Thursday 17 September 2015

MATENDO YALIYO FARADHI KWA MUISLAMU

MATENDO YALIYO FARADHI KWA MUISLAMU

{1} Kufanya amali njema kwa moyo wa bidii na unyoofu:
Mtukufu Mtume amesema: 'Kwa hakika amali zote zinategemea nia zake."

{2}Kumtegemea Mwenyezi Mungu:
Mwenyezi Mungu amesema:- "Na anayemtegemea Mwenyezi Mungu yeye humtoshea"........... {Qur'an 65:3.
"Na tegemeeni kwa Mwenyezi Mungu ikiwa nyinyi ni wenye kuamini", {Qur'an 5:23}.

{3} Kutendeana Haki: {Kuto kudhulumiana}
Mtukufu Mtume {s.a.w.w.} amesema:- "Haikamiliki imani ya kiumbe hadi awe na sifa tatu, kutoa msaada wakati wa dhiki, usawa na unyoofu kati yake na mwenziwe, mwingi wa kutoa salamu."
{4} Kuwatendea mema wazee wawili:
Mwenyezi Mungu amesema: "Na Mola wako amehukumu kuwa msimwabudu yeyote ila yeye tu, na kuwafanyia wema wazazi wawili. Kama mmoja wao akifikia uzee mbele yako au wote wawili, basi usiwaambie hata Ah; Wala usiwakemee. na useme nao kwa msemo wa heshima kabisa. Na uwainamishie bawa la unyenyekevu kwa huruma, na useme 'Mola wangu! Warehemu {Wazee wangu} kwani walinilea katika utoto".

(5} Kuwaangalia jamaa wa damu:
Mwenyezi Mungu amesema: "Mcheni Mwenyezi mungu ambaye kwaye mnaomba na {kuangalia} jamaa wa damu, hakika Mwenyezi Mungu ni mlinzi juu yenu". {Qur'an 4:2}.

[6) Kusaidiana mambo mema:
Mwenyezi Mungu katika Qur'an amesema: "Saidianeni katika wema na kumcha Mwenyezi Mungu, wala msisaidiane katika dhambi na maasi." {5:2}.
(7}Kupatanisha watu:
Mwenyezi Mimgu amesema: "Basi mwogopeni Mwenyezi Mungu na suluhisheni mambo baina yenu, na mtiini Mwenyezi Mungu na Mtume wake ikiwa nyinyi ni katika wanao amini {kweli}".{Qur’an 8:1}.
"Kwa hakika Waislamu wote ni ndugu, basi patanisheni baina ya ndugu zenu. Na mcheni Mwenyezi Mungu, {msipuuze jambo la kupatanisha} ili mrehemiwe" {Quran 49:10}.

{8}Ukweli:

Mwenyezi Mungu amesema:- "Kwa yakini Mwenyezi Mungu atawatambulisha wale walio wa kweli na walio waongo." {29:3}.   "Mwenyezi Mungu ametuamrisha tuwe wakweli" {Qur'an 9:119}.

No comments:

Post a Comment