Saturday 14 June 2014

SABABU YA KUITWA MWEZI SHAABAN

Imekuja na kuelezwa katika maana ya neno Shaaban kauli nyingi sana. Na kati ya kauli hizo ni yale yaliyo semwa na Ibnu mandhuur katika lisaanul-Arab juzu ya kwanza: (Kwa hakika umeitwa kwa jina la Shaaban kwa sababu umedhihiri na kuwa kati ya mwezi wa Ramadhani na Rajabu, na wingi wake ni Shaabaanaati, na Shaabaini, na Shaaban: Ni kizazi kitokanacho na Hamdan, Kilitoka katika vizazi vya Yemen, Na kwenye kizazi hiki hunasibishwa Aamir As-sha’abiy, na imesemekana: Shaaba ni jabali lililoko kwenye nchi ya Yemen, nalo ni lenye mapango au mabonde mawili).
Na muandishi wa Al-munjid fi llugha amesema: (umeitwa kwa jina hilo kutokana na waarabu kutawanyika na kusambaa ndani ya mwezi huo katika kutafuta maji).
Ama yaliyo kuja kutoka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w) ni kauli yake isemayo: (Kwa hakika umeitwa kwa jina la Shaaban kwa sababu ndani ya mwezi huo hutawanyika riziki za waumini).
Na amesema (s.a.w.w) (Kwa hakika umeitwa kwa jina la Shaaban kwa sababu hudhihiri ndani yake kheri nyingi kwa ajili ya Ramadhan).

No comments:

Post a Comment