Saturday 19 September 2015

MTUME AAGIZA KUFUATA QUR’AN NA AHLULBAYT

MTUME AAGIZA KUFUATA QUR’AN NA AHLULBAYT
Imepokewa kutoka kwa Sahaba Zaid bin Arqam: Amesema Mtume (s.a.w.):- "Mimi ninakuachieni vizito viwili ambavyo mkishikamana navyo hamtapotea baada yangu, Qur’an na AhIul Bait wangu, viwili hivi havitaachana mpaka vitakaponifikia katika Haudh."
TAZAMA:
Tafsir Ibn Kathir J.4 Uk. 122
Tafsirul Khazin J.1 Uk. 4
Tarikh Bughdad J.8 Uk. 442
Sahihi Muslim J.4 Uk. 1873
Sahihi Tirmidh J.2 Uk. 308
Jamiul Usul J.1 Uk. 187
AIbidayatu Wannihaya J.7 Uk. 362
Majmauz Zawaid J.9 Uk. 163


Hadithi hii inathibitisha kuwa baada ya kuondoka Mtume watakaoshika mahala pake ni Ahlul Bait (a.s.) ambao tumekwisha waona katika tukio Ia "KISAA" na katika tukio la "MUBAHALA"

Mwenyezi Mungu ameamrisha kufuata uongozi wao aliposema: "Shikamaneni na kamba ya Mwenyezi Mungu nyote wala msitengane". 3:103 Tamko la kamba hapa ni AHLUL BAIT" na hapa tutaonyesha maneno ya Imam Shaafy "Na nilipowaona watu Madhehebu yao yamewapeleka katika bahari yao ya upotovu na ujinga, nikapanda kwa jina Ia Mwenyezi Mungu katika meli yenye kuokoa, nao ni watu wa nyumba ya Mtume mwisho wa Mitume. Na nikaishika kamba ya Mwenyezi Mungu nayo ni kuwatawalisha (Ahlul Bait) kama tulivyoamuriwa kushikamana na kamba, watakapo farakana katika dini makundi sabini na kidogo kama ilivyokuja katika Hadithi. Na asipatikane wa kuokoka miongoni mwao isipokuwa kundi moja, niambieni ni kundi gani hilo enyi wenye akili na maarifa je! Katika makundi yatakayoangamia mojawaponi ni lile kundi la watu wa Muhammad? Au wao ni katika kundi litakalo salimika, niambieni. Ikiwa utasema kundi la Muhammad ni katika kundi litakalookoka, basi huo ni msimamo wa kweli, na ukisema kundi hilo ni katika makundi yatayoangamia bila shaka umepotosha uadilifu, basi niachie Ali awe kiongozi wangu na kizazi chake, na wewe bakia katika mapambo ya ulimwengu."

Imam Shaafy hapa anatukumbusha tamko muhimu Ia Mtukufu Mtume (s.a.w.) aliposema: "Mfano wa Ahlul Bait wangu ni kama mfano wa Meli ya Nuhu, atakayepanda humo ataokoka, na atakayebaki nje atazama".

TAZAMA:
Manaqib Ali Uk. 132
Mustadrakus Sahihain J.2 Uk. 343
Majmauz Zawaid J.9 Uk. 168
Kanzul Ummal J.6 Uk. 216

Hilyatul Awliyaa J.4 Uk. 306 

1 comment:

  1. Salaam.
    ..kaka leo umegusia pema.
    Quran....aliyotuwachi..ni hii inayotumiwa na masuni? Au ni hio yenu shia Mas'haf Fatima?

    na ikiwa ahl bait yupo alikuepo hai...au una maanisha Maandishi waliyobakisha?..yaani yale aliyoyatenda Mtume wetu...

    ReplyDelete