Saturday 19 September 2015

WAUMINI WATATU WA KWANZA KATIKA UISLAMU

WAUMINI WATATU WA KWANZA KATIKA UISLAMU
Katika kitabu cha Tafsir Durr-e-Manthur na katika Fathul Qadeer cha Abu Ali Muhammad Ibn Ali al-Shawkani imeandikwa hivi kwa  ushahidi wa aya ya Qurani, “Wassabiquunas Saabiquun” (Sura 56, Aya 10-12). Ibn Abi Hatim ametoa hadithi alionena Abdullah Ibn Abbas kwamba watakatifu WATATU ndio walioikubali (walioamini)  mwanzo dini ya Kiislamu, JOSHUA mtoto wa Nun alikuwa wa  kwanza kumwamini Mtume MUSA na mwenye imani alioamini mwanzo katika Al-Yaseen kuukubali utume wa Mtume Isa (Tazama  Sura 36, Aya 20-26) na wa tatu wao ni Ali mtoto wa Abu Talib  aliotangulia kukubali Utume wa Mtume wetu mtukufu.
Ibn Mardwaih katika maelezo yake kuhusu Aya hiyo hiyo ametoa  hadithi kutokana na Ibn Abbas akisema hivi kwamba aya hii  yaonyesha sifa juu ya Hizqil mwenye kuamini kati ya watu wa Firauni (Tazama Sura 40, Aya 28-33), Bwana Habib al-Najjar mwenye imani katika kabila ya Yaseen na Ali Ibn Abi Talib, kila mmoja katika wao ni wa mwanzo kuamini kati ya watu wao, na Ali ni bora wao kuliko wote.

Waumini hao watatu ndio waliowaongoza waislamu wakati mitume wao walipoondoka au kufariki. Kwa hiyo habari hii inaendelea kuthibitisha kuwa uongozi au ukhalifa baada ya Mtume ulistahili kukamatwa na Imam Ally (a.s).

No comments:

Post a Comment