Friday 13 June 2014

MWEZI WA SHAABANI

BISMILLAHIR-RAHMAANIR-RAHIIM
 Na huu ni mwezi wa Mtume wako bwana wa Mitume wako. Hakika mwezi mtukufu wa Shaaban ni mwezi mtukufu na mkubwa nao ni mwezi wa Mtume wetu Muhammad (s.a.w.w) kwani yeye alisema:  
  
شهر شعبان شهري رحم الله من أعانني على شهري

Mwezi wa Shaabani ni mwezi wangu Mwenyezi Mungu amrehemu mwenye kunisaidia juu ya mwezi wangu huu).

FADHILA ZA MWEZI WASHAABAN
Kuna habari zilizo pokelewa kutoka kwa Mtume mkarimu (s.a.w.w) na pia kutoka kwa maimamu waongofu (a.s) zijulishazo kuwa ubora wa mwezi huu mtukufu na mkubwa ni nyingi  sana na malipo ndani ya mwezi huu ni mara dufu, kwa hakika imekuja na kupolekewa habari kutoka kwa ibnu Abbas ya kuwa amesema: Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w) wakati maswahaba wake walipo kuwa wakizungumzia fadhila za mwezi wa Shaaban mbele yake: Ni mwezi mtukufu, nao ni mwezi wangu, na wabebaji wa Arshi ya Mwenyezi Mungu wanautukuza na wanafahamu haki ya mwezi huu, nao ni mwezi ambao huzidishwa ndani yake riziki za waumini kama ulivyo mwezi wa Ramadhan, na pepo hupambwa ndani ya mwezi huu, …nao ni mwezi ambao kufanya  matendo ndani yake hulipwa mara dufu, jema moja hulipwa kwa wema sabini, na kosa huanguka na kusamehewa, na madhambi hughufiriwa, na mema hukubaliwa, na Mwenye nguvu mwenyezi Mungu alie takasika Huwaelewa ndani ya mwezi huu waja wake, na huwaangali wafungaji  wa mwezi huu na wasimamji kwa ajili ya ibada, na kujifakharisha nao kwa wabebaji wa Arshi)[1].
Na amesema (s.a.w.w): (Shaaban ni mwezi wenye kutwaharisha, na Ramadhani ni mwezi wenye kufuta madhambi, ……na Ndani ya mwezi wa Shaaban huinuliwa matendo ya waja)[2].


No comments:

Post a Comment