Thursday 17 September 2015

IDADI NA WAKATI WA SALA ZA FARADHI

IDADI NA WAKATI WA  SALA ZA FARADHI
Ujue kuwa sala za Wajibu za siku zote ni tano:-
{a} Sala ya Asubuhi ni Rakaa mbili.
Na nyakati zake ni Alfajir kabla ya kuchomoza jua.

{b} Sala ya Adhuhuri ni Rakaa nne: na {c} Sala ya Alasiri ni Rakaa nne.
Na nyakati zake sala hizi mbili ni dhuhuri hadi kuchwa jua.

 {d} Sala ya Magharibi, nayo ni Rakaa tatu, na {e} Sala ya Isha nayo ni Rakaa nne.
Na nyakati zake sala hizi mbili ni magharibi hadi nusu ya usiku.


Hii ni kwa mwenye kuwa mkazi wa mji au kama mkazi wa mjini. Lakini msafiri husali sala za rakaa nne {Adhuhuri, alasiri na Isha} kwa rakaa mbili mbili kama sala ya Asubuhi.

No comments:

Post a Comment