Sunday 27 September 2015

KIINI CHA MACHAFUKO KATIKA UISLAMU

KIINI CHA MACHAFUKO KATIKA UISLAMU
Mpaka katikati ya karne ya kumi na saba (17) Uislamu ulikuwa na nguvu kubwa za kisiasa duniani. Nguvu hii ilitokana na mwenendo wa Serikali ya Wauthman (Dola ya Wauthmani) ambayo ilikuwa imetawala eneo kubwa la Afrika Kaskazini, Bara Arab, nchi za Ulaya Mashariki kama vile Bulgaria, Hungaria, Yugoslavia, Romania, na hata sehemu za Urusi n.k.
Lakini watawala wa mataifa ya Kikristo, hususan wa Ulaya Magharibi, walipoona Uislamu unazidi kuenea na kupanda mbegu safi ya utamaduni wake, wakaona vibaya kwa kuwa mwenendo wa Kiislamu una nguvu  kubwa na ni vigumu kuwafanya watu kubadilika baada ya kuingiwa na silika ya Kiislamu. Kwa haraka  kabisa wakaunda vikundi vya wataalamu mbali mbali vikiongozwa na Serikali zao kuzunguka katika mataifa ya Kiislamu kwa nia ya kutafiti njia itakayowasaidia kuondoa mshikamano wa Waislamu.
Maadui walifanya  uchunguzi kwa uyakinifu na wakabainikiwa kuwa nguvu za Waislamu hutokana na umoja wao ambao kwa hakika ndio msingi wa mafanikio ya kila tabaka. Pili, ni kuwa waliona wazi kuwa Waislamu ni wenye kujenga tabia ya kuaminiana wao kwa wao, kwa hali hiyo isingekuwa rahisi kuwaingia na kuwasaliti.
Hatua ya kwanza ikawa kupenyeza baadhi ya watu wao ndani ya Waislamu na kujifanya Waislamu kusudi wapate imani ya Waislamu.
Hatua iliyofuatia ilikuwa ni wao kuingia katika vyeo vya Kiislamu na kujifunza elimu humo. Inaripotiwa kuwa Napoleon alifika Misri na  kujifunza katika kitivo cha Sheria cha Chuo Kikuu cha Al-Azhar.
Vikundi vingine vilijihusisha na kutafiti  njia za kuingia ukoloni katika maeneo ya Kiislamu na kuziangusha Serikali zake. Waitaliano waliingia  Libya na kuanzisha utawala wao huko. Waingereza waliuangusha utawala wa Tippu Sultan mwaka 1799 na kuondolea mbali matumaini ya kisiasa ya  Waislamu katika Bara Hindi. Kuanzia hapo Ubeberu wa Kiingereza ulitashahari katika eneo hilo. Katika miaka ya 1894 Waingereza walifanikiwa kuwapata  vibaraka ambao walijitolea kuutumikia utawala wao dhidi ya Uislamu. Ghulam Ahmad wa Kadian  akaunyenyekea Ukafiri wa Kiingereza kufikia hadi ya kusema baada ya kumwamini Mwenyezi Mungu  imani ya pili ni kumwamini Malkia.
Uturuki nako Serikali iliangushwa. Hii ilikuwa baada ya vibaraka kuingia katika ngazi za juu katika Serikali. Adhana ilipigwa marufuku baada ya mapinduzi. Katika utaratibu huu maadui wa Uislamu waliweza  kufanikiwa kuuvunja umoja wa Waislamu kwa  kuwatumia wanachuoni na watu maarufu katika  wenye tamaa. Na huo basi ulikuwa mwanzo wa machafuko. Mpaka hivi sasa, na katika kila nchi zenye Waislamu na ambazo zinatawaliwa na watu wenye nia mbaya na Uislamu, wanawatumia Waislamu wenye mawazo ya kitumwa.

Miongoni mwa watu waliotumiwa kuvunja nguvu za waislamu kwa kuanzisha vita vya wenyewe kwa wenyewe katika kila kona ya bara Arabu alikuwa Muhammad Abdulwahhabi akishirikiana na mfalme wa Najdi, kazi ambayo wafuasi wake wanaendelea nayo mpaka sasa. Kila eneo lenye Mawahhabi amani imetoweka, anzia Urusi, Pakistan, Afghanistan, India, China, Iran, Iraq, Yemen, Kuwait, Saudi Arabia, Syria, Misri, Libya, Tunisia, Somalia, Lebanon, Jordan, Morocco n.k. kote kuna matukio yametokea ya kuwalipua na kuwashambulia watu wasiokuwa na hatia kwa madai tu ya kutetea madhahebu yao au kupambana na makafiri, cha ajabu utakuta wanaoitwa makafiri ni waislamu wenzao wa kishia na kisunni.

No comments:

Post a Comment