Thursday 17 September 2015

JINSI USHIA (UISLAMU SAHIHI) ULIVYOIMARIKA IRAN

JINSI USHIA (UISLAMU SAHIHI) ULIVYOIMARIKA IRAN
Katika mwaka wa 694 A.H. Falme ya Iran ilikuwa ikitawaliwa na Ghazan Khan Mughal (ambaye jina lake la Kiislamu lilikuwa Mahmud). Tokea wakati huo, Imani juu ya Ahlul Bait wa Mtume (s.aw.w.) iliendelea kukua miongoni mwa wairan, kiasi kwamba Ushia ulikua kwa uimara kabisa.
Baada ya kifo cha Ghazan Khan Muqhal mnamo mwaka wa 707 A.H., ndugu yake, Muhammad Shah Khuda Bandeh akawa mtawala wa Iran. Aliandaa mjadala wa kidini (Mdahalo) kati ya Alama Hilli, Mwanachuo msomi wa Kishia, na Khwaja Nidhamud-Din Abdul’l-Maliki Maraghe’i, Kadhi Mkuu wa (Madhehebu) Shafii na Mwanachuo mkubwa wa Kisunni wa wakati huo.
Midahalo Kati Ya Allama Hilli Na Kadhi Mkuu Kuhusu Uimamu.
Nukta ya mdahalo huu ilikuwa ni Uimamu. Allama Hilli alitoa hoja zenye nguvu sana kuthibitisha kwamba Ali alikuwa ndiye mrithi alitemfuatia mara moja Mtume (s.a.w.w.) bila mwanya, na kwa kuridhisha kabisa akabainisha uwongo wa madai ya ule upande mwingine, kiasi kwamba wale wote waliohudhuria walitosheka kabisa na jinsi ya ukweli wa Allama.
Khwaja Nidhamu’d-Din alikubali kwamba hoja za Allama haziwezi kukanushwa. Lakini akasema kwamba, kwa vile alikuwa akifuata njia za wakubwa wake waliomtangulia, haikuwa vizuri kuiacha. Aliona kwamba ilikuwa ni muhimu kudumisha mshikamano miongoni mwa Waislamu.
Mfalme Wa Irani Aliikubali Iman Ya Kishi’a.
Mfalme alisikiliza hoja hizo kwa usikivu makini, mwenyewe akaukubali msimamo wa Shi’a, na akatangaza uhalali wa Ushia katika Iran. Hatimaye alitangaza kwa magavana wa mikoa kwamba Khutuba za kila Ijumaa (zinazotolewa misikitini) zinapaswa zitangaze haki ya Ali kama mrithi wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.).
Vile vile aliamuru kwamba Kalimah iandikwe kwenye dinari (Sarafu za dhahabu) katika njia hii: “La ilaha illa llah Muhammad Rasulullah, Aliyan Waliyyullah,” maana yake, “Hakuna Mungu ila Allah; Muhammad ni Mtume wa Allah na Ali ni Walii wa Allah.” (makamu au mlezi wa watu aliyeteuliwa kiungu). Katika njia hii mizizi ya Ushi’a ilisimama kwa umadhubuti kabisa.
Karne saba baadaye, wakati wafalme wa Ki-Safavid walipoingia madarakani, utando wa ujinga na ushabiki usio na maana katika dini viliendelea kuondolewa, Ushi’a ukashamiri kila mahali katika nchi ya Iran.

Japokuwa, wako Mazoroasti katika Iran na dini nyingine kama Bahai. Lakini haipasi kuwahusisha na watu wa kawaida wa Iran, ambao wana imani katika Allah na Mtume Muhammad kama Mtume wa mwisho. Hawa wanamfuata Ali na watoto wake kumi na moja kama ilivyoamrishwa na Mtume (s.a.w.w.).

No comments:

Post a Comment