Saturday 19 September 2015

MAPINDUZI YA KIISLAMU NA HUJUMA ZA KIWAHHABI.

MAPINDUZI YA KIISLAMU NA HUJUMA ZA KIWAHHABI.
Asalaam alaykum.
Kwa hakika Mapinduzi ya Kiislam nchini Iran, yalileta mshituko mkubwa katika ghuba, na kuzisononesha tawala zote zilizoko sehemu hiyo na hasa hasa zinazohusiana na mataifa makubwa na kuyategemea kwa kila hali,na kwa upande mwingine madola hayo ya kikoloni yanazitegemea nchi hizo na miongoni mwa tawala hizi ni ule utawala wa Kiwahhabi unaotawala nchi kubwa miongoni mwa nchi za Kiislam, nchi ambayo inasifika kwa utajiri mkubwa wa asili na inanufaika kwa hali maalum ya kijiografia.

Basi ukoloni mbaya na vibaraka wake na watendaji wake wakiongozwa na walinganiaji wa Kiwahhabi wamekusudia kupinga mapinduzi ya Kiislam na kimbunga chake kwa njia mbalimbali, miongoni mwa upinzani huo ni kuzusha wasiwasi ndani yake na kuwasha mioto ya vita dhidi yake na kulazimisha vikwazo vya kiuchumi dhidi ya Mapinduzi hayo.

Na njama zote hizi za upinzani dhidi ya mapinduzi ziliposhindwa, wakakusudia kuleta picha mbaya ya utamaduni wa mapinduzi na kuondosha Maf-humu yake na kuuzushia uongo na kuupakazia uzushi ili kuwazuia watu kufuata muongozo wake na kumfuata kiongozi wa mapinduzi hayo.

Kwa hakika njama hii ya kiuadui dhidi ya utamaduni wa mapinduzi ya Kiislam, inabainika ktk mambo yafuatayo:
1) Kueneza matangazo na magazeti aina nyingi katika nchi mbalimbali za ulimwengu ili kuzungumzia dhidi ya mapinduzi na kufanya ushawishi dhidi yake na kuonyesha sura mbaya ya utamaduni wake halisi.
2)Kuchapisha vijitabu na vitabu vingi mno kuhusu utamaduni huo kwa kupitia mikono ya watu na waandishi ambao wameuza nafsi zao na hawajali isipokua mlo wao na pengine vyeo vyao vya kidunia wakiongozwa na yule muongo mkubwa Ih-Sa'an ilahi Dharir (marehemu) ambae ni miongoni mwa watu waliokua wanapata mali nyingi kutoka Saudia.
Mtu huyu alisimama kidete kwa nguvu zake zote na kwa kila kitu ambacho Saudia inakitoa ili kuleta picha mbaya ya taaluma ya mapinduzi miongoni mwa Waislam.
Na huyu bwana alikua maskini kwa kila kitu hata katika madai yake kuwa anayafahamu madh-hebu ya Shia Imamiyyah, basi anachanganya na kuvuruga na wala hapambanui baina ya Asili na na Far-i. Wala baina ya Aqida na Riwaya, na anatoa ushahidi kwa kutumia riwaya kuwa eti ndiyo madh-hebu ya Shia yalivyo.
Yapo mengi zaidi ya hayo katika uongo wake na uzushi wake na natija mbovu alizotoa.
3)Kuyaeneza Madh-hebu ya Kiwahhabi miongoni mwa vijana katika eneo hilo kwa njia mbalimbali huku wakibainisha wazi kuwa Mawahhabi ndio Waislam na kwamba wao ndio wanaompwekesha Mwenyezi Mungu na ndio wanaoitumia Qur'ani na Sunna kwa usahihi, na wasiokua wao ni makafiri!!!
Waandishi wabaya wa aina hii wamepata washabiki wengi hata hapa Afrika ya Mashariki, na washabiki hawa humkufurisha kila mtu mwenye fikra tofauti na zile za uwahhabi.
Tunamwomba Allah atuepushe na ushabiki huu wenye maradha kwa Uislamu.

Allah Mtukufu Ndiye Mjuzi Zaidi

No comments:

Post a Comment