Wednesday 23 September 2015

KUUMBWA KWA MWANADAMU

KUUMBWA KWA MWANADAMU
 Hatua ya awali ya uumbaji, pale ambapo Adam aliumbwa tunamwachia Allah.
Lakini kwa sasa hatua ya kwanza katika kuumbwa kwa Mwanadamu hurejea kwenye hali wakati Kijusu (Mimba) kinapowekwa kimpango katika tumbo la uzazi, ingawa imefungwa ndani ya aina tatu za sitiri zilizo wazi na aina tatu za viza. Ya kwanza ikiwa ni ile ya ukuta wa nje, ya pili ni ya tumbo la uzazi na ya tatu ni ya Kondo la nyuma. Huu ni wakati ambapo kijusu hakiwezi kujilisha wala kuondoa madhara yoyote yatokanayo nayo.

Mtiririko wa Hedhi umeadilishwa ili kutoa lishe kwa ajili yake, kama vile maji yanavyochukua lishe kupeleka kwenye mimea. Hivyo mpango huu huendelea mpaka kufikia wakati ambao viungo vyake vimekamilishwa, ngozi juu ya mwili wake huwa imara kiasi chakustahimili hali ya hewa - hivyo kwamba haiwezi kupata madhara yoyote kutoka kwenye hewa na macho yake yanapata uwezo wa kustahimili mwanga.
Wakati vyote hivi vinapokuwa vimekwisha fanyika, mama yake hupata uchungu wa uzazi, ambao kwa ukali humtikisa kumfikisha kwenye kuhangaika, kufikia upeo wa kuzaliwa mtoto.
Na kwa kuzaliwa mtoto, mtiririko wa heidhi uliokuwa ukipeleka lishe kwenye tumbo la uzazi unabadilishwa kwenda kwenye matiti ya mama.
Ladha yake inabadilishwa hivyo hivyo na rangi yake, na kuwa lishe aina ya pekee tofauti ambayo hufaa hasa kwa hali ya mtoto, kama na wakati ahitajiayo (hayo) hayo, kulinganishwa na mtiririko wa damu.

Wakati ule ule wa kuzaliwa kwake anaanza kutikisa na kulamba midomo yake kwa ulimi wake kuonyesha hamu yake ya (kunyonya) maziwa hukuta jozi ya matiti ya mama yake matamu mno yaliyohifadhiwa yakining'inia tayari kwa kumpatia lishe kwa ajili yake. Hupata lishe yake kutoka maziwa katika njia hii mpaka wakati huo, kwa vile mwili wake bado ni mororo, viungo vyake na matumbo yake ni laini na dhaifu.

Bila shaka Mwenyezi Mungu aliyeandaa utaratibu huu wa uumbaji anastahili kushukuriwa na kuabudiwa. 

1 comment:

  1. Jazaka Llah..kheyr.
    ni yeye tu الله wa kushukuriwa.
    ~maelezo hayo ni kutuinesha UWEZO wake kwamba yeye ni Muumbaji.....kwa hivyo tufaham kwamba hana wala hataki msaidizi ktk Uungu wake.
    kujuwa hivo tujijuwe kwamba ss ni watumwa wake tu

    ReplyDelete