Saturday 21 June 2014

MAZUNGUMZO KATI YA KHALIFA HARUN RASHID NA IMAM MUSSA ALKADHIM (a.s): Kuhusu Ahlulbayt wa Mtume (s.a.w)

Abu Ja’far Muhammad Bin Ali, mwenye lakabu ya Sheikh Saduq, katika karne ya nne hijiria., katika kitabu chake Uyun-e-Akbar ar-Ridha (vyanzo vikubwa vya Ridha), na Abu Mansur Bin Ali Tabarsi, katika kitabu chake Ihtijajj, anatoa maelezo kinaganaga ya mazungumzo ambayo yalifanyika kati ya Harun ar-Rashid na Imamu Musa Ja’far katika baraza la Khalifa. Khalifa alimuuliza Imamu: “Unawezaje kudai kwamba wewe ni dhuria wa Mtukufu Mtume? Mtume hana dhuria. Inakubaliwa kwamba dhuria ni kutoka upande wa kiume na sio upande wa kike. Wewe ni kizazi cha bint yake.”

Imamu akasoma Aya ya 84-85 kutoka Sura ya 6 ya Qur’ani Tukufu:
 “Na tukampa (Ibrahim) Is’haqa na Yakuub, wote tukawaongoa. Na Nuhu tulimuongoa zamani, na katika kizazi chake Daudi na Suleimani na Ayub na Yunus na Musa na Harun. Na hivi ndivyo tuwalipavyo wafanyao mema. Na Zakaria na Yahya na Isa na Ilyasa, wote walikuwa miongoni mwa watu wema.” (6:84-85)
Imamu akamuuliza Khalifa: “Ni nani aliyekuwa baba wa Isa?” Harun akajibu kwamba Isa alikuwa hana baba. Imamu akasema: “Kulikuwa hakuna yeyote aliyekuwa baba yake, na bado Allah alimjumuisha Isa katika dhuria wa mitume kupitia Mariamu. Hivyo hivyo ametujumuisha sisi katika dhuria wa Mtume kupitia kwa bibi yetu Bi Fatima.”
Aidha, Imamu Fakhur’d-Din Razi, katika kitabu chake Tafsir-e-Kabir, juzuu ya 4, uk. 124, anasema kuhusiana na aya hii kwamba, inathibitisha kwamba Hasan na Husein ni watoto wa Mtume wa Uislamu.
Kwa vile katika aya hii Mungu amemdhihirisha Isa kama kizazi cha Ibrahim, na Isa hana baba, uhusiano huu ni kutoka upande wa mama. Katika hali hiyo hiyo, Hasan na Husein ni dhuria wa kweli wa Mtume. Imamu Musa alimuuliza Harun kama anataka uthibitisho zaidi.
Khalifa akamuambia Imamu aendelee. Imamu akasoma Aya ya 61 kutoka Sura ya 3 ya Qur’ani Tukufu: “Watakao kuhoji katika haya baada ya kukufikia ilmu, waambie: Njooni tuwaite watoto wetu na watoto wenu, na wanawake wetu na wanawake wenu, na sisi na ninyi, kisha tuombe kwa unyenyekevu tutake laana ya Mwenyezi Mungu iwashukie waongo,”
Aliendelea, akisema kwamba hakuna mtu hata mmoja ambaye amewahi kudai kwamba katika tukio hilo la maapizano (Mubahila) dhidi ya Wakiristo wa Najran kwamba Mtume alimchukuwa pamoja na yeye mtu yeyote isipokuwa Ali Bin Abi Talib, Fatima, Hasan na Husein.
Kwa hiyo tukiifafanua aya hii tutaona kwamba “sisi” (anfusana) maana yake ni Ali Bin Abi Talib. “Wanawake” (nisa’ana) maana yake Fatima na “Watoto” (abna’ana) maana yake Hasan na Husein, ambao Allah amewatambulisha kama watoto wa Mtume mwenyewe. Kwa kusikia
hoja hii, Harun aliguta, “Hongera, Ewe Abu’l-Hasan.” Kwa uwazi mantiki hii huthibitisha kwamba Hasan na Husein (watoto wa Bibi Fatima) ni watoto wa Mtukufu Mtume.

Tuesday 17 June 2014

ZAIDI YA WAIRAQ MILIONI MBILI WAMEJITOLEA KUPAMBANA NA UGAIDI UNAOFANYWA NA MAWAHHABI WANAOJIITA ISIL.



Watu hao wamejitolea kutoka katika dini, madhehebu na makabila yote ya Iraq. Hii ni kinyume na uongo unaosambazwa na Mawahhabi kuwa vita vile ni kati ya Sunni na Shia. Hakika Mawahhabi ni maadui wa watu wote na wala sio shia pekee. Kwa mfano, walipouteka mji wa Mosul waliuwachinja masheikh wa Kisunni wapatao 12 na mamia ya masunni wa kawaida.

Monday 16 June 2014

IMAM MAHDI

As-salamun alaykum
Je itikadi ya uwepo wa Imam Al-Mahdi {atf} ni ya kimadhehebu tu, au ni ya kidini?
Ndugu msomaji kumekuwa na tuhuma nyingi na fikra mbalimbali kutoka kwa wale wasioyajuwa ya kidini na kuyasambaza pasi na kuwa na elimu nayo, kama zile za kuambiwa eti mashia wanaitikadi mpya ya ujio wa kiongozi wa kumi na mbili ajulikanaye kama Muhammad bin Al-hassan Al-mahady {atfs}. Lakini la kustaajabisha hapa ni kuwa, ukirejea vitabu vingi vya waisilamu na pia vikiwemo vya wasambazaji wa tuhma hizi, utakuta yapo ndani ya vitabu vyao yakitajwa kwa uwazi kabisa. Kwa hiyo dini zote zinaitakidi kuwa ni lazima kuje mtu atakaewaokoa watu kutokana na madhalimu na kuijaza ardhi uadilifu na usawa baada ya kuwa umejaa dhulma na jeuri [kama alivyosema Mtume {s.a.w}] katika zama za mwisho, ila sasa tofauti ni kuhusu mtu huyo ni nani?! Kwa upande wa Wakiristo wakasema ni Nabii Issa {as}, na kwa upande wa dini tukufu ya kiisilamu wakasema ni Mmoja kati ya watu wa nyumbani kwa Mtume {saww} ambaye ni Al-Mahdy {atfs}.
Lakini utofauti pia wa madhehebu ya kiisilamu ukawepo, kama hivi; amezaliwa au laa?! Ni Hassaniyu au Hussainiyu [yaani ni katika kizazi cha Imamu Hassan au Hussain {as}]?! Sasa ilipofikia hapa, wenzetu Ah-lusunna wal-jamaa wakasema hakuzaliwa bali atazaliwa katika zama za mwisho, naye ni katika kizazi chake Mtume {saww}. Na kwa Madh-hebu ya Ah-lulbayt{as} wao wakasema ameshaazaliwa na tena ilikuwa ni 15/Shaabani/255 H. na kuuchukuwa uimamu baada tu ya kufariki baba yake Imamu Al-skary{as} mwaka 260 H .Na kuhusu hili maulamaa wengi sana wakiah-lulsunna wameliandikia vitabu maalumu kabisa kama jedwali linavyoonyesha hapa chini:


1 Al-kan-njii Al-bayani fy Akh-baris-swahaba
2 Mulla Ally Muttaqy Al-burhan fy Alaamaat Mahady akhiru zamaan
3 Al-haafidh Suyutwy Al-urful-wardy fy Akh-bar Al-mahady
4 Ibnu Hajar Al-qaulul-mukh-taswar fy Alaamaat Al-mahadil-muntadhar
Pia kwa kumalizia Qur’an nayo ikatuelezea kuwa katika zama hizo ardhi itamilikiwa na Waja wema:“Na hakika tulikwisha andika katika Zaburi baada ya kumbukumbu, kuwa ardhi watairithi waja wangu wema”. {Al-anbiya’a: 105}. Na kuhusu Bw: Mtume {saww} akasema: “Itakuwaje kwenu nyinyi-katika zama hizo- atakaposhuka Masiihu bun Mariamu {as} na Imamu wenu akiwa naye”.!! Swahihul-bukhary [kwa sherehe ya Al-karmaany] ;juz;14 uk;88.Na nyinginezo ayah nyingi na hadithi kuhusu jambo hili adhim kabisa mbele ya uisilamu tulizoziacha kwa ufipisho wa karatasi yetu.

MAWAHHABI WAWADANGANYA MASUNNI ILI KUWAINGIZA KWENYE DINI YAO MPYA NA KUWATUMIA KATIKA FITINA ZAO.

Afrika ya Mashariki imefaidi mazingira ya amani sana kiasi cha karne mbili zilizopita. Watu wa imani na itikadi zote waliishi pamoja kwa upendo na mapenzi. Kila mmoja akishiriki kwenye shughuli za mwenzake za kijamii na za Kidini. Ukiangalia kwenye Jumuiya za Kiislamu, wote wakihudhuria kwenye Misikiti ya kila mmoja, waliungana pamoja katika Maulidi na hafla za Muharram, na kupanua ushirikiano wao katika miradi ya kila mmoja. Kama Rais Mstaafu Alhaji Ali Hassan Mwinyi alivyosema katika hotuba moja ya hadhara;"Misikiti mingi ya Waislamu wa (Madhehebu ya) Shafi'i iliyoko Zanzibar na Pemba ilijengwa na kutolewa na Shia Ithna-ashariyya"
Hatimaye Wahhabi walianza Tabligh (Mahubiri) yao hapa. Badala ya kujaribu kuwaleta mapagani au wasio waislamu kwenye boma ya Uislamu, nia yao kabisa ilikuwa na bado inakaziwa katika kuwabadilisha Mashafii wawe Mawahabi. Kwa lengo hili, hujifanya kama wao ni Masunni, na kuchanganyika pamoja na Masunni. Mawahabi hao wamepanda mbegu ya fitinana chuki kati ya Madhehebu mbali mbali za Kiislamu, na hususan kati ya Sunni na Shia. Wanazungumza dhidi ya Shia, na kusambaza vitabu na vijitabu (vya mambo ya dini) dhidi ya itikadi ya Shia ambavyo vimejaa mambo ya uwongo na uzushi. Kishawishi chao kiko wazi, kwa kuwatenganisha Masunni na Mashia, wakitumaini kupata urahisi wa kuingia katika jamii ya Sunni na Misikiti yao, ingawaje tumaini hili lingali bado kukamilishwa katika Tanzania.
Hebu tuangalie katika mzizi wa uovu wa kampeni hii. Huenda hapo nyuma katika mwaka 1979, ambapo Mapinduzi ya Ki-Islamu yalipotokea katika (nchi ya) Iran, na watawala wa Kiwahhabi wa Saudia walihadharishwa vikali mno, hata kabla ya tukio la Mapinduzi ya Kiislamu, wakati Ayatullah al-'uzma al-Khomeini (R.A.) akiwa bado Najaf (Iraq). Waziri wa mambo ya nchi za nje wa Saudi Arabia, akizungumza katika hadhara moja ya Waarabu, aliuonya ulimwengu wa Waarabu kwamba kama Khomeini ataruhusiwa kuendeleza harakati zake kutoka Iraq kama hapo nyuma, sio tu kwamba utawala wa Shaha utaangushwa, lakini, hali katika eneo lote vile vile itakuwa imetibuliwa. Hivyo wakaishinikiza Iraq kuweka vikwazo juu ya Khomeini kwa hofu ya kwamba, kama juhudi zake zitafanikiwa katika Iran, zitatingisha tawala zao wenyewe zisizo imara.
Haikushangaza kwamba mara tu Mapinduzi ya Kiislamu yalipoimarika nchini Iran, hawa Wahhabi wakaanza propoganda kali yenye chuki dhidi ya Khomeini, dhidi ya Iran na dhidi ya Ushia. Kalamu za kukodisha zikaanza mchakato kutoa vitabu, makala na vijitabu dhidi ya Shia. Shia waliitwa Makafiri, na pengine mtu angeuliza: Kama ni Makafiri, basi kwa nini wanapewa viza kwa ajili ya Hija na Umra? Wairani waliitwa Majus (Waabudu Moto) kwa nini? Kwa sababu kabla ya kuja kwa Uislamu waliabudu moto. Kwa hoja hii nasi hatuna haki ya kuwaita Wahhabi Mushrikina? Kwa sababu kabla ya kuja kwa Uislamu watu wa Najd walikuwa wakiabudu Masanamu.

Baadhi ya waajiriwa wao wa ngazi za juu walikuwa ni (marehemu) Ihsan Ilahi Zaheer wa Pakistan, na Manzoor Ahmad Nu'mani na Abul Hasan Ali Nadwi wa India. Sauti itokayo kwenye vinywa vyao ni katika watakiwayo na mabwana zao kuyasema, na jambia la uzayuni lilichovywa kwenye damu ya waislamu linatumika kama kalamu yao. Kitabu kinachoandikwa dhidi ya Shia na watumwa hawa, kwa miezi michache tu kinatarujumiwa katika lugha zote kubwa za ulimwengu wa Kiislamu; na hufanywa kipatikane kila mahali, kadhalika husambazwa bure miongoni mwa Mahujaji:

Sunday 15 June 2014

FADHILA ZA MATENDO YA MWEZI WA SHAABAN

Imekuja katika Tafsiri ya Imam Hasan Askariy (a.s) kuhusiana na matendo ya mwezi mtukufu wa Shaaban riwaya ifuatayo:
(Na kwa hakika Amirul-muuminiin (a.s) alipita kwa kaumu fulani kati ya waislaam waliojumuika mahala pamoja, ndani yake kukiwa hakuna Muhajiriina wala answari, nao wakiwa wameketi katika baadhi ya misikiti. Katika siku ya kwanza ya mwezi wa Shaaban, mara akawasikia wakizungumza kuhusiana na suala la usiku wa Qadri, na mambo mengine kati ya mambo waliyo tofautiana kwayo watu, na sauti zao zikiwa zimepaa juu, na ubishani na majadiliano kuwa makali kati yao, mara Mtume (a.s) akasimama na kutoa salam na wao kumpatia nafasi, na wakaanza kumuuliza kuhusu sababu ya kukaa kwake kati yao, nae akasema kuwambia na kuwaita:

 Enyi watu wenye kuzungumzia mambo yasiyo wahusu, -Enyi wazuaji wa bidaa, hii ni siku ya mwanzo ya mwezi mtukufu wa Shaaban, mola wetu ameuita kwa jina la Shaaban,  kutokana na kutawanyika na kudhihiri ndani yake kheri nyingi, hakika Mola wenu amefungua ndani ya mwezi huu milango ya pepo, na akakutandazieni na kukuonyesheni ndani yake majumba yake ya kifakhari na kheri zake zilizo nyingi ndani ya mwezi huu, na kwa thamani ndogo na kwa mambo mepesi, basi nunueni vitu hivyo, na Iblisi alie laaniwa akakutangazieni na kukuanikieni, kundi la shari zake na mabalaa yake, kwa hivyo nyinyi si vinginevyo bali nyinyi mnazidi kudidimia katika uovu na upotevu, na mnazidi kushikamana na matawi ya ibilisi, na mkijitenga na kujiweka mbali na matawi ya kheri, iliyo funguliwa milango yake kwa ajili yenu, Na huu ni mwezi mtukufu wa Shaaban na kheri zake zilizo nyingi:

Swala, Funga, Zaka, Kuamrisha mema na kukataza Mabaya, na kuwatendea wema wazazi wawili, na watu wa karibu, majirani na kusuluhisha kati ya watu walio gombana, na kutoa sadaka kwa mafukara na masikini, mnajilazimisha kufanya mambo yaliyo ondolewa kwenu, na mambo mliyo zuiliwa kuyazungumzia, kwani kufichua na kupembua siri za Mwenyezi Mungu, ambazo mwenye kuzipembua na kuzikashifu atakuwa ni miongoni mwa watu walio angamia, ama kwa hakika nyinyi lau kama mnge simama juu ya yale mliyo andaliwa na Mola wetu alie takasika, kwa ajili ya watiifu kati ya waja wake katika siku hii, basi msinge pata muda wa kujishughulisha na haya myafanyayo, na munge anza kufanya yale mliyo amrishwa kuyafanya, wakasema: Ewe amiril-muuminiin, ni mambo yapi aliyo yaandaa Mwenyezi Mungu katika siku hii kwa ajili ya waja wenye kumtii yeye? Amirul-muuminiin (a.s) Akasema:

Sinta kuhadithieni isipokuwa niliyo yasikia kutoka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w)- hadi akafikia kusema-kisha Mtume wa Mwenyezi Mungu akasema: Ninaapa kwa haki ya yule alie nituma kwa haki kama mtume, hakika Iblisi inapofika siku ya kwanza ya mwezi wa Shaaban, hutawanya majeshi yake katika pembe zote za ardhi na kona zake, anawambia: jitahidini kuwavutia baadhi ya waja wa Mwenyezi Mungu kwenu katika siku hii, na hakika Mwenyezi Mungu alie takasika, amewatawanya malaika katika pembe zote za ardhi na kona zake, anasema kuwambia: watieni uimara waja wangu na waongozeni, na wote watapata saada kupitia kwenu isipokuwa atakae kataa, na kupetuka na kufanya jeuri, hakika huyo atakuwa katika kikundi cha iblisi na wanajeshi wake, hakika Mwenyezi Mungu alie takasika inapofika siku ya kwanza ya mwezi wa Shaaban, huamrisha milango ya pepo ifunguliwe, na huuamrisha mti wa Tuuba uchomoze matawi yake juu ya dunia hii, kisha mnadi wa Mola wetu alie takasika huita:

 Enyi waja wa Mwenyezi Mungu, Haya hapa matawi ya mti wa Tuuba…, basi shikamaneni nayo yatakuinueni hadi peponi, na haya hapa matawi ya mti wa Zaquum basi jihadharini na matawi hayo yasikupelekeni kwenye moto wa jahiim, Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w): Ninaapa kwa haki ya yule ambae amenituma kwa haki kama Mtume, hakika mwenye kuuendea mlango wa mambo ya kheri na mema katika siku hii, hakika atakuwa ameshika tawi moja wapo katika ya matawi ya mti wa Tuuba, basi litampeleka na kumfikisha peponi, na mwenye kushikilia mlango wa shari katika siku hii, basi atakuwa ameshikilia tawi moja wapo kati ya matawi ya mti wa Zaquum, nalo litampeleka hadi Motoni, kisha Mtume ( s.a.w.w) akasema:


KILICHOTOKEA GHADIIR KHUM

Assalam Alaikum
Jee, kulitokea nini Siku ya Ghadir Khum?
Ghadir Khum ni sehemu iliyoko maili kadhaa kutoka Makka katika njia inayoelekea Madina. Wakati Mtume (s.a.w) alipopita sehemu hiyo tarehe 18 Dhul'Hijja (10 March 632) wakati anarudi kutoka Hijja yake ya mwisho, aya, "Ewe Mtume fikisha uliyoteremshiwa…." Iliteremshwa, kwa hiyo alisimama ili kutangaza kwa mahujaji ambao alifuatana nao kutoka Makka na ambao walikuwa watawanyike njia panda hapo kila mtu kuelekea sehemu yake. Kwa amri ya Mtume (s.a.w) mimbari maalum ilitengenezwa kwa kutumia matandiko ya ngamia kwa ajili yake. Baada ya Salat ya mchana Mtume .(s.a.w) alipanda mimbari na akatoa Khutuba yake ya mwisho mbele ya mkusanyiko mkubwa kabla ya kifo chake miezi mitatu baadae.

Sehemu ya kuvutia ya Khutuba yake, ni pake alipomchukuwa 'Ali (a.s) kwa mkono wake, Mtume s.a.w. aliwauliza wafuasi wake iwapo yeye ana mamlaka zaidi (awla) kwa waumini kuliko wao wenyewe. Kundi kubwa lile la watu likaitikia kwa sauti kubwa "Hivyo ndivyo ilivyo , Ewe Mtume wa Allah". Kisha akatangaza: "Yule ambaye kwamba mimi ni (mawla) mwenye kumtawalia mambo yake, huyu Ali vile vile ni (mawla) mwenye mkumtawalia mambo yake. Ewe Allah, kuwa rafiki kwa yule ambaye ni rafiki, na uwe adui kwa yule ambaye ni adui kwake."

Mara tu baada ya Mtume (s.a.w) kumaliza khutuba yake, aya ifuatayo iliteremshwa:
"………. Leo nimekukamilishieni dini yenu, na kuwakamilishieni neema yangu kwenu, na nimewaridhieni kwamba Uislamu ndiyo dini yenu." (Q:5:3). Baada ya Khutuba yake Mtume (s.a.w) alimtaka kila mtu kula kiapo cha utii kwa 'Ali (a.s) na kumpongeza. Miongoni mwa waliofanya hivyo ni Umar bin al-Khattab, ambaye alisema: "Hongera Ali Ibn Abi Talib! Leo umekuwa bwana wa waumini wote wanaume na wanawake."

Mwarabu mmoja aliposikia tukio la Ghadir Khum, alikuja kwa Mtume (s.a.w) na akasema: "Ulituamrisha tushuhudie kwamba hakuna mungu isipokuwa Allah na kwamba wewe ni Mjumbe wa Allah, tumekutii. Umetuamrisha kusali sala tano kwa siku, tukakutii.Umetuamrisha kufunga (saumu) mwezi wa Ramadhani, tumekutii. Kisha umetuamrisha kwenda kuhiji Makka tukakutii. Lakini hukutosheka na yote haya yote ukamnyanyua binamu yako kwa mkono wako na ukamuweka juu yetu kama mtawala kwa kusema 'Ali ni mawla wa yule ambaye mimi ni mawla kwake: je, amri hii yatoka kwa Allah au yatoka kwako wewe?"

Mtume (s.a.w) akasema: "Kwa jina la Allah ambaye ndiye Mola Pekee! Haya yanatoka kwa Allah, Mwenye nguvu na Mtukufu" Aliposikia jibu hili aligeuka na kuelekea aliko ngamia wake jike huku akisema: "Ewe Allah! Kama asemayo Muhammad ni sawa, basi vurumisha jiwe juu yetu kutoka angani na tupatie sisi adhabu kali na mateso." Kabla hajamfikia ngamia wake Allah alimvurumishia jiwe ambalo lilipiga juu ya kichwa chake na kupenyeza ndani ya mwili wake na kumuacha akiwa amekufa. Ni katika tukio hili kwamba Allah (swt) aliteremsha aya ifuatayo:
"Muulizaji aliuliza juu ya adhabu itakayo tokea. Kwa makafiri hapana awezaye kuizuia. Kutoka kwa Allah, Mola wa mbingu za daraja." (Qur'an 70:1-3) :


Wengi wa wanachuoni hawa hawakunukuu tu tangazo hili la Mtume (s.a.w) bali vile vile wanaliita sahihi: " al-Hakim al-Naysaburi, al-Mustaddrak 'ala al-Sahihyn (Beirut), juzuu 3, uk. 109-110, uk. 133, uk. 148, uk. 533. Ameelezea kwa uwazi kwamba hadithi hii ni sahihi kwa mujibu wa vigezo vya Bukhari na Muslim. al-Dhahabi alithibitisha hukumu yake.


" al-Tirmidhi, Sunan, (Cairo), juzuu 5, uk. 633.
" Ibn Majah, Sunan, (Cairo, 1952), juzuu 1, uk. 45.
" Ibn Hajar al-'Asqalani, Fath al-Bari bi Sharh Sahih al-Bukhari, (Beirut, 1988), juzuu 7, uk. 61.
" al-'Ayni, 'Umdat al-Qari Sharh Sahih al-Bukhari, juzuu 8, uk. 584.
" al-Suyuti, al-Durr al-Manthur, juzuu 2, uk. 259 na uk. 298.
" Fakhr al-Din al-Razi, Tafsir al-Kabir, (Beirut, 1981), juzuu 11, uk. 53.
" Ibn Kathir, Tafsir Qur'an al-Adhim, (Beirut) juzuu 2, uk. 14
" al-Wahidi, Asbab al-Nuzu, uk.l64.
" Ibn al-Athir, Usd al-Ghaba fi Ma'rifat al-Sahaba, (Cairo, 1932), juzuu 3, uk.92.
" Ibn Hajar al-'Asqalani, Tahhdib, (Hyderabad, 1325), juzuu7, uk. 339.
" Ibn Kathir, al-Bidayah wa al-Nihayah, (Cairo, 1932), juzuu7, uk. 340, juzuu 5, uk. 213.
" al-Tahawi, Mushkil al-Athar, (Hyderabad, 1915), juzuu 2 uk. 308-9.
" Nur al-Din al-Halabi al-Shafi'i, al-Sirah al-Halabiyya, juzuu3, uk. 337.
" al-Zrqani, Sharhe al-Mawahib al-Ladunniyya, juzuu 7, uk. 13 

UMUHIMU WA KUJIFUNZA AKIDA ZA MADHEHEBU MBALIMBALI.

Ni jambo lililo wazi na lisilopingika kuwa; dini ya Kiislamu mfano wa dini nyengine ina madhehebu tofauti, na kila dhehebu lina sifa zake katika mambo ya akida na namna ya utendaji wa amali kutokana na akida hizo wanazoziamini, lakini tofauti hizo sio kubwa kiasi ambacho pasiwe na uwezekano wa kutoshirikiana baina ya wafuasi wa dhehebu fulani na wafuasi wa dhehebu jingine, bali wafuasi hao wa madhehebu tofauti wanaweza kushirikiana na kukabiliana na fikra za watu wa kimagharibi ili kuondoa kasumba au tata zinazotolewa na watu hao kwa ajili ya kuiharifu, basi waislamu inawapasa  kuihifadhi dini yao na kutowaruhusu watu hao wenye fikra hizo mbovu kufanikiwa katika malengo yao ya kuiharibu dini hiyo takatifu.
Kwa hakika kuleta mashirikiano hayo kunahitajia kutunzwa au kuadhimishwa misingi na vigezo vya kila madhehebu, na jambo la muhimu zaidi ambalo linafaa kutekelezwa ni kuwa; kila dhehebu ni lazima litambue akida  ya dhehebu jingine, kwa sababu kufanya hivyo kunaweza kuzuia khitilafu zilizopo  baina ya dhehebu na dhehebu, na kupatikana njia zitakazoweza kuleta mashirikiano.
Njia bora inayoweza kuyafanya madhehebu kufahamiana ni kutambuana kupitia misingi ya dini yao ya Kiislamu, na kutambuana akida zao kupitia maulamaa wao maarufu waliobobea kielimu na wanaotambulika katika jamii, kwa sababu ikiwa watafahamiana akida zao kupitia wafuasi wa madhehebu yao, wafuasi ambao hawana elimu ya kutosha inayohusiana na akida zao, na wafuasi wa madhehebu tofauti wakajenga uadui na kuwekeana chuki kutokana na ikhitilafu walizonazo, hapana shaka uadui na chuki hizoz itafunga na kuzuia njia zitakazowapeleka katika mashirikiano, na mafahamiano au mashirikiano yatabadilika na kuwafanya waislamu hao watengane kutokana na tofauti zao za kiakida na kiamali.

Hivyo ni lazima tujue akida ya Historia ya kila madhehebu kupitia kwa wenye madhehebu yao badala ya kujifunza madhehebu Fulani kupitia kwa adui yao. Tukijuana tutaheshimiana na kupendana kama waislamu.

Saturday 14 June 2014

SABABU YA KUITWA MWEZI SHAABAN

Imekuja na kuelezwa katika maana ya neno Shaaban kauli nyingi sana. Na kati ya kauli hizo ni yale yaliyo semwa na Ibnu mandhuur katika lisaanul-Arab juzu ya kwanza: (Kwa hakika umeitwa kwa jina la Shaaban kwa sababu umedhihiri na kuwa kati ya mwezi wa Ramadhani na Rajabu, na wingi wake ni Shaabaanaati, na Shaabaini, na Shaaban: Ni kizazi kitokanacho na Hamdan, Kilitoka katika vizazi vya Yemen, Na kwenye kizazi hiki hunasibishwa Aamir As-sha’abiy, na imesemekana: Shaaba ni jabali lililoko kwenye nchi ya Yemen, nalo ni lenye mapango au mabonde mawili).
Na muandishi wa Al-munjid fi llugha amesema: (umeitwa kwa jina hilo kutokana na waarabu kutawanyika na kusambaa ndani ya mwezi huo katika kutafuta maji).
Ama yaliyo kuja kutoka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w) ni kauli yake isemayo: (Kwa hakika umeitwa kwa jina la Shaaban kwa sababu ndani ya mwezi huo hutawanyika riziki za waumini).
Na amesema (s.a.w.w) (Kwa hakika umeitwa kwa jina la Shaaban kwa sababu hudhihiri ndani yake kheri nyingi kwa ajili ya Ramadhan).

MUISLAMU ANATAKIWA KUWA NA TABIA NJEMA.

Mtume Mohammad ametambulishwa katika Qur’ani kama ifuatavyo:
“Na hakika una tabia njema kabisa.” (68:4)

Mtume wetu ametajwa na Qur’an kuwa ni mtu mwenye tabia njema kabisa. Ni sunnah na lazima kwa kila muislamu kuwa na tabia njema na huruma kwa wanadamu wote kama alivyokuwa kiongozi na muombezi wa umma huu. Kuna aya nyingine ambao Allah anasema kuwa kama Mtume angekuwa ni mjeuri basi watu wangemkimbia. Sijui hawa watu wanaodhani kuwa Uislamu ni ubabe wamezisoma kweli aya hizi au wanacho kitabu kingine wanachokifuata tofauti na Qur’an?
Mwaka jana katika mahafali ya chuo kikuu cha SUA alisimama mhadhiri mmoja wa kiwahhabi na kutangaza hadharani kuwa muislamu lazima awe mbabe na kwamba anapokutana na kafiri katika njia nyembamba ni haramu kumpisha kafiri katika njia na kwamba kilicho sunnah na kumsukuma akupishe wewe Muislamu ndio upite njiani na yeye apite porini. Nilisikitika sana na sikubaliani na Uislamu bandia wa namna hii.

Kama hivyo wanavyodai waislamu hawa wa bandia itakuwa na maana gani ayah hii ambayo inasema:
 “Waite watu katika njia ya Mola wako kwa hikima na mauidha mema, na ujadiliane nao kwa nama iliyo bora…” (16:125)

Je inawezekana kufanya tabligh kwa ubabe na mauaji kama wanavyofanya Mawahhabi na magaidi wengine? 

Friday 13 June 2014

NDOA YA MUHAMMAD MUSTAFA NA KHADIJA

Khadija, binti ya Khuwaylid, alikuwa mkazi wa Makka. Naye pia alikuwa wa kabila la Quraishi. Aliheshimiwa sana na watu wa Makka kwa sababu ya tabia yake ya mfano na uwezo wake kifedha. Kama vile watu wa Makka walivyomuita Muhammad 'Sadiq' na 'Amin', walimuita Khadija 'Tahira', yenye maana ya "Aliye safi." Alikuwa akijulikana pia miongoni mwa Waarabu kama 'Malkia wa Wafanya biashara.' Wakati wote misafara ilipoondoka Makka au kurudi Makka, waliona kwamba mzigo wake ulikuwa mkubwa kwa ujazo kuliko mizigo yote ya wafanyabiashara wa Makka ikichanganywa pamoja.
Muhammad alipokuwa na umri wa miaka 25, ami yake na mlezi wake, Abu Talib, alimshauri Khadija, na kuelewa kwake kwa kimya, kwamba amchague yeye kama wakala wake katika mmoja wa misafara yake, uliokuwa uondoke kwenda Syria punde tu, mara.
Khadija kwa kweli alikuwa akihitaji wakala kwa wakati ule hasa. Alikubali kumchagua Muhammad kama wakala wake. Alichukua madaraka ya bidhaa za Khadija, na msafara ukatoka kwenda Syria. Mtumwa wa Khadija, Maisara, pia alifuatana naye na akamsaidia kama msaidizi wake.
Safari hii ya kibiashara kwenda Syria ilifanikiwa kupita matarajio, na Khadija alivutiwa sana na uwezo wa wakala wake na uaminifu wake kiasi kwamba aliamua kumpa madaraka ya shughuli zote za biashara zijazo baadaye. Safari hii pia ilithibitisha kuwa mwanzo wa ndoa yao.
Makubaliano ya ndoa, katika mfumo rahisi wa kizamani, yanaonyesha kupendana kwa Muhammad na Khadija; yanamuelezea yeye Muhammad kama mtu hodari zaidi wa kabila la Quraish; na anatamka mahari ya wakia kumi na mbili za dhahabu na ngamia ishirini, ambayo ilitolewa kwa ufadhili wa ami yake, Abu Talib.
Abu Talib alisoma khutba ya ndoa ya Muhammad na Khadija, na hotuba yake au waadhi unathibitisha bila shaka yoyote kwamba alikuwa akiabudu Mungu mmoja.
Alianza hotuba yake katika mfumo wa "Kiislam" kwa kutoa sifa na shukrani kwa Allah (s.w.t.) kwa rehma zake na baraka zisizoidadi na neema, na alimalizia kwa kumuomba Rehma na neema Zake juu ya maharusi wapya hao.
Ndoa ya Muhammad na Khadija ilifanikiwa sana. Imebarikiwa na furaha kuu isiyo na kifani kwa wote, mume na mke. Khadija alijitolea maisha yake kwenye huduma kwa mumewe na Uislamu. Alitumia utajiri wake mkubwa wote kwa kuimarisha Uislamu, na katika ustawi wa Waislamu.
Khadija alikuwa na hisia za ujumbe kama zile zile alizokuwa nazo Muhammad, na alikuwa na shauku kama aliyokuwa nayo ya kuona Uislamu unaushinda upagani. Kwa shauku yake ya kuuona ushindi wa Uislamu, aliongeza uwajibikaji na uwezo. Alimuondoa mumewe katika ulazima wa kutafuta maisha, na hivyo kumuwezesha kutoa muda wake wote katika ulazima wa kutafuta kujiandaa kwa kazi kubwa iliyokuwa imelala mbele yake.
Huu ndio mchango wa maana sana alioutoa kwenye kazi ya mumewe kama Mtume wa Mungu. Alikuwa ndio egemeo ambalo Muhammad alilihitaji katika miaka yote ya maandalizi kwa ajili ya Utume.

Ndoa ya Muhammad na Khadija ilibarikiwa pia na kuzaliwa kwa binti yao, Fatima Zahra. Ingawa neema ambazo Mungu amewajaalia juu yao zilikuwa nyingi, hapakuwa na yoyote waliyoithamini zaidi ya binti yao, Fatima Zahra. Alikuwa ni mboni ya macho ya baba yake, na "Bibi wa Peponi" wa baadaye. Baba na Mama walitoa kwa wingi mno mapenzi yao juu yake, na alileta matumaini ndani ya nyumba yao.

FIKRA ZA KIWAHHABI NI KUYAKUFURISHA MADH-HEB NA KUPANDA MBEGU YA CHUKI NA UTENGANO MIONGONI MWA WAISLAMU.

Enyi Waislam wenye utambuzi,
Asalaam alaykum. Mmesoma nasiha za mara kwa mara kutoka mtandao wa alhidaaya.com. Huu ni mtandao wa Mawahhabi ambao lengo lao ni kuwapotosha Waislam, kuleta chuki na utengano miongoni mwa Waislam na kuwakufurisha wote ambao sio Mawahhabi. Watu hawa ni muhimu sana wawaambie Waislam asili ya dini yao, wametoka wapi, walipotea wapi na wafanye juhudi gani sasa ili wote tushikamane na kamba ya Mwenyezi Mungu na wala tusifarakiane. Na wanaogopa kurudi kwenye tarekh maana tarekh itawaumbua. Ni bahati mbaya sana kwamba wamenasa ktk fikra potofu za kiwahhabi na kuwa wafuasi wa Muawiyyah na Yazid na inshallah Mwenyezi Mungu ni Mlipaji Bora kabisa.
Naam maneno yangu haya yana ushahidi. Nitamchukia na kumpinga sana yeyote, kwa ushahidi madhubuti sio ushahidi blaa blaa na ninapofanya hivyo sijali yeyote mradi tu nautetea Uislam Mtukufu, Mtukufu Mtume(s.a.w.w) na Ahlul Bayt Rasulullah(s.a.w.w) na ikiwa kufanya haya ni kuwa rawafidha basi mimi ni rawafidha mkubwa.
Ewe msomaji mtukufu,
Kipo kitabu kiitwacho "AS-HIATU-WA AT-TASHAYUU" kilichotungwa na Mpakistani mwenye chuki ambaye ni miongoni mwa wanaofadhiliwa na Mawahhabi, jina lake ni Ihsan Ilahi Dhahir na kimechapwa Saudia. Na ndani yake mtungaji anazitupa tuhuma na uzushi dhidi ya Ushia, na anadai kwamba yeye anaeleza kutokana na vitabu na rejea za Mashia.
Kwa mfano, utaona katika uk wa 20 wa kitabu hicho, anataja neno la Al-Marhum Al-Ustadh Mheshimiwa Sheikh Muhammad Hussein Al Mudhafar, kisha analisherehesha kufuatana na vile apendavyo yeye na vile nafsi yake inayoamrisha maovu inavyomtuma.
Tunaweka wazi neno hilo pamoja na sherhe ya Wahhabi huyu ili uone mwenyewe jinsi Mawahhabi waliofilisika kwa dalili, wanavyotegemea maneno ya tuhuma, uzushi na uongo dhidi ya Shia. Mar-hum Al-Mudhafar anasema:
"Fakanatid-Daawatu Littashayui Liabil-Hassan Alayhis-Salaam Min Sahihir-Risalat Salallahu Alayhi Waalihi Wasallam Tamshi Minhu Janban Liyanbi Maad-dawat Lish-Shahadatayn"
Tafsir Yake:
Mwito kutoka kwa Mtume (s.a.w.w) kumfuata Abul Hassan Ali(a.s) ulikua ukienda sambamba na mwito wa Shahada mbili.
Na maana ya maneno yake haya ni kwamba:
Ushia haukuzalikana kutokana na hali ya kimazingira wala sio madhheb yaliyoanzishwa baadaye, bali ni Madh-heb ya asili ambayo chanzo chake kinaanzia kwa mwenyewe Mtume Muhammad (s.a.w.w), kwani Mtume (s.a.w.w) alikua akilingania watu juu ya Uimam wa Amirul-Muuminina Ali(a.s) sambamba na wito wa Shahada mbili.
Kisha Wahabi huyu muovu anayawekea Taaliq maneno ya Sheikh Mudhafar na anasema:
"Hakika Mtume (s.a.w.w)[kwa mujibu wa madai ya Mudhafar] alikua akimfanya Ali kua ni mshirika wake katika Unabii wake na ujumbe wake"!!!
iwapo mwandishi huyu sio mtumwa wa matamanio yake yenye chuki na mwenye kufadhiliwa na Mawahabi, na iwapo ni mchunguzi wa Itikadi za Kiislam za Kishia angesema na kusimamia Haki.
Uk 49 anatuhumu Ushia kwamba umepokea fikra zake kutoka kwa Abdallah Bin Sabaa aliyezalikana kutoka kwa Myahudi wa Yemen, na anavyoitakidi Tabari ni kwamba Abdallah Bin Sabaa alidhihirisha Uislam na kuficha Uyahudi na mapenzi yake kwa Imam Ali(a.s) aliyafanya kifuniko cha kueneza fikra zake.
Mwandishi huyu wa Kiwahhabi anategemea mambo aliyoyapokea Tabari kuhusu uzushi huu, Amma sanad ya riwaya ambayo Tabari anaielezea ni kama ifuatavyo neno kwa neno:
"Aliniandikia As-Sariyyu kutoka kwa Shuaib, kutoka kwa Seif, kutoka Atiyyah naye toka kwaYazid Al-Faq-Asi: Abdallan Bin Sabaa alikuwa Myahudi katika watu wa Sanaa...."[vile vile ameipokea riwaya hii Ibn Khaldun Al-Magharib na Ibn Kathir Ash-Shami na walio mfano wa Tabar miongoni mwa maadui wa Ahlul-Bait].
Sasa tunaiweka riwaya hii kwenye meza ya uchunguzi.
Kwa mtazamo wa haraka ndani ya vitabu vya elimu ya rijali (ambavyo vimeandikwa na wanachuoni wa Kisunni) vitatutosheleza kufahamu hali za wapokezi hawa:
1)As-Sari sawa sawa akiwa ni As-Sari Ibn Ismail Al-Kufi au As-Sari Ibn A'sim aliyekufa mwaka 258 kila mmoja wao ni miongoni mwa waongo na wazushi.
Tazama:
a)Tahdhibut-Tahdhib cha Ibn Hajar Juz 3 uk 46
b)Tarekh Al-Khatib Juz 1 uk 193
c)Mizanul-Itidal Juz 1 uk 37
d)Lisanul Mizan Juz 3 uk 13
2)Shuaib Ibn Ibrahim A-Kufi: Majhul
[Hatambulikani hali yake] Tazama:

a)Mizanul-Itidal Juz1 uk 447
b)Lisanul-Mizan Juz 3 uk 145.
Haya ndiyo mategemeo ya uzushi na uongo wa Mawahhabi dhidi ya Ushia. Hawa ndio watetezi wa Tawhid na Sunna. Wao ni wapenzi na watetezi wa Muawiya na Yazid wauaji wa Bwana wa Vijana wa Peponi Imam Hussein(A.S) na watu wa nyumba ya Mtume (s.a.w.w)Na malipo mema yapo kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu.

MTUME MOHAMMAD (S.A.W.W) APEWA UANACHAMA WA SHIRIKISHO LA VIJANA WAADILIFU.

Baada ya kuwa kijana, Muhammad aliingizwa kama mwanachama wa lile Shirikisho la Wenye Maadili. Kama ilivyotajwa mapema, hili Shirikisho limejiapia lenyewe kuwalinda wayonge, kuwapinga madhalimu na waonevu, kukomesha unyonyaji wa namna yoyote ile.
Ikumbukwe kwamba ulikuwa ni ukoo wa Bani Hashim, ambao Muhammad nabii wa baadae alitokana nao, ambao ndio ulioanzisha lile Shirikisho la Wenye Maadili. Taratibu zao za kisiasa, Bani Hashim walikwishatangaza vita juu ya udhalimu na dhulma. Waliweka wazi kwamba hawatakula njama na wenye nguvu dhidi ya wanyonge; wala hawangeridhia katika unyonyaji wa maskini kwa Maquraishi wa Makka.
Sio miaka mingi baadae, Muhammad alikuwa aanzishe utaratibu wa ujenzi upya wa jamii ya wanadamu, sehemu ya uchumi ambayo itatambua wazi uharibifu wa unyonyaji. Angezichukua zile "fursa" za Maquraishi na "haki " zao za kunyonya maskini na wanyonge, kutoka kwao.
"Lile Shirikisho la Wenye Maadili linaelekea kuchukua sehemu muhimu sana katika maisha ya Makka, na kwa sehemu kubwa kuelekezwa kwa watu na sera ambazo baadae Muhammad alijikuta anapingana nazo. Hususan ukoo wake wa Bani Hashim ulikuja kuwa na wajibu mkubwa katika Shirikisho la Wenye Maadili."

(Muhammad, Prophet and Statesman, 1961)

Kueneza chuki dhidi ya Ushia na dhidi ya Iran ndiyo silaha ya mabeberu

Siku ya Jumanne ilikuwa ni siku ya kuadhimisha sikukuu ya mab'ath ya kupewa Utume Mtume wetu Muhammad SAW.  Sambamba na maadhimisho ya sikukuu hiyo, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, leo asubuhi ameonana na maafisa wa mfumo wa Jamhuri ya Kiislamu, matabaka mbali mbali ya wananchi na wageni wanaoshiriki kwenye mashindano ya kimataifa ya Qur'ani Tukufu pamoja na mabalozi wa nchi za Kiislamu waliopo nchini Iran.
Huku akisisitizia udharura wa ulimwengu wa Kiislamu kulipa umuhimu mkubwa suala la kutafakari mambo kwa kina, kuwa na muono mpana na wa mbali, kuwa na fikra zinazojenga na kuwa na welewa wa kutosha na wa kweli kuhusiana na kambi ya maadui wa umma wa Kiislamu na vile vile kushikamana umma wa Kiislamu na kutozipa nguvu tofauti za kiitikadi na utaifa amesisitiza kuwa, leo hii bendera ya Uislamu imeshapeperushwa juu, na moyo wa kujitambulisha Kiislamu Waislamu duniani umepata nguvu sana sasa hivi ikilinganishwa na huko nyuma.
Amesema, taifa la Iran pia kutokana na kuwa na dhana nzuri na kuwa na imani na msaada wa Mwenyezi Mungu, limo katika kupiga hatua za kimaendeleo na kuyaweka nyuma matatizo sambamba na kupata ushindi mtawalia katika mapambano yake na dhulma, ujahili na ukosefu wa uadilifu.
Ayatullah Udhma Khamenei, aidha ametoa mkono wa baraka kwa mnasaba wa maadhimisho ya siku ya kubaathiwa na kupewa Utume, Mtume wa Uislamu SAW na kusema kuwa, sababu kubwa ya kutumwa Mitume wa Mwenyezi Mungu hususan Mtume wa Uislamu SAW ni kuwaongoza watu kwenye kutumia akili, hekima na kutafakari mambo kwa kina.
Ameongeza kuwa: Iwapo suala la kutafakari kwa kina mambo na kutumia nguvu ya akili na muono wa mbali litaenea katika jamii ya Waislamu, basi bila ya shaka yoyote matatizo mengi ya ulimwengu wa Kiislamu yatatatuka.
Vile vile ameashiria namna baadhi ya watu wanavyoyafahamu kimakosa mafundisho ya Uislamu na Qur'ani Tukufu na jinsi wasivyo na elimu ya kutosha kuhusu mafundisho hayo matukufu na kusema: Kutokuwa na mtazamo sahihi na kushindwa kuwa na welewa wa kina kuhusiana na mafundisho matukufu ya Uislamu na Qur'ani Tukufu kumepelekea leo hii baadhi ya watu watumie jina la Uislamu kuwadhulumu Waislamu wengine na hata kuwaua kwa umati ambapo hali ni mbaya kiasi kwamba imefikia hadi huko barani Afrika watoto wa kike wasio na hatia wanatekwa nyara kwa kutumia jina la Uislamu.
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu aidha ameashiria mfano mwingine ambao ndani yake nguvu ya akili na kutafakari mambo kwa kina inabidi itumike vizuri katika mazingira ya hivi sasa ya ulimwengu wa Kiislamu na kusema kuwa: Leo hii maadui wametangaza vita vya wazi dhidi ya Uislamu na silaha kubwa inayotumiwa na maadui hao ni kuzusha mizozo na hitilafu za kiitikadi na vita baina Waislamu wa Kishia na Kisuni na kama kama nguvu ya akili na kutafakari kwa kina mambo itatumizuri ika vbasi itawezekana kuuona mkono wa adui na shabaha zake na kutotumbukia kwenye njia ya kufanikisha malengo ya watu wanaoitakia mabaya dini tukufu ya Kiislamu.
Ayatullah Udhma Khamenei, ameutaja mshikamano na kuundwa umma mmoja wa Kiislamu kuwa ni miongoni mwa mahitaji ya dharura kwa ulimwengu wa Kiislamu na huku akisisitiza kuwa moja ya shabaha kuu za kuzusha mirafakano kati ya Waislamu na kueneza chuki dhidi ya madhehebu ya Kishia na dhidi ya Iran, ni kambi ya kibeberu kutaka kuficha matatizo yake na kuulinda utawala ghasibu wa Kizayuni.
Ameongeza kuwa: Kinachotarajiwa kutoka kwa mataifa ya Waislamu hususan wasomi, wanafikra na watu wenye vipaji na ushawishi katika ulimwengu wa Kiislamu ni kuwa na tadibiri na mtazamo mpana na wa mbali na kuitambua vilivyo kambi ya maadui wa umma wa Kiislamu na kwa njia hiyo ndipo itawezekana kutambua vizuri uhakika huo ulio wazi.
Vile vile amesisitiza kuwa, duru za kisiasa za Magharibi hivi sasa zinaeneza ujahilia ule ule ambao Bwana Mtume Muhammad SAW alitumwa na Mwenyezi Mungu kuja kupambana nao na kuuangamiza. Amesema: Ukosefu wa uadilifu, ubaguzi, kutojali heshima ya mwanadamu, kuyachanganya pamoja masuala ya kijinsia na kupiga propaganda za kuchochea uchafu wa kimaadili na wanawake kutembea uchi, yote hiyo ni mifano ya utamaduni fasidi wa Kimagharibi ambao kwa hakika ni kurejea kwenye ujahilia ule ule wa zama za huko nyuma ingawa kwa sura mpya ya kisasa.
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ameashiria pia njama kubwa zinazofanywa na maadui kwa lengo la kuzima mwamko wa Kiislamu na kusema kuwa: Ingawa njama hizo za maadui zinaonekana kijuu juu kuwa zimefanikiwa katika baadhi ya maeneo, lakini uhakika wa mambo ni kuwa, haiyumkiniki na ni muhali kukandamiza na kuzima mwamko wa Kiislamu.
Ayatullah Udhma Khamenei amegusia pia hatua za maendeleo zilizopigwa na taifa la Iran chini ya kivuli cha kuwa na imani na ujumbe aliokuja nao Bwana Mtume Muhammad SAW na mshikamano wa ndani wa taifa hili na ushujaa wake katika kukabiliana na adui pamoja na kuwa na hisia za matumaini kutokana na ahadi za nusra na msaada kutoka kwa Mwenyezi Mungu akiongeza kuwa: Leo hii kwa taufiki ya Mwenyezi Mungu, serikali yenye nguvu mpya ya Iran na watendaji wake wanafanya kazi kubwa katika medani tofauti wakiwa na hisia za kulinda heshima ya Uislamu.
Kiongozi Muadhamui amekutaja kuweko matatizo na changamoto mbali mbali katika maisha ya mwanadamu kuwa ni jambo la kawaida kabisa na kuongeza kwamba: Watu wenye hekima na tadibiri huwa wanakubali kuvumilia matatizo kwa ajili ya kufikia kwenye heshima, hadhi ya mwanadamu na kuwa karibu na Mwenyezi Mungu lakini watu wasio na hekima, badala ya kuikubali Wilaya na uongozi wa Allah, wanakimbilia kwenye utawala wa mashetani na matokeo yake ni kujidhalisha na kujidunisha mbele ya mashetani hao.
Ayatullahil Udhma Khamenei ameendelea kulitolea ufafanuzi suala hilo kwa kuzungumzia kalibu na misingi iliyowekwa na Qur'ani Tukufu akisema: Kwa mujibu wa aya za Qur'ani Tukufu, watu ambao katika kutafuta heshima wanaacha Wilaya na uongozi wa Mwenyezi Mungu na kukimbilia kwa maadui wa Uislamu na ubinadamu na kwenye utawala wa mashetani, hatima yao ni kuwa duni na kamwe hawawezi kupata heshima bali hawatapata shukrani hata kutoka kwa hao mashetani wanaojidhalilisha kwao.
Amesisitiza kuwa: Tunapaswa kujifunza kutokana na fomula na msingi huu uliobainishwa na Qur'ani Tukufu na kuitambua njia sahihi na ya kweli ya kutufikisha kwenye ufanisi wa kweli ambayo ndiyo hiyo njia ya uongofu wa Qur'ani Takatifu.
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu ameitaja siri ya mafanikio na ushindi wa kila namna wa mfumo wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika nyakati tofauti kwenye mapambano mbali mbali ya kiuchumi, kisiasa, kijamii na kimataifa kwamba ni kutegemea na kuwa na nia nzuri na ahadi za Mwenyezi Mungu na kusisitiza kwamba: Hiyo ndiyo njia ya taifa la Iran na katika siku za usoni pia njia ya taifa hili itakuwa ni hiyo hiyo.
Mwishoni mwa hotuba yake, Ayatullah Khamenei amemuomba Mweyezi Mungu ammiminie rehema Zake Imam mtukufu (Imam Khomeini Mwenyezi Mungu amrehemu) kutokana na kutufungulia njia hii. Vile vile amemuomba Allah awamiminie rehema Zake mashahidi waliomwaga damu zao katika njia hii na rehema za Mwenyezi Mungu zilishukie taifa la Iran ambalo limethibitisha uimara wake katika hatua na vipindi vyote vya njia hii na rehema za Allah ziwafikie pia viongozi na maafisa wote wanaohusika katika ufanikishaji wa njia hii na ambao wako tayari wakati wote kujitolea na kufanya jitihada kubwa katika njia hiyo.
Kabla ya miongozo hiyo ya Kiongozi Muadhamu, Hujjatul Islam Walmuslimin Hassan Rouhani, Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametoa mkono wa baraka kwa mnasaba wa maadhimisho ya siku ya kupewa Utume Mtume Muhammad SAW na kusema kuwa, mab'ath ni ufufuo mkubwa katika historia na ni neema kwa ajili ya kutumia vizuri akili kulingana na wahyi utokao kwa Mwenyezi Mungu.
Amesema, Bwana Mtume Muhammad SAW aliweza kuzivutia nyoyo kwa upole na maadili yake adhimu na kumtunukia mwanadamu elimu, uhuru na umaanawi.
Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameitaja mifarakano, ukosefu wa uadilifu, machafuko na misimamo mikali ya kufurutu ada kuwa ni matatizo makubwa ambayo kambi ya ukafiri imeutwisha ulimwengu wa Kiislamu na kuongeza kuwa: Leo hii Mapinduzi ya Kiislamu yanalingania umoja, mshikamano na kuwekwa pembeni hitilafu ndogo ndogo katika umma wa Kiislamu ili umma huo uweze kusimama kwa nguvu moja kupambana na kambi ya kufru.


NAENDELEA NA UCHUNGUZI WA MADHEHEBU SAHIIHI: Chuoni:

Baada ya kuzifuatilia zile Hadithi katika Bukhari, Muslim, na Tirmidhiy huko maktaba ya
chuo chetu, ulinithibitikia ukweli wa usemi wake, na nilisitushwa na Hadithi zingine zilizo
zaidi ya hizi kwa dalili za wajibu wa kuwafuata Ahlu-Bayt, jambo lililonifanya niishi katika
hali ya mshtuko. Kwa nini hatujasikia Hadithi hizi hapo kabla.
Nilizionyesha kwa baadhi ya wenzangu chuoni ili washirikiane na mimi katika wakati huu
muhimu, baadhi waliathirika na baadhi hawakujali, lakini mimi niliazimia kuendelea na
uchunguzi hata kama kufanya hivyo kutanigharimu umri wangu wote. Ilipowadia siku ya
Alhamisi, nilikwenda kwa Abdul’mun’imu, alinipokea kwa mapokezi mema kwa utulivu na
akasema: “Ni wajibu juu yako usiharakie na uendelee na utafiti kwa ufahamu wote.”
Kisha tulianza uchambuzi wa mambo mengine mbalimbali, uliendelea mpaka jioni ya siku
ya Ijumaa, nilifaidika na mengi na nilivijua vitu vingi ambavyo nilikuwa sivijui, na kabla ya
kurejea kwangu chuoni aliniomba vitu vingi nivitafute.
Iliendelea hali kama hii kwa muda, na hali ya mjadala kati yangu na yeye ilikuwa ikibadilika
kati ya muda na muda, kwani wakati mwingine nakuwa mkali wa maneno kwake, na
pengine nafanya inadi kwenye ukweli uliowazi. Kwa mfano nilikuwa ninaporejea baadhi ya
Hadithi katika vyanzo na ninakuwa na uhakika kuwa ipo, huwa namwambia: “Kwa kweli
Hadithi hizi hazipo.” Mpaka sasa sijui ni kitu gani kilikuwa kinanisukuma nifanye hivyo ila ni
kutambua kushindwa na utashi wa ushindi.
Kwa sura kama hii na kwa uchambuzi wa ziada mbele yangu ukweli mwingi ulifichuka
mbele yangu ambao ilikuwa sikuutazamia, na nilikuwa katika muda wote huu nafanya
mjadala sana na wanafunzi wenzangu, na wenzangu walipoona nawakera waliniomba
nijadiliane na mwalimu, aliyekuwa akitufundisha Fiq’hi, nikasema: Hapana kizuizi kwangu, lakini tu kuna vizuizi kati yangu na yeye ambavyo vinanizuia kuwa na uhuru wa kuongea.
Hawakukinaika na hili, na wakasema: Kati yetu na wewe kuna Ustadh, ukimtosheleza sisi tu
pamoja na wewe.
Nikasema: Mas’ala sio kutosheka, bali ni dalili na uthibitisho, na kutafuta ukweli. Na katika
somo la kwanza la fiq’hi nilianza mjadala naye kwa sura ya maswali mengi, nilimuona
hanipingi sana bali ni kinyume alikuwa anatilia mkazo kuwapenda Ahlul-Bayt (a.s.) na kuwa
kuwafuata na kuzitaja fadhila zao ni lazima.
Na baada ya siku nyingi aliniomba niende kwenye maktaba yake kwenye makao ya chuo na
baada ya kwenda kwake alinipa kitabu chenye juzuu kadha nacho ni (Usul-Kaafiy),
ambacho ni miongoni mwa vyanzo vya Hadithi vinavyoaminika mno kwa Shia. Aliniomba
nisikipuuze kitabu hiki kwa kuwa ni turatha ya Ahlu-Bayt. Sikusema kitu kwa shitukizo kama
hili, nilichukua kitabu na nilimshukuru kwa hilo.
Nilikuwa nakisikia kitabu hiki na sikupata kukiona, ni jambo ambalo lilinifanya nimshuku
kuwa ni Shia Dr. huyu, pamoja na kuwa namtambua kuwa ni mfuasi wa Malik, na baada ya
swali na kutaka tafsiri yake ilinibainikia kuwa yeye ni Sufiy, ni mwenye kujihusisha na
kuwapenda Ahlul-Bayt (a.s.).
Na wenzangu walipotambua maafikiano haya kati yangu na huyu ustadh, waliniomba
nifanye mjadala na ustadhi mwingine aliyekuwa akitusomesha mada ya Hadith, na alikuwa
mtu wa dini sana mnyenyekevu mwenye tabia njema. Na nilikuwa nampenda sana,
nilikubali ombi lao, na ilianza kati yetu mijadala mingi, na nilikuwa namuuliza usahihi wa
baadhi ya hadithi, alikuwa anatilia mkazo kuwa ziko sahihi, na baada ya muda nilihisi
kutopenda kwake na kutoridhika kwake na mjadala wangu, pia wenzangu walihisi hivyo,
hapo niliwaza njia bora ya kuendelea na mjadala ni maandishi.
Hivyo basi nilimwandikia jumla ya Hadithi na riwaya ambazo kwa wazi zajulisha wajibu wa
kufuata madhehebu ya Ahlul-Bayt (a.s.) na nilimwomba atafiti usahihi wake. Na nilikuwa
namuuliza kila siku juu ya majibu, naye hutoa udhuru kuwa hajafanya utafiti. Nilimfuatilia
kwa njia hii mpaka alihisi kuwa namdhiki.
Akaniambia zote ni sahihi. Nikasema kwa kweli ziko wazi zikihusu wajibu wa kuwafuata
Ahlul-Bayt. Hapo hakujibu na aliondoka haraka kwenda maktaba.
Mwenendo huu ulikuwa ni mshitusho kwangu na ni jambo lililonifanya nione ukweli wa usemi
wa Shia. Lakini nilipenda kwenda polepole na kutoharakia hukumu.
Na miongoni mwa ajabu ya tukio la bahati ni kwamba mkuu wa chuo naye ni ustadhi Ulwan,
alikuwa anatusomesha somo la tafsiri, siku moja akasema katika kutafsiri kauli yake ALLAH (s.w.t):
“Kwa kweli Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w) alipokuwa Ghadiir Khum, alinadi kuwaita
watu wakajikusanya, aliushika mkono wa Ali (a.s.) akasema: “Ambaye mimi ni mtawala

wake hivyo Ali ni mtawala wake.”

Sheria za Kiislamu na demokrasia ndiyo misingi miwili mikuu katika aidiolojia ya Imam Khomeini

Wapenzi wa Imam Khomeini (MA) kutoka kila kona ya Iran wameshiriki katika kumbukumbu za mwaka wa ishirini na tano wa kufariki dunia muasisi wa Mapinduzi ya Kiislamu, zilizofanyika katika eneo alipozikwa mwanachuoni huyo mkubwa, na kuonyesha taswira isiyo na kifani ya hamasa, kusimama kidete, heshima na mapenzi yao kwa malengo matukufu ya Mapinduzi ya Kiislamu na wakati huo huo kutangaza kwa mara nyingine tena utiifu wao kwa mwanachuoni huyo aliyetangulia mbele ya Haki.
Ayatullahil Udhma Sayyid Ali Khamenei, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amehudhuria hadhara hiyo kubwa iliyojaa nuru na kuhutubia hadhirina. Katika hotuba yake, amezungumzia asili na sababu ya kuongezeka kila leo hamu na mapenzi ya mataifa ya walimwengu ya kuusoma na kuzidi kuuelewa mfumo wenye nguvu kubwa na unaozidi kuimarika wa Jamhuri ya Kiislamu ambao umeiundwa juu ya msingi wa sheria za Kiislamu na demokrasia iliyotokana na mafundisho ya dini tukufu ya Kiislamu. Amesema sheria za Kiislamu na demokrasia ni vitu viwili vikuu vilivyomo kwenye chuo na aidiolojia ya Imam Khomeini (MA).  Vile vile amesisitiza kuwa, wananchi na viongozi wa Iran wameshikamana vilivyo na nakala hiyo mpya ya kisiasa – kiraia na kuongeza kuwa: Usumbufu na njama za kila namna zinazofanywa na Marekani na kupungua kasi ymoyo wa kuelekea kwenye mwamko wa Imam Khomeini (MA) ni changamoto mbili kuu ambazo iwapo taifa la Iran litazitambua na kuzishinda, litaweza kuendeleza vizuri njia iliyojaa fakhari na ufanisi ya Imam (MA).
Katika sehemu ya kwanza ya hotuba yake mbele ya hadhara hiyo adhimu ya kitaifa, Ayatullahil Udhma Khamenei  amelitaja suala la kuzidi kuvutiwa walimwengu na hasa wa mataifa ya Waislamu na Imam Khomeini na Jamhuri ya Kiislamu kuwa ni uhakika muhimu sana na kuongeza kuwa: Hivi sasa na baada ya kupita miaka 25 tangu afariki dunia Imam Khomeini (MA) matabaka mbali mbali ya watu hasa vijana na watu muhimu katika ulimwengu wa Kiislamu wamezidi kuwa na hamu na shauku ya kuitambua zaidi aidiolojia ya demokrasia ya kidini, nadharia ya Fakihi Mtawala (Wilayatul Faqih) na masuala mengine yanayohusiana na Mapinduzi ya Kiislamu.
Ameyataja mashambulizi yasiyosita na makubwa mno wa kisiasa na kipropaganda ya maadui wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kuwa ni moja ya sababu zilizoongeza hamu ya mataifa ya walimwengu kutaka kuyajua zaidi Mapinduzi ya Kiislamu na kuongeza kwamba: Fikra za walio wengi katika ulimwengu wa Kiislamu; hivi sasa na kuliko wakati mwingine wowote, zimekuwa na hamu kubwa zaidi ya kuujua wasifu na uhalisia wa mfumo wa kiutawala wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ambao unashambuliwa kwa mashambulizi makubwa kiasi chote hiki kutoka kila kona ya dunia na zina hamu na kuelewa siri ya taifa la Iran ya kuweza kusimama kidete na kupata mafanikio makubwa katika misimamo yake licha ya kukumbwa na dhoruba zote hizo za mashambulizi ya kila upande ya maadui.
Aidha ameutaja uwezo, nguvu na maendeleo yanayoongezeka kila leo ya taifa la Iran kuwa ni sababu nyingine inayoyafanya mataifa ya dunia yawe na shauku ya kuijua zaidi Jamhuri ya Kiislamu na mfumo wa demokrasia ya kidini unaotawala nchini Iran.
Ayatullah Khamenei ameutaja mwamko wa Kiislamu na hisia za kupinga uistikbari na ubeberu kuwa ni moja ya matunda ya shauku na hamu ya mataifa hasa ya Kiislamu ya kuyatambua zaidi Mapinduzi ya Kiislamu na kusisitiza kwamba: Kambi ya kibeberu, inaendelea kufanya makosa ya kiistrajitia kwa kudhani kuwa imeweza kung’oa mizizi ya mwamko wa Kiislamu kwani mtu anapoangalia kwa kina na kuelewa mambo yaliyopelekea kutokea mwamko wa Kiislamu atatambua vyema kuwa mwako huo si kitu kinachoweza kuondoka, na kwamba mwamko huo utachomoza tena na tena na kupanuka kwa nguvu za hali ya juu zaidi.
Amesema, kizazi cha vijana katika ulimwengu wa Kiislamu kinatafuta majibu ya maswali muhimu ya kihistoria kwamba kwa nini na kivipi Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imeweza kusimama imara katika kipindi chote hiki cha miaka 35 licha ya kushambuliwa kutoka kila upande kiuadui, kijeshi, kisiasa na kipropaganda pamoja na kuwekewa mashinikizo na vikwazo vikubwa mno na Marekani ambavyo havijawahi kushuhudiwa mfano wake na wakati huo huo taifa la Iran kila leo likawa linazidi kupiga hatua za kimaendeleo na kuwa imara tena bila ya kuwa taifa la kihafidhina.
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu ameendelea kutoa ufafanuzi kuhusu sababu zinazoifanya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kuwa na mvuto wa aina yake akisema: Mataifa ya dunia na kizazi cha vijana na tabaka la watu wenye ushawishi katika ulimwengu wa Kiislamu wanayaona maendeleo mbali mbali ya taifa la Iran katika nyuga za anga na anga za mbali, wanaona namna Iran ilivyo katika orodha ya nchi kumi za dunia zilizo na maendeleo makubwa sana ya kielimu, wanaona jinsi kasi ya maendeleo ya kielimu ilivyo mara 13 zaidi nchini Iran ikilinganishwa na wastani wa kasi hiyo duniani na wanatambua kuwa taifa la Iran ni nambari moja katika siasa za eneo la Mashariki ya Kati na limesimama imara katika kupambana na utawala ghasibu wa Kizayuni na kuyahami na kuyatetea mataifa yanayodhulumiwa.
Ayatullahil Udhma Khamenei ameongeza kuwa: Mambo hayo humfanya kila mtu awe na shauku na hamu ya kutaka kuijua zaidi na zaidi Jamhuri ya Kiislamu.
Vile vile amekutaja kufanyika uchaguzi wa 32 katika kipindi cha miaka 35 iliyopita tena kwa kujitokeza kwa wingi wa kupigiwa mfano wananchi wa Iran katika uchaguzi huo, na kujitokeza kwa hamasa kubwa na kwa wingi mno wananchi wa Iran katika maandamano ya Bahman 22 (Februari 11, zinapofikia kileleni sherehe za Mapinduzi ya Kiislamu) na katika maandamano ya Siku ya Quds (Ijumaa ya mwisho ya mwezi Mtukufu wa Ramadhani) kuwa ni uhakika mwingine unaozifanya fikra za walimwengu zivutiwe na Iran.
Ameongeza kuwa: Sisi tumezoea kushuhudia mambo hayo na hatuuoni uadhama na umuhimu wake machoni mwetu, lakini uhakika huo wenye mvuto unawafanya watu walioko nje na wa nchi nyinginezo kujiuliza maswali mengi na kustaajabishwa sana na mambo hayo…
Kiongozi Muadhamu ameongeza kuwa, matukio na uhakika huu wote wa kuvutia umetokana na fikra za kipekee za mwasisi wa Mapinduzi ya Kiislamu yaani Imam Khomeini (MA) na ameendelea na hotuba yake kwa kutoa taswira fupi lakini iliyobeba vitu vingi ya chuo na aidiliojia ya Imam Khomeini (MA).
Nukta kuu iliyokuwemo kwenye sehemu hiyo ya hotuba ya Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ni uhakika huu kwamba kwa ajili ya kufikia kwenye lengo, inabidi tusipoteze njia ya lengo hilo na kwa ajili ya kupiga hatua katika njia sahihi pia tunamuhitajia mwasisi huyo (Imam Khomeini – MA) mwenye fikra za busara na anayeangalia mbali.
Ayatullah Khamenei amekutaja kujenga mfumo wa kiraia – kisiasa juu ya msingi mantiki ya Kiislamu ndiyo shabaha kuu ya Imam Khomeini na kuongeza kuwa: Kuporomoka utawala kibaraka, fasidi na wa kidikteta wa Shah na kung’oa mizizi ya utawala huo ulikuwa ni utangulizi wa ujenzi wa jengo adhimu ambalo Imam alilipigania kwa hima yake kubwa na kwa kushirikiana na wananchi wa Iran.
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ametoa ufafanuzi zaidi kuhusu nguzo na misingi mikuu ya mfumo wa kisiasa wa wananchi uliokusudiwa na Imam Khomeini (MA) kwa kugusia nukta mbili kuu za kimsingi ambazo zimeshikamana kikamilifu akisisitiza kuwa: Kwanza kabisa ni sheria za Kiislamu ambazo ndiyo roho na msingi mkuu wa Jamhuri ya Kiislamu na pili ni kuwakabidhi wananchi kazi za kuendesha nchi kupitia mfumo wa kidemokrasia.
Ameongeza kuwa: Hakuna mtu aliyefikiria kwamba Imam Khomeini (MA) angeliweza kuchukua uchaguzi kutoka katika utamaduni wa Magharibi na kuuchanganya na fikra ya Kiislamu kwani ni jambo lisilo na chembe ya shaka kwamba, kama uchaguzi na demokrasia isingelikuwa inawezekana kuichukua ndani ya sheria za Kiislamu, basi Imam wetu aliyekuwa muwazi na mwenye misimamo isiyotetereka, angelilitangaza wazi suala hilo.
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu amesisitiza kuwa: Kwa mujibu wa chuo na aidiolojia ya Imam Khomeini, sheria za Kiislamu ambazo ndio uhalisia na asili ya mfumo wa Kiislamu zinapaswa zizingatiwe kikamilifu katika masuala yote, katika utungaji sheria, katika utungaji wa sera katika kuteua na kuondoa viongozi, katika miamala ya kawaida ya watu na kwenye masuala mengineyo yote, na wakati huo huo mchakato wa kazi katika mfumo huo wa kisiasa na kiraia ufanyike kwa mujibu wa demokrasia inayozingatia sheria za Kiislamu; na wananchi nao imma kwa njia ya moja kwa moja au isiyo ya moja kwa moja waweze kuchagua viongozi wa nchi yao.
Kiongozi Muadhamu amekutaja kutekelezwa kikamilifu sheria za Kiislamu kuwa kutapelekea kudhaminiwa misingi minne mikuu ambayo ni kujitegemea, uhuru, uadilifu na umaanawi.
Ameongeza kuwa: Kushikamana na sheria zilizojaa ufanisi za Kiislamu, mbali na kuleta uhuru wa watu binafsi na wa kijamii, unalikomboa pia taifa kutoka katika minyororo ya mabeberu yaani unaliletea taifa uhuru wa kitaifa na vile uadilifu unaoambatana na umaanawi na kuchunga mafundisho ya Mwenyezi Mungu.
Baada ya hapo Ayatullahil Udhma Khamenei amebainisha nukta nyingine ya kimsingi ya Imam Khomeini (MA) akisema: Katika chuo na aidiolojia ya Imam, nguvu na ushindi wowote unaopatikana kwa njia za mabavu na kutumia silaha haukubaliki, tab’an nguvu na uwezo unaotokana na chaguo la wananchi unakubalika na unaheshimiwa na mtu yoyote hapaswi kupinga maamuzi hayo ya wananchi na kama mtu atafanya hivyo basi ajue kuwa hiyo ni fitna.
Ayatullah Khamenei ameitaja nakala ya kisiasa - kiraia ya Imam Khomeini (MA) kuwa ni ukurasa mpya katika sarufi ya kisiasa duniani na katika kubainisha vipengee vingine vya nakala hiyo mpya amesema: Kuwasaidia watu wanaodhulumiwa na kupambana na dhulma ni miongoni mwa vipengee vikuu vya chuo na aidiolojia hiyo ya Imam.
Amefafanua zaidi kwa kuashiria uungaji mkono kamili na ambao haukusita hata mara moja wa Imam Khomeini (MA) kwa taifa madhulumu la Palestina na kuongeza kuwa: Kusimama kidete katika kupambana na dhulma na kuvunja wazi wazi haiba ya madhalimu ni msingi mkuu katika aidiolojia ya Imam Khomeini (MA) jambo ambalo inabidi viongozi na wananchi wote wa Iran walizingatie sana wakati wote.
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ameutaja ufanikishaji wa kivitendo vya vipengee vya nakala ya kisiasa – kiraia ya Imam kuwa ni moja ya tofauti kubwa na zawazi zilizopo baina ya aidiolojia hiyo ya Imam na aidiolojia nyingine zinazoishia kwenye maneno tu na hapo hapo akauliza swali hili la kimsingi akisema: Je, kazi kubwa iliyofanywa na Imam kwa mafanikio makubwa, itaendelea?
Amejibu swali hilo kwa kusema ndio, lakini kwa masharti.
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesisitiza kwa kusema: Katika jedwali jamali na lenye mvuto la Imam, kwa kawaida na mara zote kunakuwa na vyumba vilivyo wazi ambavyo upo uwezekano wa kuvijanaza na kuendelea na njia hii muhimu mno lakini kwa sharti la kufanya hima na kuwa na welewa wa kitaifa na kuchunga njia nzuri za kuvijaza vyuma hivyo.
Ayatullahil Udhma Khamenei amesifu uaminifu na utiifu wa taifa la Iran kwa malengo matukufu ya Imam Khomeini (MA) akisisitiza kuwa: Mwenendo uliooneshwa na taifa la Iran katika kipindi chote hiki cha miaka 25 ya tangu kufariki dunia Imam mtukukfu unaonesha kuwa vyomba vyote vitupu na vilivyo wazi katika jedwali hilo vitaweza kujazwa na kwamba chini ya kivuli cha kuendeleza njia ya Imam, Iran azizi kwa taufiki ya Mwenyezi Mungu itafikia kwenye vilele vya juu kabisa vya nguvu na uwezo.
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ameendelea na hotuba yake kwa kuwakhutubu hadhirina na mataifa yote akiyasisitizia nukta moja ya kimsingi kwa kusema: Kuendelea na njia ya Imam Khomeini (MA) na kufanikisha malengo matukufu ya mwanachuoni huyo, ni mfano wa kila lengo jingine muhimu, lazima kutakuwa na vizuizi na changamoto za kila namna ndani yake, na kama vizuizi na changamoto hizo hatutazitambua na kuziondoa, basi kuendelea na njia hiyo kutakuwa kugumu au hata kutakuwa hakuwezekani.
Hapo hapo Ayatullahil Udhma Khamenei ametaja changamoto mbili za nje na ndani na kusema kuwa ndizo changamoto kuu ambazo inabidi vijana, watu wenye ushawishi na vipaji, watoa nadharia na wasomi na wanafikra wa Iran wazizingatie na kuzipa uzito wa hali ya juu.
Ametoa ufafanuzi kuhusiana na changamoto za nje kwa kugusia usumbufu, kero na ukwamishaji unaofanywa na uistikbari wa kimataifa na hasa hasa Marekani na kuongeza kuwa: Tab’an baadhi ya wanafikra wa kisiasa wa Magharibi wanasema wazi kuwa, usumbufu na kero hizo hazina faida yoyote lakini pamoja na hayo Marekani bado inaendelea kutekeleza njama zake hizo kuu.
Ayatullah Khamenei ameongeza kuwa: Wamarekani wamezigawanya nchi za dunia na mirengo ya kisiasa na shaksia mbali mbali ulimwenguni katika mafungu matatu, kundi la nchi zinazotii amri, kundi la tawala na mirengo ambayo hivi sasa inakwenda nayo pole pole na tawala na mirengo isiyokubali kuburuzwa.
Ameongeza kuwa: Marekani inaziunga mkono kikamilifu na kwa kila namna tawala na nchi ambazo zinatii amri zake na ambazo zimejisalimisha kwake na haishughulishwi na uovu unaofanywa na tawala hizo katika jamii ya kimataifa, tab’an kupitia uungaji mkono wake huu wa kila upande, Marekani inajali tu maslahi yake na kuzibebesha tawala hizo ufanikishaji wa maslahi yake hayo.
Kiongozi Muadhamu amegusia baadhi ya mifumo ya tawala za kiimla na za kidikteta kupindukia zinazoungwa mkono na Marekani akisema kuwa: Kuhusiana na nchi hizo ambazo ndani yake hakuna uchaguzi hata mmoja unaofanyika na wala wananchi wake hawana nguvu za kusema hata neno moja, Marekani inakwepa kuziita nchi hizo kuwa ni za kiimla na kidikteta na badala yake inaziita kuwa ni nchi zinazotawaliwa na mfumo dume (kwa sababu zinatii amri za Marekani).
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu amelitaja kundi la pili la nchi zilizomo kwenye mgao wa Marekani kuwa ni nchi ambazo kutokana na kuwa na maslahi ya pamoja na Marekani, Washington imeamua kwenda nazo pole pole lakini wakati wowote inapopata fursa haichelei kushindilia jambia lake kwenye moyo wa nchi hizo.
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amezitaja nchi za Ulaya kuwa ni mfano wa wazi wa nchi hizo na kusisitiza kwamba: Tab’an licha ya kwamba Marekani inakwenda pole pole na nchi hizo za Ulaya kwa kulinda maslahi yake, lakini wakati huo huo inafanyia ujasusi maisha binafsi ya wananchi wa Ulaya na hata viongozi wa nchi hizo na inafanya hivyo kijeuri kiasi kwamba haiko tayari hata kuomba radhi.
Ameongeza kuwa: Tab’an nchi za Ulaya zimefanya kosa kubwa la kihistoria kwa kukubali kwao kutumikia manufaa na maslahi ya Marekani jambo ambalo linakwenda kinyume kabisa na maslahi ya mataifa yao.
Ayatullahil Udhma Khamenei amelitaja kundi la tatu la nchi za dunia kwa mujibu wa mgao huo wa Marekani kuwa ni lile la nchi ambazo hazikubali kuburuzwa na ubeberu wa Marekani.
Amesisitiza kuwa: Siasa za Marekani kuhusiana na nchi hizo ni kutumia bila mipaka wala kikomo uwezo wake wote kuhakikisha kuwa inatoa pigo kwa nchi hizo na inazisambaratisha.
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ametoa ufafanuzi zaidi kuhusu njia zinazotumiwa na Washington dhidi ya nchi ambazo hazikubali kuburuzwa na Marekani akisema: Tab’an hivi sasa uvamizi wa kijeshi si kitu kinachopewa kipaumbele na Marekani kutokana na dola hilo la kibeberu kupata hasara kubwa katika uvamizi wake wa kijeshi kwenye nchi za Iraq na Afghanistan.
Ameongeza kuwa, stratijia nyingine kubwa inayotumiwa na viongozi wa Washington kuhusiana na nchi zinazoendesha mapambano na zisizokubali kuburuzwa na Marekani ni kutumia vibaraka wake katika nchi hizo na kuongeza kuwa: Kufanya njama za mapinduzi ya kijeshi au kuwashawishi wananchi wamiminike barabarani kupinga tawala za nchi hizo ni miongoni mwa mbinu kubwa zinazotumiwa na Marekani kupitia vibaraka wake.
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ameongeza kuwa: Serikali yoyote ile katika nchi yoyote ile inayoingia madarakani kwa kura za wananchi, lazima watakuweko watu wachache ambao hawakuipa kura zao serikali hiyo na ambao ni wapinzani wa serikali hiyo. Sasa Marekani inatumia suala hilo kuwachochea wapinzani hao kuwaingiza baadhi ya watu mitaani kupinga serikali hiyo.
Ameongeza kuwa: Mifano ya siasa hizo za Marekani zinaonekana kwa uwazi katika baadhi ya nchi za Ulaya. Tab’an sisi hatuhukumu chochote katika suala hilo lakini tunajiuliza, wale maseneta wa Marekani wanaoonekana kwenye maandamano ya mitaani katika nchi hizo za Ulaya wanafanya nini kwenye maandamano hayo yasiyowahusu?
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu amekutaja kuanzisha na kuyatia nguvu makundi ya kigaidi kuwa ni mbinu nyingine inayotumiwa na Marekani kukabiliana na nchi hizo zisizotii amri zake na ambazo hazikubali kuburuzwa na dola hilo la kibeberu.
Amesema: Iraq, Afghanistan na baadhi ya nchi za Kiarabu pamoja na Iran yetu azizi ni wahanga wakuu wa mbinu hiyo ya Marekani dhidi ya nchi hizo.
Ayatullah Khamenei ameashiria pia uungaji mkono wa Marekani kwa kijigenge cha kigaidi cha wanafiki (MKO) na namna wanachama wa kigenge hicho cha kigaidi walivyo na uhusiano wa moja kwa moja na taasisi za utawala wa Marekani likiwemo Baraza la Congress la nchi hiyo na kuongeza kuwa: genge la kigaidi la wanafiki (MKO) ambalo limewaua kigaidi maulamaa, wasomi, na shakhsia wakubwa wa kisiasa na kiutamaduni pamoja na wananchi wengi wa Iran, linafanya vitendo vyake vya kigaidi chini ya uungaji mkono kamili wa Marekani.
Kiongozi Muadhamu amezitaja mbinu nyingine zinazotumiwa na Marekani dhidi ya nchi huru duniani ambazo hazikubali kuburuzwa kuwa ni kuzusha mizozo na mifarakano kati ya viongozi wa juu wa tawala za nchi hizo na kuzusha upotofu katika imani na itikadi za kidini za watu wa nchi hizo.
Ameongeza kuwa: Kwa taufiki na kwa msaada wa Mwenyezi Mungu, Wamarekani wameshindwa katika njama zao zote hizo mbele ya taifa la Iran na kwamba njama zao zote likiwemo jaribio la mapinduzi ya kijeshi, kuunga mkono wafanya fitna na wachocheaji wake, njama za kuwamimina barabarani baadhi ya wananchi na kuzusha ufa na hitilafu kati ya viongozi zote zimeshindwa kutokana na imani na mwamko wa taifa la Iran.
Baada ya kumaliza kubainisha changamoto za nje, Ayatullahil Udhma Khamenei ameanza kuzungumzia changamoto za ndani ya mfumo wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran akisema: Changamoto hizo na hatari kubwa itatokea wakati taifa na viongozi wa Iran watakapouweka mbali na kuusahau moyo na misimamo ya mwamko wa Imam mtukufu.
Kuhusiana na suala hilo Ayatullah Khamenei ameashiria kufanyika makosa katika kumjua rafiki na adui na kushindwa kumtambua adui wa asili na adui asiye wa asili na kuongeza kuwa: Watu wote wanapaswa kuzingatia kuwa, hawapaswi kughafilika na adui mkuu na wa asili katika matukio yote.
Kiongozi Muadhamu ametoa mfano mmoja wa wazi wa kushindwa kumtambua adui wa kweli na asiye wa kweli kwamba ni vitendo viovu na vya aibu vya makundi yasiyojua kitu na ya kijahili ya Kitakfiri, Kiwahabi na Kisalafi dhidi ya Ushia na kusisitiza kuwa: Watu wote wanapaswa kuzingatia kuwa, adui mkuu ni mashirika ya kijasusi ya mabeberu na watu ambao wanayachochea makundi hayo kwa kuyapa fedha na silaha.
Ameongeza kuwa: Tab’an kila mtu atakayefikiria kuichokoza Jamhuri ya Kiislamu kwa hakika atapata pigo na majibu makali sana kutoka kwa taifa la Iran, lakini pamoja na hayo sisi tunaamini kuwa, mkono wa adui ambao haukujificha sana na ambao unawachochea Waislamu kuuana wao kwa wao ndiye adui yetu mkuu na wa asili na si haya makundi yaliyodanganywa yakadanyika.
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amekutaja kupoteza mshikamano wa kitaifa, kukumbwa na uvivu na kutokuwa na mori wa kufanya kazi, kufanya kazi chache, kutawaliwa na uvunjikaji moyo na kukata tamaa na vile vile kuwa na fikra ghalati na potofu ya kudhani hatuwezi au kwamba huko nyuma pia hatukuweza, kuwa ni vipengee vingine vya changamoto za ndani ya mfumo wa Jamhuri ya Kiislamu na kusisitiza kuwa: Kama ambavyo Imam wetu azizi alisema, sisi tunaweza na kwamba azma na nia ya kweli ya kitaifa pamoja na uongozi na usimamiaji wa mambo kijihadi utaweza kuondoa mikwamo yote na kutatua matatizo yote ya usoni.
Mwishoni mwa miongozo yake, Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu amesisitiza kwamba: Jina lenye baraka la Imam mtukufu na mipango ya mwasisi huyo wa Jamhuri ya Kiislamu kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu italisaidia taifa la Iran katika hatua zote na kuiletea Iran azizi mustakbali unaong’ara kupitia kuleta matumaini, hamasa, mori na uchangamfu katika masuala yote.
Kabla ya hotuba ya Kiongozi Muadhamu, Hujjatul Islam Walmuslimin Sayyid Hasan Khomeini, amewakaribisha wafanya ziara na wapenzi wa mwasisi wa Jamhuri ya Kiislamu na kuzitaja jitihada za kuwaondolea shida watu na maeneo yaliyoko nyuma kimaendeleo, kuwasaidia wanyonge na kung’oa mizizi ya umaskini kwamba ndiyo yaliyokuwa malengo na shabaha kuu za Imam Khomeini (MA) na kuongeza kwamba: Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullahil Udhma Sayyid Ali Khamenei pia siku zote amekuwa akiyapa umuhimu na sisitizo la kipekee malengo na shabaha hizo za Imam, na hilo ni somo kwa watu wote.
Mfawidhi wa Haram Tukufu ya Imam Khomeini (MA) vile vile ameutaja utatuzi wa matatizo ya kiuchumi kuwa unahitajia tadibiri, mantiki, ushirikiano mkubwa kati ya Mihimili Mitatu Mikuu ya dola (Serikali, Bunge na Mahakama) na umoja na mshikamano wa kitaifa.
Ameongeza kuwa: Uchumi inabidi ufungamane kikamilifu na utamaduni wa kupambana na umaskini na kubaki nyuma kimaendeleo.