Monday 16 June 2014

MAWAHHABI WAWADANGANYA MASUNNI ILI KUWAINGIZA KWENYE DINI YAO MPYA NA KUWATUMIA KATIKA FITINA ZAO.

Afrika ya Mashariki imefaidi mazingira ya amani sana kiasi cha karne mbili zilizopita. Watu wa imani na itikadi zote waliishi pamoja kwa upendo na mapenzi. Kila mmoja akishiriki kwenye shughuli za mwenzake za kijamii na za Kidini. Ukiangalia kwenye Jumuiya za Kiislamu, wote wakihudhuria kwenye Misikiti ya kila mmoja, waliungana pamoja katika Maulidi na hafla za Muharram, na kupanua ushirikiano wao katika miradi ya kila mmoja. Kama Rais Mstaafu Alhaji Ali Hassan Mwinyi alivyosema katika hotuba moja ya hadhara;"Misikiti mingi ya Waislamu wa (Madhehebu ya) Shafi'i iliyoko Zanzibar na Pemba ilijengwa na kutolewa na Shia Ithna-ashariyya"
Hatimaye Wahhabi walianza Tabligh (Mahubiri) yao hapa. Badala ya kujaribu kuwaleta mapagani au wasio waislamu kwenye boma ya Uislamu, nia yao kabisa ilikuwa na bado inakaziwa katika kuwabadilisha Mashafii wawe Mawahabi. Kwa lengo hili, hujifanya kama wao ni Masunni, na kuchanganyika pamoja na Masunni. Mawahabi hao wamepanda mbegu ya fitinana chuki kati ya Madhehebu mbali mbali za Kiislamu, na hususan kati ya Sunni na Shia. Wanazungumza dhidi ya Shia, na kusambaza vitabu na vijitabu (vya mambo ya dini) dhidi ya itikadi ya Shia ambavyo vimejaa mambo ya uwongo na uzushi. Kishawishi chao kiko wazi, kwa kuwatenganisha Masunni na Mashia, wakitumaini kupata urahisi wa kuingia katika jamii ya Sunni na Misikiti yao, ingawaje tumaini hili lingali bado kukamilishwa katika Tanzania.
Hebu tuangalie katika mzizi wa uovu wa kampeni hii. Huenda hapo nyuma katika mwaka 1979, ambapo Mapinduzi ya Ki-Islamu yalipotokea katika (nchi ya) Iran, na watawala wa Kiwahhabi wa Saudia walihadharishwa vikali mno, hata kabla ya tukio la Mapinduzi ya Kiislamu, wakati Ayatullah al-'uzma al-Khomeini (R.A.) akiwa bado Najaf (Iraq). Waziri wa mambo ya nchi za nje wa Saudi Arabia, akizungumza katika hadhara moja ya Waarabu, aliuonya ulimwengu wa Waarabu kwamba kama Khomeini ataruhusiwa kuendeleza harakati zake kutoka Iraq kama hapo nyuma, sio tu kwamba utawala wa Shaha utaangushwa, lakini, hali katika eneo lote vile vile itakuwa imetibuliwa. Hivyo wakaishinikiza Iraq kuweka vikwazo juu ya Khomeini kwa hofu ya kwamba, kama juhudi zake zitafanikiwa katika Iran, zitatingisha tawala zao wenyewe zisizo imara.
Haikushangaza kwamba mara tu Mapinduzi ya Kiislamu yalipoimarika nchini Iran, hawa Wahhabi wakaanza propoganda kali yenye chuki dhidi ya Khomeini, dhidi ya Iran na dhidi ya Ushia. Kalamu za kukodisha zikaanza mchakato kutoa vitabu, makala na vijitabu dhidi ya Shia. Shia waliitwa Makafiri, na pengine mtu angeuliza: Kama ni Makafiri, basi kwa nini wanapewa viza kwa ajili ya Hija na Umra? Wairani waliitwa Majus (Waabudu Moto) kwa nini? Kwa sababu kabla ya kuja kwa Uislamu waliabudu moto. Kwa hoja hii nasi hatuna haki ya kuwaita Wahhabi Mushrikina? Kwa sababu kabla ya kuja kwa Uislamu watu wa Najd walikuwa wakiabudu Masanamu.

Baadhi ya waajiriwa wao wa ngazi za juu walikuwa ni (marehemu) Ihsan Ilahi Zaheer wa Pakistan, na Manzoor Ahmad Nu'mani na Abul Hasan Ali Nadwi wa India. Sauti itokayo kwenye vinywa vyao ni katika watakiwayo na mabwana zao kuyasema, na jambia la uzayuni lilichovywa kwenye damu ya waislamu linatumika kama kalamu yao. Kitabu kinachoandikwa dhidi ya Shia na watumwa hawa, kwa miezi michache tu kinatarujumiwa katika lugha zote kubwa za ulimwengu wa Kiislamu; na hufanywa kipatikane kila mahali, kadhalika husambazwa bure miongoni mwa Mahujaji:

No comments:

Post a Comment