Wednesday 23 September 2015

BAHLUL NA WAZIRI WA KHALIFA HARUN RASHID

BAHLUL NA WAZIRI WA KHALIFA HARUN RASHID
Siku moja Waziri mmoja wa Harun alimwambia Bahlul, "Ewe Bahlul, Khalifa amefanya wewe uwe mtawala na Hakimu wa ufalme wa mbwa, kuku na nguruwe wote."

Bahlul alimjibu: "Basi kuanzia hivi sasa, wewe hauna budi kuzitii amri zangu kwani wewe pia upo miongoni mwa raia wangu."

Wote waliokuwa pamoja na Waziri walicheka mno na kulimfanya aondoke kimya kwa kuaibishwa.

FUNZO KUTOKANA NA HABARI HII.
1.  Watawala waache kuwanyanyasa na kuwakejeli wananchi walio chini yao, vinginevyo wananchi watakuwa na haki ya kujitetea na kuwafedhehesha watawala hao.

2.  Kila mtu anahaki zake, na anatakiwa alinde haki zake kwa kila hali. Hakuna sababu ya msingi ya kumfanya mwananchi awe mwoga katika nchi yake mwenyewe. 

No comments:

Post a Comment