Thursday 12 June 2014

MTUME MOHAMMAD (S.A.W.W) ACHUKIA VITA NA UMWAGIKAJI WA DAMU

Wakati Muhammad alipokuwa na umri wa miaka ishirini, ilizuka vita miongoni mwa Maquraish, kabila lake, na kabila la Hawazin. Ingawa alikuwapo katika kampeni za vita hii, hakushiriki kwenye nafasi yoyote katika mapigano. Hakuua au kujeruhi mtu yoyote, hivyo kuonyesha katika kipindi hiki cha mwanzo cha maisha yake, kuchukia kwake umwagaji wa damu. Anasemekana, hata hivyo, kuwahi kuokota mishale kutoka uwanjani, na kuitoa kwa ami zake ambao walikuwa wanapigana.

Huu ndio msimamo wa Mtume mpaka alipokufa hakuwahi kuivamia nchi yoyote. Kazi ya Mtume ilikuwa kuwalinda waislamu dhidi ya mashambulizi na wala sio kuanzisha mashambulizi kama wafanyavyo leo baadhi ya watu wanaodai kuwa ni waislamu. Kila palipotokea mwanya wa kufanya mazungumzo ya amani alifanya hivyo mara moja ili kuepusha vita. Angalia vita ya Khandaq imefanyikia katika mji wa Madina, yaani makafiri walisafiri mamia ya maili kwenda kuwashambulia waislamu, hapo hakuna njia nyingine isipokuwa kuhihami. Vita ya Uhudi nayo imefanyikia kwenye eneo la Uhudi ambalo ni jirani na Madina, hata vita ya Badri ilifanyikia karibu na Madina. 

No comments:

Post a Comment