Friday 25 September 2015

WAISLAMU TUMTII NANI PAMOJA NA ALLAH?
Mwenyezi Mungu anasema: "Mtiini Mwenyezi Mungu na mtiini Mtume na Ulul'amri katika nyinyi" (4:59). Katika Aya hii kuna mambo matatu muhimu: a. Kumtii Mwenyezi Mungu (b) Kumtii Mtume (c) Kuwatii Ulul'amri.
Kumtii Mwenyezi Mungu, maana yake ni kushika amri zake na kuacha makatazo yake. Kama ambavyo; kumtii Mtume (s.a.w.) maana yake ni kufuata uongozi wake.
Katika Aya hii mwenyezi Mungu anaamrisha wa atiiwe Ulul'amri na yeyote ambaye Mwenyezi Mungu anaamrisha atiiwe lazima awe maasum (Mwenye kuhifadhiwa na makosa). Basi, lazima Ulul'amri waliotajwa katika Aya hii wawe Maasum. Naam; kidogo tujikumbushe lile tukio Ia "KISAA" Mwenyezi Mungu aliposema: "Hakika Mwenyezi Mungu anataka kukuondoleeni uchafu watu wa nyumba (ya Mtume) na (anataka) kukutakaseni sana sana." (33:33)
Hapa tutaangalia Nukta mbili katika Aya hii: (a) AR'RIJSU = Uchafu, matendo mabaya, Haramu, Laana, Kufru, Adhabu. Tazama: Al-Muujamal wasit (kamusi) Kwa mantik hii utaona kuwa: Ahlul Bait, Mwenyezi Mungu amewaondolea uchafu na matendo mabaya. Amewaepusha haramu, hawana laana, wanarehema, amewaondolea kufru na adhabu.
(b). At'tuhru: Kutokuwa na uchafu wa aina yoyote. Taz: Al-muujamal wasit (Kamusi) Kwa hiyo; Ahlul Bait (a.s.) hawana uchafu wa aina yo yote. Natija inaonyesha kuwa: Ahlul Bait ni Watakatifu na ni Maasum.
Hawa wanaotiiwa hapa ni Ahlulbayt wa Mtume (saww) ambao Mtume aliwatangaza kuwa ni viongozi baada yake, nao ni Imam Ally (a.s) ambaye ni khalifa wa kwanza, Imam Hassan yaani khalifa wa pili, Imam Hussein yaani Khalifa wa tatu,... na khalifa wa 12 ni Imam Muhammad Mahdi (a.s). hawa ndio urul-amri waliowataja Mwenyezi Mungu katika aya hapo juu kwa tafsiri sahihi itokanayo na Mtume mwenyewe.
Sio kila kiongozi mwislamu anaingia katika kauli hii kwa sababu ziko aya nyingine ambazo Allah ametukataza kuwatii viongozi madhalimu, waovu na watenda dhambi.

No comments:

Post a Comment