Friday 25 September 2015

MATENDO MATUKUFU KWA MUISLAMU {I}

MATENDO MATUKUFU KWA MUISLAMU {I}

{1}Kuwa na tabia nzuri:-
Mtukufu Mtume {s.a.w.w.} amesema:- "Hakika aliye kamilika imani miongoni mwa walioamini ni yule mwenye tabia nzuri".
{2}Kuwa na elimu:
Mwenyezi Mungu amesema:- "Kwa hakika wanaomwogopa Mwenyezi Mungu miongoni mwa waja wake ni wale wataalamu {wanavyuoni}".   {Quran Sura ya 35 aya ya 28}.
Mtukufu Mtume {s.a.w.w} amesema:- "Mwenye kutafuta elimu {mwanafunzi} hupendwa na Mwenyezi Mungu, hupendwa na Malaika, hupendwa na Mitume, na wala hatapenda elimu {ya dini} isipokuwa yule mtu ambae ni mwema."
{3}Ushujaa:
MtukufuMtume {s.a.w.w.} amesema:-"Haimfai mwenye imani awe bahili wala mwoga'". Mwenyezi Mungu anawasifu wenye imani katika Qur'an hivi:

''Muhammad ni Mtume wa Mwenyezi Mungu na walio pamoja naye ni wenye nyoyo thabiti {mashujaa} mbele ya makafiri". {Qur'an Sura ya 48, aya ya 29}.

No comments:

Post a Comment