Friday 25 September 2015

IMANI YA KUWEPO KWA MANABII WA MWENYEZI MUNGU

IMANI YA KUWEPO KWA MANABII WA MWENYEZI MUNGU
Inapothibitika kwamba Muumba wetu ni Mwenyeezi Mungu Mtukufu, na ni Muumba Mwenye Hekima, haiwezekani kwa viumbe wake kumuona, kumgusa, kumwenza au kuzungumza Naye, hivyo, ni lazima kwamba Manabii na Mitume Wake wawe ni miongoni mwa viumbe wake, ili kwamba waweze kuwawaidhi waja Wake yale mambo yenye manufaa kwao, na ambayo ni muhimu kwa kuwepo kwao, na ikiwa hatutawafuata, itatuongoza kwenye mauti.
Hivyo, ni lazima Mwenyeezi Mungu kwa ajuaye kuwapelekea viumbe vyake Mitume wake, ambao wanawaamrisha mema na kuwakataza maovu, nao watabaki na kuendelea kuwepo katika dunia hii kutoka Kwake. Wao ni Mitume na Manabii wake miongoni mwa viumbe wake. Wanawafundisha watu hekima, na wanajishirikisha pamoja nao katika mambo yao.
Mwenyeezi Mungu amewapa elimu, hekima, hoja na dalili, kwa mfano, wanawahuisha maiti, wanawaponyesha vilema n.k. Hivyo, dunia haiwezi kuwa tupu bila ya "Hoja"(Imamu) ya Mwenyeezi Mungu, ambaye ana elimu ni shahidi wa maneno na vitendo vya haki vya Mtume, na uadilifu wa Mwenyeezi Mungu.
Tunaamini kwamba dunia haiwezi kuwa tupu bila ya "Hoja" (Maimamu) Zake zinazotoka katika kizazi cha Mitume tu;
Vile vile Mwenyezi Mungu humchagua Mtume Wake miongoni mwa kizazi cha Mitume. Ni hivyo, kwa sababu Mwenyeezi Mungu ameweka njia imulikayo kwa wanaadamu. Ameumba kizazi tohara na kisafi, na miongoni mwao amewachagua Mitume na Manabii Wake ambao ni wateule wa Mwenyeezi Mungu na mfano bora kwa wanaadamu.

Walitoharishwa tangu kwenye manii ya wazazi wao na wakawekwa salama katika mifuko ya uzazi ya mama zao. Uchafu wa ujinga haukuwagusa, wala hawakuchanganyika nao baadaye, kwa sababu Mwenyezi Mungu amewapa daraja tukufu na adhimu kabisa.
Hivyo, yeye ambaye ni hazina ya elimu ya Mwenyeezi Mungu, mdhamini Wake wa yasioonekana, mwenye kujua siri Zake, Hoja Yake kwa viumbe Vyake, kinywa chake na ulimi Wake, lazima awe nazo sifa Zake. Kwa hivyo, Hoja (yaani Imamu) anatoka miongoni mwa vizazi vya Mitume, ili kwamba kwa kuwa nayo elimu ya Mtume aweze kuwa badala ya Mtume, na amrithi kama wasii wake, ili kwamba ikiwa watu watakataa kumkubali, aweze kuwanyamazisha.
Elimu ya Mtume wa mwenyeezi Mungu (s.w.t.) ambayo watu walikuwa nayo, ilidumu (baada ya Mtume Mtukufu) kwa muda mfupi, kwa sababu kwa haraka tofauti kati yao zikatokeza, na wakaanza kutumia maoni na fikara zao wenyewe. Kama wangelimkubali Hoja (Imamu au Khalifa) wakamtii na kumfuata, haki ingesimamiwa na Hoja, tofauti na mabishano yangeondoka, dini ingekuwa imara na salama, na imani ingeshinda shaka.
Baada ya kufariki kwa Mtume wa Mwenyeezi Mungu (s.w.t.), watu hawakuungana kumfuata Hoja huyo, wala kumtii. Kwa hakika, hakuna Mtume au Nabii wa Mwenyeezi Mungu, ambaye umati wake hawakutofautiana baada yake. Sababu ya tofauti zao miongoni mwao ni kwa ajili ya kupinga na kujitenga na Hoja, ambaye amechaguliwa baada ya Mtume wa Mwenyeezi Mungu.

No comments:

Post a Comment