Friday 13 June 2014

NAENDELEA NA UCHUNGUZI WA MADHEHEBU SAHIIHI: Chuoni:

Baada ya kuzifuatilia zile Hadithi katika Bukhari, Muslim, na Tirmidhiy huko maktaba ya
chuo chetu, ulinithibitikia ukweli wa usemi wake, na nilisitushwa na Hadithi zingine zilizo
zaidi ya hizi kwa dalili za wajibu wa kuwafuata Ahlu-Bayt, jambo lililonifanya niishi katika
hali ya mshtuko. Kwa nini hatujasikia Hadithi hizi hapo kabla.
Nilizionyesha kwa baadhi ya wenzangu chuoni ili washirikiane na mimi katika wakati huu
muhimu, baadhi waliathirika na baadhi hawakujali, lakini mimi niliazimia kuendelea na
uchunguzi hata kama kufanya hivyo kutanigharimu umri wangu wote. Ilipowadia siku ya
Alhamisi, nilikwenda kwa Abdul’mun’imu, alinipokea kwa mapokezi mema kwa utulivu na
akasema: “Ni wajibu juu yako usiharakie na uendelee na utafiti kwa ufahamu wote.”
Kisha tulianza uchambuzi wa mambo mengine mbalimbali, uliendelea mpaka jioni ya siku
ya Ijumaa, nilifaidika na mengi na nilivijua vitu vingi ambavyo nilikuwa sivijui, na kabla ya
kurejea kwangu chuoni aliniomba vitu vingi nivitafute.
Iliendelea hali kama hii kwa muda, na hali ya mjadala kati yangu na yeye ilikuwa ikibadilika
kati ya muda na muda, kwani wakati mwingine nakuwa mkali wa maneno kwake, na
pengine nafanya inadi kwenye ukweli uliowazi. Kwa mfano nilikuwa ninaporejea baadhi ya
Hadithi katika vyanzo na ninakuwa na uhakika kuwa ipo, huwa namwambia: “Kwa kweli
Hadithi hizi hazipo.” Mpaka sasa sijui ni kitu gani kilikuwa kinanisukuma nifanye hivyo ila ni
kutambua kushindwa na utashi wa ushindi.
Kwa sura kama hii na kwa uchambuzi wa ziada mbele yangu ukweli mwingi ulifichuka
mbele yangu ambao ilikuwa sikuutazamia, na nilikuwa katika muda wote huu nafanya
mjadala sana na wanafunzi wenzangu, na wenzangu walipoona nawakera waliniomba
nijadiliane na mwalimu, aliyekuwa akitufundisha Fiq’hi, nikasema: Hapana kizuizi kwangu, lakini tu kuna vizuizi kati yangu na yeye ambavyo vinanizuia kuwa na uhuru wa kuongea.
Hawakukinaika na hili, na wakasema: Kati yetu na wewe kuna Ustadh, ukimtosheleza sisi tu
pamoja na wewe.
Nikasema: Mas’ala sio kutosheka, bali ni dalili na uthibitisho, na kutafuta ukweli. Na katika
somo la kwanza la fiq’hi nilianza mjadala naye kwa sura ya maswali mengi, nilimuona
hanipingi sana bali ni kinyume alikuwa anatilia mkazo kuwapenda Ahlul-Bayt (a.s.) na kuwa
kuwafuata na kuzitaja fadhila zao ni lazima.
Na baada ya siku nyingi aliniomba niende kwenye maktaba yake kwenye makao ya chuo na
baada ya kwenda kwake alinipa kitabu chenye juzuu kadha nacho ni (Usul-Kaafiy),
ambacho ni miongoni mwa vyanzo vya Hadithi vinavyoaminika mno kwa Shia. Aliniomba
nisikipuuze kitabu hiki kwa kuwa ni turatha ya Ahlu-Bayt. Sikusema kitu kwa shitukizo kama
hili, nilichukua kitabu na nilimshukuru kwa hilo.
Nilikuwa nakisikia kitabu hiki na sikupata kukiona, ni jambo ambalo lilinifanya nimshuku
kuwa ni Shia Dr. huyu, pamoja na kuwa namtambua kuwa ni mfuasi wa Malik, na baada ya
swali na kutaka tafsiri yake ilinibainikia kuwa yeye ni Sufiy, ni mwenye kujihusisha na
kuwapenda Ahlul-Bayt (a.s.).
Na wenzangu walipotambua maafikiano haya kati yangu na huyu ustadh, waliniomba
nifanye mjadala na ustadhi mwingine aliyekuwa akitusomesha mada ya Hadith, na alikuwa
mtu wa dini sana mnyenyekevu mwenye tabia njema. Na nilikuwa nampenda sana,
nilikubali ombi lao, na ilianza kati yetu mijadala mingi, na nilikuwa namuuliza usahihi wa
baadhi ya hadithi, alikuwa anatilia mkazo kuwa ziko sahihi, na baada ya muda nilihisi
kutopenda kwake na kutoridhika kwake na mjadala wangu, pia wenzangu walihisi hivyo,
hapo niliwaza njia bora ya kuendelea na mjadala ni maandishi.
Hivyo basi nilimwandikia jumla ya Hadithi na riwaya ambazo kwa wazi zajulisha wajibu wa
kufuata madhehebu ya Ahlul-Bayt (a.s.) na nilimwomba atafiti usahihi wake. Na nilikuwa
namuuliza kila siku juu ya majibu, naye hutoa udhuru kuwa hajafanya utafiti. Nilimfuatilia
kwa njia hii mpaka alihisi kuwa namdhiki.
Akaniambia zote ni sahihi. Nikasema kwa kweli ziko wazi zikihusu wajibu wa kuwafuata
Ahlul-Bayt. Hapo hakujibu na aliondoka haraka kwenda maktaba.
Mwenendo huu ulikuwa ni mshitusho kwangu na ni jambo lililonifanya nione ukweli wa usemi
wa Shia. Lakini nilipenda kwenda polepole na kutoharakia hukumu.
Na miongoni mwa ajabu ya tukio la bahati ni kwamba mkuu wa chuo naye ni ustadhi Ulwan,
alikuwa anatusomesha somo la tafsiri, siku moja akasema katika kutafsiri kauli yake ALLAH (s.w.t):
“Kwa kweli Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w) alipokuwa Ghadiir Khum, alinadi kuwaita
watu wakajikusanya, aliushika mkono wa Ali (a.s.) akasema: “Ambaye mimi ni mtawala

wake hivyo Ali ni mtawala wake.”

No comments:

Post a Comment