Saturday 26 September 2015

NAMNA NABII IBRAHIM (A.S) ALIVYOFUNDISHA KUHUSU MWENYEZI MUNGU

NAMNA NABII IBRAHIM (A.S) ALIVYOFUNDISHA KUHUSU MWENYEZI MUNGU
Namna Nabii Ibrahiim (AS) alivyoonesha kuwa, nyota, mwezi na jua si miungu. Na hizi ni hoja zetu tulimpa nabii Ibrahiimu juu ya watu wake. Usiku ulipomwingilia akaona nyota. Akasema "hii ni Mola wangu" Ilipotua akasema " Siwapendi miungu wanaopotea" Na siku ya pili alipouona mwezi akasema: "Huu ndiye Mola wangu" Ulipotua akasema "Asiponiongoa Mola wangu, bila shaka nitakuwa miongoni mwa wapotofu. Na siku ya tatu alipoliona jua, akasema Hili jua ndilo Mola wangu. Huyu ni Mola wangu mkubwa, lilipotua akasema Enyi watu wangu! Mimi simo katika hayo mnayoyashirikisha na Mwenyezi Mungu. Mimi nimeuelekeza uso wangu kwa yule aliyeumba mbingu na ardhi, hali ya kuwa nimewacha Dini ya upotevu. (6:74-83).
Namna nabii Ibrahiim (AS) alivyoonesha washirikina kuwa masanamu si miongu. "Wakasema: Je wewe umeifanya hivi miungu yetu, ee Ibrahiim? Akasema: Siyo bali amefanya huyu mkubwa wao, basi waulizeni kama wanaweza kunena! Basi wakajirudi nafsi zao na wakasema Hakika ninyi mlikuwa katika madhalimu" (26:58-64).
Namna Ibrahiimu alivyombwaga mfalme kwa hoja: "Hukumsikia yule aliyehojiana na Ibrahiim juu ya Mola wake kwa sababu Mwenyei Mungu alimpa ufalme? Ibrahiimu akasema "Mola ni yule anayehuisha na kufisha" Yeye akasema "Mimi pia nahuisha na kufisha" Ibrahiimu akasema: "Mwenyezi Mungu hulichomoesha jua mashariki, basi wewe lichomoze magharibi". Akafedheheka yule aliyekufuru na Mwenyezi Mungu hawaongozi watu madhalimu"(2:258).

Umuhimu wa kufikiri kwa kujenga hoja: Qur'an kwa nafsi yake inajieleza mara kwa mara kuwa hoja za ujumbe wake ziko wazi kwa watu wanaotumia akili, wenye kuzingatia, wenye kutafakari. "Na hakuna atakayeamini ila kwa idhini ya Mwenyezi Mungu, naye hujaalia uchafu uwaendee wale wasiotumia akili zao"(10:100).
Katika aya hizi tunajifunza kuwa Mwenyezi Mungu ni wa milele, hafi hata kwa dakika moja, haonekani kwa macho, yeye ni muweza wa kila kitu. Na kwamba vingine vinauwezo kiasi walivyowezeshwa na Mwenyezi Mungu tu. Hivyo tumwabudu Mwenyezi Mungu muumba na sio miungu ya kubuni na watu wenzetu kama wafanyavyo wakristo wanao dai kuwa Yesu ni mwana wa Mungu na ni Mungu mwenyewe.

No comments:

Post a Comment