ni bora wao kuliko wote.

Waumini hao watatu ndio waliowaongoza waislamu wakati mitume wao walipoondoka au kufariki. Kwa hiyo habari hii inaendelea kuthibitisha kuwa uongozi au ukhalifa baada ya Mtume ulistahili kukamatwa na Imam Ally (a.s).

HAWA NDIO WATU WALIOUPINGA UKHALIFA BANDIA WA ABUBAKAR SIDIQ (R.A

HAWA NDIO WATU WALIOUPINGA UKHALIFA BANDIA WA ABUBAKAR SIDIQ (R.A)
Ndani ya Uislamu uchaguzi sio kitu kinachopokelewa vizuri lakini baada ya Mtume kufariki, waroho wa madaraka walikutana katika ukumbi iitwao Saqifatu bani Saida na kufanya uchaguzi mbovu kuliko chaguzi zote duniani, ambapo Abubakr alichaguliwa kwa kutumia upanga wa Umar bin Khatab ambaye alitangaza katika ukumbi huo kuwa Khalifa ni Abubakar na yeyote atakayepinga atakamkata kichwa. Waislamu kwa woga walikubali utawala huo wa kibabe na ukatili mkubwa.
Lakini Masahaba majasiri walipinga, miongoni mwao wakiwa Mashia ambao walikuwa wakiitwa Mashia wa Imam Ally (a.s).
Historia inaonesha kuwa baadhi ya wapingaji hao ni Bwana mkubwa wa Kiansar Saad bin Ubbadah na mwanawe Qais bin Saad, Ali bin Abi Talib, Zubair bin Al-Awwam,[1] Abbas bin Abdil-Mutalib, Bani Hashim wengine na baadhi ya Masahaba ambao walikuwa wakiona kuwa Ukhalifa ni haki ya Ali (a.s.) na walipinga baia hiyo na wakabakia nyumbani kwa Ali mpaka wakatishiwa kuchomwa moto.[2]
REJEA
[1]-Sahih Bukhar Juz. 8 uk. 26 Babu Rajmil-Hubla Minaz-zina.
[2]--Tarikhul-Khulafai cha Ibn Qutaibah Juz. 1 uk. 18


Kwa kulinganisha hayo tunaona Mashia wanathibitisha kinyume cha usemi wa Masunni na wanasisitiza ya kwamba Mtume (s.a.w.) alimbainisha Ali kuwa ni Khalifa na akatamka hili katika matukio mengi na lililo mashuhuri ni lile la Ghadir Khum.

FUNDISHO KUTOKANA NA KIFO CHA MIRZA TAHIR QADIAN, IMAM WA JUMUIYA YA AHMADIYA.

FUNDISHO KUTOKANA NA KIFO CHA MIRZA TAHIR QADIAN, IMAM WA JUMUIYA YA AHMADIYA.

Assalaam Alaykum Warahmatullah Wabarakatuh.
Imam wa Jumuiya ya Ahmadiya, Mirza Tahir Qadiani afariki dunia. Yule aliyeitwa Imam na Khalifa wa Kujitawaza wa Jumuiya ya Ahmadiya, Mirza Tahir Ahmad Qadiani alifariki duniya mnamo Aprili 19 2003. Kila mtu lazima afe siku yake ikifika, lakini vifo vingine ni fundisho kwa wengine. Mnamo mwaka 1988 Mirza Tahir Ahmad alitoa chagizo la Mubahila (dua ya maapizano) kwa Umma mzima wa Waislamu, akiwaita makafiri na waongo. Changamoto hii ya Mubahila ikamuelemea Mirza. Ilimtia matatani na kumuweka katika hali ngumu ambayo hakuweza kujinusuru nayo kamwe na hatimaye ikamtowa uhai.


Baada ya kutoa changamoto hii, Mirza aliishi kwa kujificha lakini wanazuoni wa kiislamu wakayafanya maisha yake yawe ya moto kwa kumchagiza mara kwa mara kufanya naye dua ya maapizano. Wanazuoni wengi waliikubali changamoto yake na wakamwita katika duwa ya ana kwa ana ya maapizano (kama ilivyokuwa Sunna ya Mtume Muhammad (s.a.w).

Said Abdul Hafiiz Shah aliyeanzisha harakati dhidi ya Ahmadiya mwaka 1991, naye pia aliikubali changamoto ya mubahila (dua ya maapizano) lakini Mirza Tahir hakuwa na ujasiri wa kukabiliana na yeyote katika dua ya maapizano. Kutokea kwenye jukwaa la harakati dhidi ya ahmadiya, waislamu wakamchagiza Mirza kufanya naye Mubahila katika miaka ya 1994, 1995, 1997, 1998 na 2000, lakini Mirza Tahir alipiga kimya kiasi kwamba alishindwa hata kulijibu tu chagizo hilo achililia mbali kulikubali.

Sheikh Manzoor Ahmed Chinioti amekuwa akienda London kila mwaka tangia mwaka 1989 na amekuwa akimchagiza Mirza kujiapiza kwamba yeye (Mirza Tahir) hakuwahi kufanya mambo ya kishoga (ubaradhuli). Ni muhimu kukumbuka kuwa baba yake Mirza Tahir, Mirza Bashiruddin Mahmud, Khalifa wa pili, alikuwa mzinzi, Muhuni, baradhuli wa kutupwa ambaye hakuacha kumpitia hata binti yake wa kuzaa na hakuwaacha hata ndugu zake ambao kwa sheria ya dini ya ufunuo, ni haramu hata kuwaoa.
Lakini wapi? Mirza Tahir amebakia kujificha nyumbani kwake Gressenhall. Mfuwasi wa zamani wa Ahmadiyya, Ahtesham-ul-Haq Abdul Bari, anayejishughulisha na harakati dhidi ya Ahmadiyya/Kadiyani mjini Mumbay, naye pia ametoa changamoto za mara kwa mara za Mubahila ambapo mwaka 1995 alikwenda hadi kwenye makao makuu ya Ahmadiyya mjini London kwaajili ya kufanya maapizano ya ana kwa ana na Mirza Tahir ambaye alikataa kumpa nafasi hiyo.
Lakini hatimaye Mirza Tahir alifanya kosa baya sana la kukubali changamoto ya duwa ya maapizano (japo si ya ana kwa ana).

Mnamo Juni 3 1999 duwa ya maapizano iliafikiwa baina ya bwana Illias Suttar wa Karachi na Murabi wa Qadiyani wa Karachi bwana Mohammed Othman Shahiid. Msingi wa maapizano haya ulikuwa ni ile changamoto ya mubahila aliyeitowa Mirza Tahir mwaka 1988. Mashahidi watatu kutoka kila upande walishuhudiya tukio hili la kihistoriya. Mnamo Julai 30 1999, mbele ya wajumbe 18.500 wa Kadiyani waliotoka sehemu mbali mbali ulimwenguni ambao walijumuika kwa ajili ya mkutano wa mwaka (Jarsa Salana) mjini London, Mirza Tahir alitamka hadharani kuikubali changamoto hii ya Illias Suttar na kusema: "Mungu atamuadhibu mtu muongo ndani ya kipindi cha mwaka mmoja.

Hata kabla ya mwangwi wa maneno yake haujamalizika, kweli muongo akatiwa mkononi na Mungu. Mnamo Agosti 20 1999 wakati Mirza Tahir alipokuwa akitowa Hotuba ya Ijumaa nchini Norway, ghafla alipigwa na kiarusi kilichomfanya aseme maneno yasiyoeleweka. (Ambacho kilisababisha hotuba yake ivurugike na kutoeleweka).
Haraka haraka akakimbiziwa London ambako alikaa ndani kwa takriban mwezi mzima. Mnamo Septemba 10,1999 alitoa hotuba ya dakika kumi ambapo alikiri kuwa alipatwa na ugonjwa wa akili ambao ulimfanya ashindwe kujielezea na hiyo ndiyo sababu iliyomfanya asionekane hadharani. Siku hiyo hakuweza kuongoza sala na badala yake Imamu akawa Ataul Mujiib Rashid. Kwa kipindi fulani baada ya hapo alikuwa akionekana kufanya makosa ya mara kwa mara katika hotuba na sala, wakati mwingine akimaliza sala baada ya rakaa moja tu.
Adhabu hii ya Mungu ilidhihirisha mbele ya macho ya walimwengu kuwa Mirza Tahir pamoja na Mirza Gulam Ahmadi Kadiyani walikuwa waongo.

Illias Suttar bado yu hai na bukheri wa afya hadi leo. Jumuiya ya Ahmadiyya imepiga kimya cha jumla juu ya swala hili la Mubahila ya Illias Suttar. Ndani na nje ya jumuiya hiyo, mara kwa mara watu wamekuwa wakiuliza: " Ni nani mshindi wa Mubahila? " Lakini Mirza Tahir naye amenyamaza kimya juu ya swala hili na hakutowa tamko lolote rasmi hadi mwisho wa uhai wake.

kutokana na tukio hili tunajifunza kwamba tusing’ang’anie imani zetu hata kama ni potofu bali tuwe tayari kubadilika pale ukweli unapotudhihirikia. 

Thursday 17 September 2015

MATENDO YALIYO FARADHI KWA MUISLAMU

MATENDO YALIYO FARADHI KWA MUISLAMU

{1} Kufanya amali njema kwa moyo wa bidii na unyoofu:
Mtukufu Mtume amesema: 'Kwa hakika amali zote zinategemea nia zake."

{2}Kumtegemea Mwenyezi Mungu:
Mwenyezi Mungu amesema:- "Na anayemtegemea Mwenyezi Mungu yeye humtoshea"........... {Qur'an 65:3.
"Na tegemeeni kwa Mwenyezi Mungu ikiwa nyinyi ni wenye kuamini", {Qur'an 5:23}.

{3} Kutendeana Haki: {Kuto kudhulumiana}
Mtukufu Mtume {s.a.w.w.} amesema:- "Haikamiliki imani ya kiumbe hadi awe na sifa tatu, kutoa msaada wakati wa dhiki, usawa na unyoofu kati yake na mwenziwe, mwingi wa kutoa salamu."
{4} Kuwatendea mema wazee wawili:
Mwenyezi Mungu amesema: "Na Mola wako amehukumu kuwa msimwabudu yeyote ila yeye tu, na kuwafanyia wema wazazi wawili. Kama mmoja wao akifikia uzee mbele yako au wote wawili, basi usiwaambie hata Ah; Wala usiwakemee. na useme nao kwa msemo wa heshima kabisa. Na uwainamishie bawa la unyenyekevu kwa huruma, na useme 'Mola wangu! Warehemu {Wazee wangu} kwani walinilea katika utoto".

(5} Kuwaangalia jamaa wa damu:
Mwenyezi Mungu amesema: "Mcheni Mwenyezi mungu ambaye kwaye mnaomba na {kuangalia} jamaa wa damu, hakika Mwenyezi Mungu ni mlinzi juu yenu". {Qur'an 4:2}.

[6) Kusaidiana mambo mema:
Mwenyezi Mungu katika Qur'an amesema: "Saidianeni katika wema na kumcha Mwenyezi Mungu, wala msisaidiane katika dhambi na maasi." {5:2}.
(7}Kupatanisha watu:
Mwenyezi Mimgu amesema: "Basi mwogopeni Mwenyezi Mungu na suluhisheni mambo baina yenu, na mtiini Mwenyezi Mungu na Mtume wake ikiwa nyinyi ni katika wanao amini {kweli}".{Qur’an 8:1}.
"Kwa hakika Waislamu wote ni ndugu, basi patanisheni baina ya ndugu zenu. Na mcheni Mwenyezi Mungu, {msipuuze jambo la kupatanisha} ili mrehemiwe" {Quran 49:10}.

{8}Ukweli:

Mwenyezi Mungu amesema:- "Kwa yakini Mwenyezi Mungu atawatambulisha wale walio wa kweli na walio waongo." {29:3}.   "Mwenyezi Mungu ametuamrisha tuwe wakweli" {Qur'an 9:119}.

IDADI NA WAKATI WA SALA ZA FARADHI

IDADI NA WAKATI WA  SALA ZA FARADHI
Ujue kuwa sala za Wajibu za siku zote ni tano:-
{a} Sala ya Asubuhi ni Rakaa mbili.
Na nyakati zake ni Alfajir kabla ya kuchomoza jua.

{b} Sala ya Adhuhuri ni Rakaa nne: na {c} Sala ya Alasiri ni Rakaa nne.
Na nyakati zake sala hizi mbili ni dhuhuri hadi kuchwa jua.

 {d} Sala ya Magharibi, nayo ni Rakaa tatu, na {e} Sala ya Isha nayo ni Rakaa nne.
Na nyakati zake sala hizi mbili ni magharibi hadi nusu ya usiku.


Hii ni kwa mwenye kuwa mkazi wa mji au kama mkazi wa mjini. Lakini msafiri husali sala za rakaa nne {Adhuhuri, alasiri na Isha} kwa rakaa mbili mbili kama sala ya Asubuhi.

AHLULBAYT WAMETAKASWA – HAWAFANYI DHAMBI

AHLULBAYT WAMETAKASWA – HAWAFANYI DHAMBI
Ninataka kuongelea tukio la "KlSAA" Iliposhuka Ayatut Tat'hir:- Hakika Mwenyezi Mungu anataka kukuondoleeni uchafu watu wa nyumba (ya Mtume) na (anataka) kukutakaseni sana sana" 33:33.

Iliposhuka Aya hii Mtume alimchukua Ali na Fatima na Hasan na Husein, akawafunika nguo kisha akasema: "Ee Mola! Hawa ni watu wa nyumba yangu, basi waondolee uchafu na uwatakase sana sana." Mama Ummu Salma (mke wa Mtume) alipotaka kuingia humo, Mtume (s.a.w.) akamzuia:
Kama ambavyo kwenye tukio la Mubahala ulipofika wakati wa kuomba maombi maalum kwa ajili ya maapizano kati yake na Wakristo wa Najrani, Mtume alimchukua Ali na Fatima na Hasan na Husein tu. Ingawa wakati huo Mtume (s.a.w.) alikuwa nao wakeze, na Masahaba ambao ni marafiki zake pia, lakini hapa hawakuingia.
Wake za Mtume na Masahaba hawakuingia katika "KISAA" na hawakusimama katika uwanja wa Mubahala, kwa sababu Mwenyezi Mungu aliwahusisha darja hii Ahlul Bait tu peke yao.

TAZAMA:
Tafsirul Khazin Juzu ya 3 Ukurasa wa 259
Tafsirul Ibn Kathir Juzu ya 3 Ukurasa wa 494
Tafsirul Qurtubi Juzu ya 14 Ukurasa wa 183
Zadul Masir Juzu ya 6 Ukurasa wa 381

JINSI USHIA (UISLAMU SAHIHI) ULIVYOIMARIKA IRAN

JINSI USHIA (UISLAMU SAHIHI) ULIVYOIMARIKA IRAN
Katika mwaka wa 694 A.H. Falme ya Iran ilikuwa ikitawaliwa na Ghazan Khan Mughal (ambaye jina lake la Kiislamu lilikuwa Mahmud). Tokea wakati huo, Imani juu ya Ahlul Bait wa Mtume (s.aw.w.) iliendelea kukua miongoni mwa wairan, kiasi kwamba Ushia ulikua kwa uimara kabisa.
Baada ya kifo cha Ghazan Khan Muqhal mnamo mwaka wa 707 A.H., ndugu yake, Muhammad Shah Khuda Bandeh akawa mtawala wa Iran. Aliandaa mjadala wa kidini (Mdahalo) kati ya Alama Hilli, Mwanachuo msomi wa Kishia, na Khwaja Nidhamud-Din Abdul’l-Maliki Maraghe’i, Kadhi Mkuu wa (Madhehebu) Shafii na Mwanachuo mkubwa wa Kisunni wa wakati huo.
Midahalo Kati Ya Allama Hilli Na Kadhi Mkuu Kuhusu Uimamu.
Nukta ya mdahalo huu ilikuwa ni Uimamu. Allama Hilli alitoa hoja zenye nguvu sana kuthibitisha kwamba Ali alikuwa ndiye mrithi alitemfuatia mara moja Mtume (s.a.w.w.) bila mwanya, na kwa kuridhisha kabisa akabainisha uwongo wa madai ya ule upande mwingine, kiasi kwamba wale wote waliohudhuria walitosheka kabisa na jinsi ya ukweli wa Allama.
Khwaja Nidhamu’d-Din alikubali kwamba hoja za Allama haziwezi kukanushwa. Lakini akasema kwamba, kwa vile alikuwa akifuata njia za wakubwa wake waliomtangulia, haikuwa vizuri kuiacha. Aliona kwamba ilikuwa ni muhimu kudumisha mshikamano miongoni mwa Waislamu.
Mfalme Wa Irani Aliikubali Iman Ya Kishi’a.
Mfalme alisikiliza hoja hizo kwa usikivu makini, mwenyewe akaukubali msimamo wa Shi’a, na akatangaza uhalali wa Ushia katika Iran. Hatimaye alitangaza kwa magavana wa mikoa kwamba Khutuba za kila Ijumaa (zinazotolewa misikitini) zinapaswa zitangaze haki ya Ali kama mrithi wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.).
Vile vile aliamuru kwamba Kalimah iandikwe kwenye dinari (Sarafu za dhahabu) katika njia hii: “La ilaha illa llah Muhammad Rasulullah, Aliyan Waliyyullah,” maana yake, “Hakuna Mungu ila Allah; Muhammad ni Mtume wa Allah na Ali ni Walii wa Allah.” (makamu au mlezi wa watu aliyeteuliwa kiungu). Katika njia hii mizizi ya Ushi’a ilisimama kwa umadhubuti kabisa.
Karne saba baadaye, wakati wafalme wa Ki-Safavid walipoingia madarakani, utando wa ujinga na ushabiki usio na maana katika dini viliendelea kuondolewa, Ushi’a ukashamiri kila mahali katika nchi ya Iran.

Japokuwa, wako Mazoroasti katika Iran na dini nyingine kama Bahai. Lakini haipasi kuwahusisha na watu wa kawaida wa Iran, ambao wana imani katika Allah na Mtume Muhammad kama Mtume wa mwisho. Hawa wanamfuata Ali na watoto wake kumi na moja kama ilivyoamrishwa na Mtume (s.a.w.w.).