Saturday 26 September 2015

SIDDIQ (WAKWELI) NI WATATU TU, KATIKA UISLAMU

SIDDIQ (WAKWELI) NI WATATU TU, KATIKA UISLAMU
Imam Muhammad ibn Ismail al-Bukhari katika kitabu chake Tarikh al-Kabeer, ametaja maneno ya Mtume wetu (s.a.w.w.) yalioelezwa na Ibn Abbas kuwa watu watatu ni “Siddiq”: hakika bila shaka Hizqil  mwamini kati ya watu wa Firauni, Habib al-Najjar mwamini kati ya ukoo wa Yaseen na Ali Ibn Abi Talib ndio wa kweli.
Nawab Siddiq Hasan Khan wa Bhopal katika kitabu chake cha tafsir  kiitwacho Tafsir Fathul Bayan ameeleza hadithi kutokana na Ibn Abi Laila, na hadithi hiyo hiyo imetolewa na Tafsir Durr-e-Manthur  ya Jalaluddin Suyuti lakini iko tafauti ya baadhi ya maneno tu,  wanasema kwamba “Ni watukufu watatu tu ambao hawakukufuru au  kumuasi Mwenyezi Mungu kabisa hata kiasi cha kupepesa macho na  walikimbilia kuamini dini ya haki. Miongoni mwao na wa mwanzo na bora wao ni Ali Ibn Abi Talib; wa pili mwamini katika kaumu ya Firauni, na watatu wao anatokana na ukoo wa Yaseen. Na watatu hawa tu ni Siddiq (Washuhudiawo na kweli).”
Wa kweli au Siddiq hapa inakusudiwa, ni watu wa mwanzo kusilimu katika kaumu yao na tena hawakuwahi kufanya dhambi, bali walipousikia Ukweli wa Uislamu waliupokea mara moja bila kusita na wakaufuata moja kwa moja bila kuchanganya na mila zao zingine.

Nakuombeni tufuate nyendo zao, nasi tuingie katika Uislamu moja kwa moja bila kuchanganya na mila zingine za ajabu ajabu.

No comments:

Post a Comment