Saturday 19 September 2015

HAWA NDIO WATU WALIOUPINGA UKHALIFA BANDIA WA ABUBAKAR SIDIQ (R.A

HAWA NDIO WATU WALIOUPINGA UKHALIFA BANDIA WA ABUBAKAR SIDIQ (R.A)
Ndani ya Uislamu uchaguzi sio kitu kinachopokelewa vizuri lakini baada ya Mtume kufariki, waroho wa madaraka walikutana katika ukumbi iitwao Saqifatu bani Saida na kufanya uchaguzi mbovu kuliko chaguzi zote duniani, ambapo Abubakr alichaguliwa kwa kutumia upanga wa Umar bin Khatab ambaye alitangaza katika ukumbi huo kuwa Khalifa ni Abubakar na yeyote atakayepinga atakamkata kichwa. Waislamu kwa woga walikubali utawala huo wa kibabe na ukatili mkubwa.
Lakini Masahaba majasiri walipinga, miongoni mwao wakiwa Mashia ambao walikuwa wakiitwa Mashia wa Imam Ally (a.s).
Historia inaonesha kuwa baadhi ya wapingaji hao ni Bwana mkubwa wa Kiansar Saad bin Ubbadah na mwanawe Qais bin Saad, Ali bin Abi Talib, Zubair bin Al-Awwam,[1] Abbas bin Abdil-Mutalib, Bani Hashim wengine na baadhi ya Masahaba ambao walikuwa wakiona kuwa Ukhalifa ni haki ya Ali (a.s.) na walipinga baia hiyo na wakabakia nyumbani kwa Ali mpaka wakatishiwa kuchomwa moto.[2]
REJEA
[1]-Sahih Bukhar Juz. 8 uk. 26 Babu Rajmil-Hubla Minaz-zina.
[2]--Tarikhul-Khulafai cha Ibn Qutaibah Juz. 1 uk. 18


Kwa kulinganisha hayo tunaona Mashia wanathibitisha kinyume cha usemi wa Masunni na wanasisitiza ya kwamba Mtume (s.a.w.) alimbainisha Ali kuwa ni Khalifa na akatamka hili katika matukio mengi na lililo mashuhuri ni lile la Ghadir Khum.

No comments:

Post a Comment